GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,709
- 109,144
Ilikuwa ni mida ya saa nane kuelekea saa tisa mchana alasiri ya leo ambapo wapiganaji wetu wanajeshi wa jeshi la ulinzi la Tanzania wakiwa katika mazoezi yao ya nyika au safari ndefu na wakati huo wakiwa wanatoka walikotoka na wanarudi zao kambini Lugalo na Makongo kuendelea na ratiba zao zingine ndipo walipokuwa wanapita kimakundi makundi hapa kilipo chuo cha computer ( kilicho chini ya UDSM ) cha UCC campus ya Mbezi beach hapa Makonde ndiyo katika hali ambayo naiita ni ya kutaka sifa za kijinga kijana mmoja ( mwanafunzi ) huku akiwa amekaa na wenzake akawa anawapiga picha huku akiwarekodi wapiganaji wetu huku akifurahi kama vile anawakejeli na kuwachoresha.
Kilichotokea hapo ni kwamba kijana alikula vibao vya uhakika ambavyo vilimfanya akonde ghafla, kuona haitoshi wakamgaragaza katika matope yaliyopo karibu pale na kuamua kupiga simu kwa mkubwa wao Lugalo ambaye alikuja maeneo ya hapo chuoni kisha wakatokomea na kijana na kilichojiri huko mimi sijui na wala sitaki kujua japo nimeshakihisi nini kilimtokea au kimemtokea.
Wito wangu vijana au wadogo zangu hebu jaribuni basi kujifunza japo kidogo kanuni za hawa wapiganaji wetu na tujitahidi kutumia hizi smartphones zetu kwa umakini mkubwa. Labda kitendo hiki cha wajeda kinaweza kuwa onyo na fundisho kwa wale wengine ambao wamekuwa na tabia za kishobo shobo kama huyu dogo na nashindwa kuelewa mbona watu wote tukiwa tupo maeneo ya kuanzia pale njia panda ya Kawe au daraja lile la Mlalakuwa huwa tunakuwa na nidhamu kubwa na iliyotukuka sasa iweje maeneo mengine huwa hatuheshimu taratibu zao hawa wapiganaji wetu?
Hivi mtu katoka Bagamoyo nyika kwa nyika kwa kutembea na anarudi kambini kujipumzisha tena jua letu hili la Dar likiwa linawachoma halafu wewe kibushuti tu unaleta za kuleta kwanini wasikuzingue? Kwa kiasi fulani nawapongeza wapiganaji wetu ili kuleta nidhamu na kuwa funzo kwa wengine ili jambo hili lisije kujirudia tena.
Kilichotokea hapo ni kwamba kijana alikula vibao vya uhakika ambavyo vilimfanya akonde ghafla, kuona haitoshi wakamgaragaza katika matope yaliyopo karibu pale na kuamua kupiga simu kwa mkubwa wao Lugalo ambaye alikuja maeneo ya hapo chuoni kisha wakatokomea na kijana na kilichojiri huko mimi sijui na wala sitaki kujua japo nimeshakihisi nini kilimtokea au kimemtokea.
Wito wangu vijana au wadogo zangu hebu jaribuni basi kujifunza japo kidogo kanuni za hawa wapiganaji wetu na tujitahidi kutumia hizi smartphones zetu kwa umakini mkubwa. Labda kitendo hiki cha wajeda kinaweza kuwa onyo na fundisho kwa wale wengine ambao wamekuwa na tabia za kishobo shobo kama huyu dogo na nashindwa kuelewa mbona watu wote tukiwa tupo maeneo ya kuanzia pale njia panda ya Kawe au daraja lile la Mlalakuwa huwa tunakuwa na nidhamu kubwa na iliyotukuka sasa iweje maeneo mengine huwa hatuheshimu taratibu zao hawa wapiganaji wetu?
Hivi mtu katoka Bagamoyo nyika kwa nyika kwa kutembea na anarudi kambini kujipumzisha tena jua letu hili la Dar likiwa linawachoma halafu wewe kibushuti tu unaleta za kuleta kwanini wasikuzingue? Kwa kiasi fulani nawapongeza wapiganaji wetu ili kuleta nidhamu na kuwa funzo kwa wengine ili jambo hili lisije kujirudia tena.