Kile kinachoendelea pale ubungo ni UCHAFU si fly over,nimekuwa nikisema kila siku ni mara mia moja lile daraja la mfugale pale Tazara kuliko huu UCHAFU unaoendelea kujengwa pale Ubungo.
Moja wapo ya maendeleo ya miji na majiji ni kupendezesha miji hiyo na majiji hayo kupitia barabara nzuri na majengo mazuri,sasa kila nkifiria kile kinachoendelea pale Ubungo ndo maana nasema ule ni UCHAFU,haiwezekani leo tupo kwenye dunia ya maendeleo na kasi ya kulipendezesha jiji la Dar es salaam tunaenda kujenga ule UJINGA,pale ilipaswa lipigwe flyover la maana ambalo Nchi zote za Afrika Mashariki wangekuja kujifunza bongo,ule ni UCHAFU, UCHAFU, UCHAFU, UCHAFU mpaka Aibu!!,
Nimekuwa nkiongea hili mara nyingi lakini cha ajabu wabongo wengi mapunguani na ambao hawajaona flyover wanashadadia kwamba ni Nzuri.
Ule UCHAFU umejengwa bila plan yeyote na ndo maana ukitaka kuangalia wale ambao wanatokea Kimara,Mwenge kuelekea buguruni,kuna njia wameichimba ili magari yasiguse zile nguzo ambazo ni metre 5.3 au 5.5 kama sijakosea,Hauwezi kuchimba barabara ili kuongeza urefu wa mita kwenda juu kama kweli ilikuwa kwenye Plan.
narudia tena kusema ule ni UCHAFU.
CHIFWINOLOGY²