Sielewi ujenzi unaoendelea Ubungo interchange

Sielewi ujenzi unaoendelea Ubungo interchange

Labda huna utaalamu wa ujenzi, waulize wataalamu watakujibu. Kuna mtu aliuliza hajui kinachoendelea wakati wa ujenzi wa barabara za mwendo kazi, eti wanapwaruza tu na kuharibu barabara. Mwishowe kikatokea kitu cha uhakika na magari yanachapa mwendo. Tulia mwisho wa siku utaona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ilibadili mawazo kuhusu mchoro wa kwanza.
Rejea

Mchoro wa kwanza gharama zilikuwa kubwa sana japo serikali inajitapa ina hela
Yaani hawa jamaa shida sana! Kila kitu ni kunung'unika tu!
 
Kama nitakuwa nimesema uwongo ninaomba radhi kabla. Kinachojengwa sasa hivi Ubungo ni tofauti na kile cha awali. Mwanzoni ilikuwa ni interchange halafu na barabara ilikuwa itoke Ubungo hadi Kibaha. Financing ilikuwa ni partly ya WB na partly fedha za ndani.

Kutokana na sera za Jiwe kukataa kuwafidia waliobomolewa nyumba zao ikiwa ni pamoja na kudharau mazuio ya Mahakama juu ya kuwabomolea wamiliki wa nyumba hizo, WB walijitoa kufadhili kwa kuwa taratibu zinawakataza. Taratibu za WB zinakataza kujuhusisha na mradi wowote unao kandamiza haki za binadamu.

Baada ya hapo Serikali ikaamua kuwa kwa vile "unga hautoshi basi tukoroge uji badala ya kupika ugali" kwa kuwa ingredients ni hizo hizo na sufuria liko jikoni. Ndiyo maana mradi wa barabara unaishia Kibamba, na interchange imekuwa daraja juu ya daraja.

Kama nimekosea naomba radhi
Barabara inaishia kibamba?


Mbona wapo Hadi kiluvya huko?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meko msanii sana yaani ! Mama yangu mzazi aliwahi niambia nikiwa mdogo kuwa"kua mwanangu uyaone"kweli naendelea kushuhudia hizi movie za kikorea
Wanajamvi,naombeni kuuliza,hivi kile kitu kinachojengwa pale ubungo ndo kile kile ambacho Magufuli alituambia watani zake wazaramo tutapiga picha sana pale au kile ni kitu kingine?nisaidieni please mnaojua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajamvi,naombeni kuuliza,hivi kile kitu kinachojengwa pale ubungo ndo kile kile ambacho Magufuli alituambia watani zake wazaramo tutapiga picha sana pale au kile ni kitu kingine?nisaidieni please mnaojua
...It serves the same.
 
Nilikuwa nimesimama sehemu taswira ya interchange ya ubungo ikanijia nikauona utukufu wa awamu ya V kupitia interchange ile,ghafla taswira ya watoto fulani wakiwa darasani wamekaa chini kwa kukosa madawati ikanijia nikahuzunika sana.
 
Back
Top Bottom