Siasa za Mbeya 2005-2010

Mwe mwe mweeee!!!!
Nitamchuna ngozi mtu, siasa za Mbeya zinatisha
 
Siasa za mbeya ndo zilivyo, ukabila ndo msingi mkuu, hata hivyo mmesahau kuwa mtanzania ni gazeti la fisadi rostam, mnategemema liandike lolote zuri kuhusu mwandosya?


Siyo kweli hoja yako ya ukabila. Jimbo hili wananchi wake wote ni Wanyakyusa. Idea yako ya ukabila inatoka wapi? Fikiria kabla ya ku-post
 
 
KIla siku Mbeya tu, jamani si waacheni wananchi washughulikie maendeleo badala ya migogoro kila siku?

Inaelekea kuna watu wanaitumia migogoro ya Mbeya kama miradi ya kisiasa na magazeti.
 
KIla siku Mbeya tu, jamani si waacheni wananchi washughulikie maendeleo badala ya migogoro kila siku?

Inaelekea kuna watu wanaitumia migogoro ya Mbeya kama miradi ya kisiasa na magazeti.

Ni kweli kabisa.Hakuna maendeleo n siasa tu na yote hayo ni Mkuu wa Mkoa na kundi lake
 
HUO NI MRADI WA MWAKIPESILE NA MULLA KULA FEDHA YA EPA

Tatizo la Mkoa wa Mbeya ni ushamba na ulimbukeni wa watu wa Mbeya.

Watu wa Mbeya hawana aibu, ....

fauloo......... umetukana watu

nani mshamba? nani limbukeni? nani hana aibu?

acha hizo
 

Mkuu, Huyo Mwanjala si dereva wa malori, bali ni mfanyabiashara mwenye kumiliki kampuni ya usafirishaji mizigo.
 
Mtanzania umenena ukweli,watu wanafanyia biashara jina la Mbeya. Kila gazeti linaloanzishwa nchini linaangalia soko la habari toka Mbeya. Hivi karibuni mwandishi mmoja alikuwa akitafuta mtu wa kuandikia gazeti moja linaliotarajiwa kuanza kutoka hivi karibu na inadaiwa ni la Jeetu Patel, habari ya kwanza wanataka uchambuzi wa ziara ya JK Mbeya kuhusu zomeazomea ya Mwanjelwa na mawe ya Kanga.

Kazi kubwa ya Wabunge wa kuteuliwa, viti maalumu, wakuu wa wilaya wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa ni siasa na si kuhamasisha maendeleo ya watu wao.

Wilaya ya Kyela imekuwa ya pili kimkoa mwaka huu baada ya jiji katika kufaulisha wanafunzi wa darasa la saba, lakini kuna hatari ya watoto zaidi ya 4,000 kukosa nafasi kutokana na kutokukamilika au kujengwa kwa madarasa. Diwani na WDC yake na DC wako kwenye siasa na hata waliposaidiwa pesa na Mbunge wao bado hakuna kilichofanyika.

Wananchi inabidi kuamka na kuwakataa viongozi wao wanaoendekeza siasa za kijinga zisizo na tija kwao kwani husikii mahubiri ya maendeleo bali nani yuko kwa nani, nani anampinga nani, hatutafika.
 

Acha utoto na ukuwadi, do you think Mwakyembe is what you think
 
Siyo kweli hoja yako ya ukabila. Jimbo hili wananchi wake wote ni Wanyakyusa. Idea yako ya ukabila inatoka wapi? Fikiria kabla ya ku-post



What about Wasafwa, Wandali na makabila ya watu wa Mbozi, Vwawa na kwingineko? Nakubaliana na wewe kuwa tatizo siyo ukabila.
 
Mkuu yani Prof Mwandosya,Prof Mwakusya,Dr.Mwakyembe pamoja na usomi wao uliotukuka bado wanachanganywa na watu wa type ya kina Makamba,Nchimbi au RA?

Mkuu, kwenye politics hakunaga msomi hata sik moja, Ndiyo maana Makamba, darasa la nne anashikilia mpini wa Serikali yote ya ccm. Imagine kunatokea disaster yoyote ile kwa mwenyekiti na makamu, maamuzi makubwa yote ya nchi hii (of course yako chini ya CCM) yatakuwa chini ya MAKAMBA! Unaelewa hilo!
 
What about Wasafwa, Wandali na makabila ya watu wa Mbozi, Vwawa na kwingineko? Nakubaliana na wewe kuwa tatizo siyo ukabila.

Plase ignore this response, I thought we were discussing Mkoa rather than Jimbo.
 


Usiseme hivyo mkuu.Usomi lazima uwepo katika siasa.Unafikiri Makamba angekwenda shule angekuwa anaropoka ropoka hovyo?Hao CCM wenyewe wanasema mgombea wao wa urais lazima awe na elimu ya chuo kikuu.Kwanini wasiseme hata mwenye elimu ya darasa la saba?
Hata huo mpangilio wako siyo wa kikatiba.Kama rais hayupo majukumu yake yatafanywa na Makamu wa rais,kama nae hayupo basi ni Waziri Mkuu(spika?) Makamba hatofanya maamuzi makubwa ya nchi.Hao ma top wa CCM walishaandika ilani ya chama 2005-2010 na jukumu la utekelezaji liko kwa serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…