Siasa za Mbeya 2005-2010

Huyu Mwanakatwe ingefaa apigwe sana maana amezidi kuandika habari za uongo.

Habari zingine zinaandikwa na Dr. Mwakyembe, yeye anaweka jina lake tu na kutuma Nipashe.

Polisi kwanini hawataki kutoa report ya Dr. Mwakyembe kuchomwa kisu? Itabidi tuandamane kuitaka hiyo report.
 

Kwanini nawewe usipigwe sana kwa kurusha majungu JF? Uandamane na nani?
 
Ni upuzi mtupu kumpiga vita aliyechaguliwa na watu badala ya kumpa nafasi ashindwe mwenyewe. Wamebaki kuumbuliwa kila wanapojaribu kumpiga vita Mwakyembe. Sasa hadhi ya Mwakyembe ni ya kitaifa na sio kiwilaya, ni vipofu tu wasioliona hilo.

Huyo mccm naye ndio nyimbo zao za kila siku. Wanadhani wote wanaowasikiliza ni wajinga. Ukweli watu wanaujua hata kama hawausemi. Kwani alikuwa anafundisha pale na kukaribisha malumbano? Angewapa nafasi kumhoji, labda mtoto wa darasa la sita angemwuliza swali ambalo Mulla huenda asingejibu ila kufoka.

Haifai kujisifia nguo uliyoivaa mwenyewe, waachie wanaokuona wakisifie. Kujifagilia mwenyewe ni kupiga kelele.

Leka
 
.........Habari zingine zinaandikwa na Dr. Mwakyembe, yeye anaweka jina lake tu na kutuma Nipashe.............

Kijana, una uthibitisho wowote usio na mawaa wa madai haya mazito?
 
huyu mulla haeleweki kabisa........anafikiri wanambeya wanaburuzwa kiasi hicho,nina wasiwasi na misimamo yake maana bado anatukumbusha mbali...kwamba haamini kuwa mbeya kuna mgogoro wa kisiasa? mwanzo wa yote ni kati ya jk nas prof.mwandosya na baadae kati ya mwakipesile na dr.mwakyembe baadae kati ya mwakalinga aliepandikizwa kwa pamoja na mafisadi na jk....the chain is very long.Misimamo ya huyu bwana imekaa kisharishari nadhani atakuwa ustadhi huyu,katoka wapi jamani anapofikiri ni shukurani kwa wanambeya rais kuteuwa baadhi ya watumishi........kwake mulla inaingia akilini kumteua presidential candidate na professor wa mawasiliano kutunza mazingira, kwa taarifa yako haya ni matusi makubwa.Siamini kama kaambiwa hivyo na rais........nani kamchagua mtu kama huyu anaeukataa ukweli? Hakuna anaeweza kubisha kuwa jk kautosa mkoa wa mbeya na wanambeya wameshaandika na watamhukumu kwa haki kulingana na matendo yao.........
 
kama kweli mwakyembe anafanya hivyo basi ni vizuri na tutajua mengi.....kwani mbona wana jf kibao wanatumia majina yasiyo ya kwao mifano ni mingi sana jaribu kufuatilia majina mbalimbali utajua......
Kijana, una uthibitisho wowote usio na mawaa wa madai haya mazito?
 
Hilo nalo neno.....hapo napo pana ajenda pana,kuna kitu watu wengi hawajui kuhusu wanambeya,hawa huwa hawamwaamini sana mtu ambaye hawamfahamu na kingine ni kuwa hawaoni sababu ya kuwa na mtu amabae sio mzaliwa wa mbeya wakati wana wasomi lukuki...pengine jk alishauriwa kuhusu hay.......
Hivi mkoa gani mwingine ambapo mkuu wa mkoa ni mzaliwa wa mkoa huo?
 
mzee wewe unaonekana una kyela yako, maana mambo unayoyaeleza hayapo kyela, mimi ni mwanakyela ninamfahamu msanii mwakalinga, ebu muulize mwakalinga degree yake ya kwanza aliposhindwa kuipata bongo baada ya kudisco kwenye chuo kimoja hapa tanzania, akueleze vizuri!!! maana unaonekana humfahamu huyu jamaa.
halafu mbona ajamuuliza mwakipesile? huyo mwanyala aliona mambo magumu na alipoamua kurudi kambi ya mwakipesile hapo ndipo palitokea tofauti, muulize vizuri huyo jamaa.
muulize alipataje nafasi ya kuenda na rais marekani pale rais alipoongozana na wafanyabiashara kwenda marekani? Nafikiri tutawasiliana baada ya uchaguzi, mimi nitakuwa huko kupiga kura mwakani. pia nitakuwepo huko december hii ili tuendelee kuona hivyo unavyolipoti.(Wapambe njaa au wa kutumwa utawaona tu) huu ni mtizamo tu na ufinyu wa kufikiri. mtu makini hawezi kujibu kwa kutumia nguvu kiasi hichi badala ya hoja.
 
Last edited:

Hii nimeipenda saana. Mkuu umesema ukweli mtupu.
 


Duh...Mwakalinga alikwenda na Rais Marekani?au mimi sijakuelewa?mzee fafanua hapo mimi sijakuelewa
 

Mijitu yenye wivu wa kijinga utaiona tu, kazi yao kukimbilia failure moja katika mafanikio 100. Hata kama huyo Mwakalinga ange disco kama unavosema, je hapo alipo sasa amefikaje? Unajua watu wapenda maendeleo wanaangalia yule kafanikiwa vipi ili na wenyewe waige. Mijitu yenye wivu inaangalia yule aliwahi kuteleza wapi ili wacheke na kuridhisha nyoyo zao zilizojaa wivu.

Je nyie ambao hamkudisco mafanikio yenu yako wapi? mmeifanyia nini Kyela na familia zenu zaidi ya kuishia kuogopa hata kurudi kuendeleza kwenu? Huu mji wenu ulikuwa umejaa Wakinga wenye nacho wakati wenyeji wanazagaa tu mjini. Akina Mwakalinga wameuchangamsha, nyie mnaanza kuona wivu.

Mbona huyo mbunge wako aliyekutuma uje ubwabwaje hapa alichemsha form six akaishia kwenda chuo cha uandishi wa habari badala ya UDSM? Je mafanikio yake ya elimu kwasasa tuyapuuze kwasababu tu hakufanya vizuri form six?

Kama Mwakalinga ni msanii,basi nchi hii imejaa wasanii kwa asilimia 99. Inaelekea hata Kyela hukai na nafikiri ndio wale wale mliosoma na kupata elimu nzuri kupitia Kyela na sasa mmekimbilia mijini na mnakuja kwenu kama watalii.

Unaanza hata kuona Mwanjala kwenda na JK USA ni deal kubwa la kuliwekea jungu? Kama hujui kila mfanyabiashara anayeongozana na hawa viongozi huwa amepata hiyo nafasi kwasababu moja ama nyingine. Lazima umheshimu huyo Mwanjala, maana hajasoma kama nyie wengine lakini ana mafanikio kwenye biashara zake anazozifanya. Sisi huku wilayani tunawaona akina Mwanjala kama watu wa kuwaiga, watu waliohangaika kwa kuchapa kazi mpaka wakafika wlipofikia.

Sasa wewe msomi mwenzetu una mafanikio gani hata kwenye kazi yako? Nyie ndio mmeua mashirika yetu na utendaji wenu hata serikalini mbovu kabisa.
 
kasyabone tall

kasyabone tall has no status.
Member
Join Date: Sun Sep 2009
Posts: 29
Thanks: 0
Thanked 7 Times in 6 Posts
Rep Power: 0







IMBOMBONGAFU na Mhandisi,
Muacheni kijana apumuwe kidogo maana yeye bado ni mgeni. Pamoja na ugeni wote naona ana ujasiri wa kushambulia wanyeji tayari ndani ya JF. Ni kijana mdogo bado na hata kazi hajaanza maana anaishi kwa kutunzwa na kaka yake.

Mtanzania, nafikiri ukisoma vizuri huu ujumbe na ule nilikutumia mwanzo, utaona kuwa ni mtu yuleyule. Hata Mwakalinga mwenyewe huwa anamsikia tu na milele hajamuona. Ni mwenyeji wa Mbeya yes, ila ni kule milimani na si Kyela, wewe wafahamu ni wapi.
 
Kasyabone ni watu wa Rungwe hao, no wonder anamtetea mtu wa kwao.

Badala ya kuja na data zake, yeye anakuja kuendeleza umbeya ule ule. Dr kahangaika kweli kweli kutafuta madudu ya Mwakalinga na mpaka sasa kashindwa, ndio maana wanahangaika na sababu za Mwakalinga kuondoka SUA miaka zaidi ya 20 iliyopita.

Leteni hoja juu ya hawa fahari wawili watawezaje kuisaidia Kyela kupambana na ujinga, maradhi na umaskini? Tunajua Mwakalinga sio mbunge lakini kafanya juhudi kubwa kusaidi mashule kwenye ujenzi na vifaa kwa zaidi ya miaka 20 sasa, na pia anatoa ajira kwa vijana. Je Mwakyembe kaifanyia nini Kyela miaka yake yote toka anapata ajira?
 
 

Wewe huijui Kyela, kaa kimya. Wengi wanaopiga kelele kuhusu Mwakyembe hapa sio watu wa Kyela. Hawana uchungu na Kyela zaidi ya kuwa na mtu wa kupigana na akina RA.

Ni kweli Mwakyembe ni jina kubwa kitaifa lakini Kyela tunahitaji mbunge wa Kyela; wa kutatua matatizo ya Kyela.

Mwakyembe kapewa miaka mitano na kashindwa kufanya mabadiliko yoyote Kyela. Alikuwa mbunge wa East Africa na alishindwa hata kusaidia vijana wasome shule, ni mabadiliko gani hayo unayoyaongelea?

Mbunge gani huyo anaenda kununua kisu dukani ili amsingizie kijana kwamba alitaka kumwua?
 
Last edited:
 


eeh haya tupe update zaidi kwa hiyo bwana Mwakyembe hajafanya lolote hapo kwenu kyeala ina maana anafanya nini mjengoni??

Lakini na wewe ni mwanachama hai wa CCM or maana kuna watu mnatumiwa hapa
 
 
Huyu kijana jana aliandika huu ujumbe.

Nikawa na hamu leo ya kuelewa nini ataandika leo. Leo nakuta huu ujumbe.


Yaani nikisoma hapo juu nina uhakika kabisa huyu mwaandishi ni nani. Mhandisi na wengine, huyu dogo ni mbishi kama dagaa. Hata mfanyenye hamtamuweza. Sanasana atakuja hapa kwa jina jingine na kuanza kudai mie ana/ni/wafahamu na atamwaga data zangu/zenu hapa.

Kijana anza upya. Fanya homework yako vizuri. Yaani umeshindwa hata kitu kimoja kuandika alichofanya Mwakyembe zaidi ya kuzunguka kichaka. Kama elimu na shule, hizo si shule za Lowassa?

Sitaki kukupa pressure kwa sasa. Ila data za Mwakyembe zipo na zinasubiri muda mwanana ufike. Kama Mwakyembe angelikuwa MKALI kama unavyomsema, kwa nini unahaha sasa? Hivi unafikiri kukiwa na mechi katika ya Taifa Star na Brazil, wachezaji gani hawatalala? Je kama ni final kati ya German na Argentina, nani watalala? Wapambe wa Mwakyembe msiwe na wasiwasi kama mnavyosema ni kweli kuwa Mwakyembe kafanya mengi Kyela. Yeye ni shujaa wa Taifa na Kyela ikiwa sehemu sasa kwa nini mnahema kama MJUSI aliyebanwa mlangoni? Mechi nzito siyo?
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…