Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
Waungwana wa JF nawasalimu,
Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.
Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.
Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.
Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.
Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.
Nimesoma, nimesikia na kuona kuwa Katibu wa Halmashauri ya Taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Paul Makonda akitoa maagizo kwa Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kumapa miezi sita kuyatekeleza. Makonda alitoa maagizo hayo aliyoyasema kuwa ni ya chama (CCM) huko Dodoma.
Pamoja na nguvu kubwa ya chama tawala (CCM) juu ya Serikali ambayo huundwa na chama hicho, si sawa kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Hata Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa huepuka kumpa maagizo Waziri Mkuu hadharani. Vivyohivyo kwa Makamu wa Rais.
Waziri Mkuu, kichama, ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM; Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa nafasi yake, ni sehemu ya ndani kabisa ya chama. Waziri Mkuu, kiserikali, ni mtendaji mkuu wa serikali na mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni. Hushauriana na Rais hata kwenye teuzi mbalimbali, zikiwamo za Mawaziri.
Kulingana na nafasi ya Waziri Mkuu ndani ya CCM na Serikali, si sawa wala busara kumuagiza hadharani kufanya hili au lile. Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM katika nafasi nilizozitaja, ni kiongozi wetu kitaifa. Tunamheshimu na anapaswa kulindiwa heshima yake. Kumuagiza kwa kumtaja hadharani kunaweza kutafsirika kama kumtweza na kumbagaza.
Waziri Mkuu ana majukumu makubwa na mengi. Anafanya kazi kubwa na nyingi. Anafanya kazi za chama chake-CCM na Serikali yetu. Tumheshimu Waziri Mkuu wetu....asitwezwe kwa mgongo wa chama na maagizo ya chama.