Watanzania wengi hawasomi Katiba ndio maana wanashangaa CCM kumpa maagizo Waziri Mkuu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,290
9,720
Ndugu zangu Watanzania,

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitaka kumficha jambo mtanzania basi wewe weka jambo husika katika mfumo wa maandishi halafu kaa pembeni na utulie tu uone atakachokifanya. Ndio maana namuunga mkono Rais samia aliyesema watanzania wapewe Elimu ya katiba kwa miaka mitatu, japo mimi naona kwa watanzania hawa inapaswa iwe ni miaka minne ya elimu ya katiba ndio wataelewa vizuri.

Nimeshangazwa na watu kushangaa chama cha Mapinduzi kupitia mwenezi wake kutoa maelekezo kwa Waziri Mkuu kumaliza na kutatua changamoto za ardhi ndani ya miezi sita. Napenda kuwaambia kuwa chama ni kikubwa kuliko waziri mkuu na serikali yote kwa ujumla wake.chama kinaweza kuielekeza serikali kufanya jambo lolote lile na serikali inapaswa kutekeleza ndani ya muda husika na kurudisha mrejesho.

Ili mtu ateuliwe na awe waziri mkuu wa Taifa letu ni lazima mtu huyo awe mbunge aliyechaguliwa kutoka jimboni moja kwa moja na siyo kuteuliwa na Rais kupitia zile nafasi kumi,.na ili mtu awe mbunge ni lazima awe mwanachama wa chama cha siasa na awe amependekezwa na chama husika kugombea na kupeperusha bendera ya chama husika katika uchaguzi. Mpaka hapa unaona na kuelewa ni nani mkubwa kati ya chama na waziri mkuu,maana kuufikia uwaziri mkuu ni lazima uwe kwanza mbunge wa kuchaguliwa ambapo ni lazima uwe umetokana na chama cha siasa. Kwa hiyo waziri Mkuu ni mdogo kwa CCM na anapaswa kutekeleza maagizo ya CCM.

Kwa kuelewa zaidi chukua katiba yetu na soma ibara ya 51 ili kuyaelewa vyema haya niliyoandika hapa. Maana naona kuna watu wanafanya kukurupuka na kuropoka sana kutokana na uelewa mdogo wa katiba yetu na kuwa wavivu wa kusoma katiba yetu,wengine ni wasomi lakini wavivu wa kusoma katiba na kuingia kwenye mkumbo wa kuongea vitu pasipo kuelewa katiba inasema nini.

Lakini pia kwa mujibu wa ibara ya 39 ya katiba yetu imeeleza wazi wazi kuwa ili mtu awe Rais wa Taifa letu ni lazima awe mwanachama wa chama cha siasa na awe amependekezwa na chama husika kupeperusha bendera ya chama chake.mpaka hapa unaona pia hata Rais mwenyewe ni mdogo kwa chama na kwamba anapaswa Kufuata ,kutii, kutekeleza na kutimiza maelekezo ya chama chake.kwa hiyo chama kinauwezo wa kumuagiza hata Rais kufanya na kutekeleza jambo lolote lile lenye maslahi kwa Taifa letu na watanzania wote kwa ujumla wake. Maana mtu hawezi kuwa Rais kama hana chama hata kama mtu huyo anapendwa kiasi gani.hatuna mgombea binafsi katika nchi yetu.

Ikumbukwe na kueleweka ya kuwa chama ndicho huunda serikali,lakini katu na kamwe serikali haiundi chama. CCM ndiyo iliyounda serikali na siyo serikali iliyoiunda CCM,kwa hiyo serikali ipo chini ya CCM kwa kutekeleza ilani ya CCM.

CCM Ndio huenda na kupanda majukwaani kuomba kura kwa wananchi na kunadi ilani yake. CCM Ndio hupigwa vumbi,jua na kutoka jasho majukwaani ili kuomba ridhaa ya watanzania kuongoza nchi .kwa hiyo watendaji wote wa serikali wana wajibu wa kutekeleza ilani ya CCM kikamilifu. Na CCM inapaswa kuhakikisha kuwa hakuna uzembe unafanyika na mtendaji yeyote yule wa serikali katika utekelezaji wa ilani yake.hakuna cha nani wala nani linapokuja suala la utekelezaji wa ilani yake, ni lazima iwe kali na mbogo maana ni CCM Ndio itakayokwenda kuulizwa na wananchi imefanya nini katika miaka mitano iliyokuwa imepewa kuongoza Taifa letu.

Kabla ya kulalamika lalamika tuwe tunasoma kwanza katiba yetu ,tuwe tunatafuta kwanza taarifa sahihi,ukweli wa mambo,tuwe watafiti ,tuwe wafuatiliaji wa mambo na siyo kukaririshwa vitu kama makasuku na wapotoshaji .tunahitaji kuwa na utamaduni wa kusoma mambo ili kujenga ufahamu wa mambo mengi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Wakati unatuhabarisha hivyo usisahau kwamba mhasibu unaweza kumpa kazi na akagoma kuachia muamala kama vigezo vya kihasibu havijazingatiwa. Mtu akishakuwa Waziri Mkuu anawajibika kiserikali.
 
Wakati unatuhabarisha hivyo usisahau kwamba mhasibu unaweza kumpa kazi na akagoma kuachia muamala kama vigezo vya kihasibu havijazingatiwa. Mtu akishakuwa Waziri Mkuu anawajibika kiserikali.
Unaelewa msingi wa hoja yangu? Msingi wa hoja yangu upo katika nguvu ya chama kumpa maelekezo waziri Mkuu ambaye ni mtendaji mkuu wa serikali katika kutekeleza jambo lolote lile.kwa kuhakikisha kuwa naye anatoa maelekezo kwa watendaji walio chini yake na wanaohusika na utekelezaji wa maagizo ya chama.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitaka kumficha jambo mtanzania basi wewe weka jambo husika katika mfumo wa maandishi halafu kaa pembeni na utulie tu uone atakachokifanya. Ndio maana namuunga mkono Rais samia aliyesema watanzania

0742-67662
Inawezekana vp mjinga namba moja na shetani wa kuzimu awaone wenzake wavivu?kwa uandishi huu wewe shetani umesoma katiba ipi? Mungu chukua hili lishetani haraka Sana lichome moto liteketee kabisa halifai kuendelea kuwa sehemu ya wananchi
 
Inawezekana vp mjinga namba moja na shetani wa kuzimu awaone wenzake wavivu?kwa uandishi huu wewe shetani umesoma katiba ipi? Mungu chukua hili lishetani haraka Sana lichome moto liteketee kabisa halifai kuendelea kuwa sehemu ya wananchi
Atakuchukuwa wewe uliyelaana katika ardhi hii ya Tanzania na uliyechukizo mbele za Mwenyezi Mungu.
 
Unaelewa msingi wa hoja yangu? Msingi wa hoja yangu upo katika nguvu ya chama kumpa maelekezo waziri Mkuu ambaye ni mtendaji mkuu wa serikali katika kutekeleza jambo lolote lile.kwa kuhakikisha kuwa naye anatoa maelekezo kwa watendaji walio chini yake na wanaohusika na utekelezaji wa maagizo ya chama.
Wewe pimbi unajichanganya. Hakuna asiyejua kuwa CCM ndiyo imeunda serikali, na hakuna anayehoji chama kuiagiza serikali bali ishu ni poyoyo bashite kutoa maagizo kwa Waziri Mkuu,yeye siyo msemaji wa CCM bali ni mwenezi tu,mtendaji mkuu wa CCM ni Katibu Mkuu.

Huyo bashite wako alikurupuka ndiyo maana kaenda kwa PM kuyasawazisha. Hata wewe hapa jukwaani unajipa usemaji wa CCM,unakosea sana na hiyo njaa yako ndiyo maana wenye chama wanakudharau wanakuacha usote tu huku ukipishana na teuzi. Soma job description ya mwenezi utoe tongotongo uache kutujazia takataka zako humu.
 
Wakati unatuhabarisha hivyo usisahau kwamba mhasibu unaweza kumpa kazi na akagoma kuachia muamala kama vigezo vya kihasibu havijazingatiwa. Mtu akishakuwa Waziri Mkuu anawajibika kiserikali.
Hizi ni akili za Somo la Uraia ila siyo uhalisia wa mambo.
 
Wewe pimbi unajichanganya. Hakuna asiyejua kuwa CCM ndiyo imeunda serikali, na hakuna anayehoji chama kuiagiza serikali bali ishu ni poyoyo bashite kutoa maagizo kwa Waziri Mkuu,yeye siyo msemaji wa CCM bali ni mwenezi tu,mtendaji mkuu wa CCM ni Katibu Mkuu. Huyo bashite wako alikurupuka ndiyo maana kaenda kwa PM kuyasawazisha. Hata wewe hapa jukwaani unajipa usemaji wa CCM,unakosea sana na hiyo njaa yako ndiyo maana wenye chama wanakudharau wanakuacha usote tu huku ukipishana na teuzi.
Wewe huwezi kuelewa kitu na mibangi yako hiyo. Makonda alikuwa anazugumza kwa niaba ya chama kwa kupeleka maagizo ya chama kwenda kwa serikali kupitia waziri mkuu. Utaelewa nini wewe wakati kichwani mwako tu ni sifuri bin sifuri.😄😄😄😄 Wewe ni zero brain. Kichwa kitupu.
 
Wewe huwezi kuelewa kitu na mibangi yako hiyo. Makonda alikuwa anazugumza kwa niaba ya chama kwa kupeleka maagizo ya chama kwenda kwa serikali kupitia waziri mkuu. Utaelewa nini wewe wakati kichwani mwako tu ni sifuri bin sifuri. Wewe ni zero brain. Kichwa kitupu.
Huna akili unachojua ni kuandika ujinga tu humu ndiyo maana mamlaka ya uteuzi inakupuuza maandiko yako hayana maudhui zaidi ya uchawa tu. Utasota sana kwa akili matope hizi. Subiri uolewe tu
 
Huna akili unachojua ni kuandika ujinga tu humu ndiyo maana mamlaka ya uteuzi inakupuuza maandiko yako hayana maudhui zaidi ya uchawa tu. Utasota sana kwa akili matope hizi. Subiri uolewe tu
Wewe kichwa chako ni mzigo uliobeba kama Boga tu maana kichwa lako halikusaidii kufikiri chochote kile
 
Kijana unatumia vyema nafasi yako kuhakikisha tumbo litajaa vizuri siku moja , yaweza kuwa wewe ndiyo mvivu wa kusoma kwakuwa hayo uliyosema wananchi wengi wetu tunayajua . Hizi Zama za kusifia na mapambio kaza buti sema wakati ujao weka akaunti namba ya benki ili upate chochote kitu .
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitaka kumficha jambo mtanzania basi wewe weka jambo husika katika mfumo wa maandishi halafu kaa pembeni na utulie tu uone atakachokifanya. Ndio maana namuunga mkono Rais samia aliyesema watanzania

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Oyaaa! Naskia wake wa viongozi mnaanza kuwalipa kiinua mgongo
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitaka kumficha jambo mtanzania basi wewe weka jambo husika katika mfumo wa maandishi halafu kaa pembeni na utulie tu uone atakachokifanya. Ndio maana namuunga mkono Rais samia aliyesema watanzania wapewe Elimu ya katiba kwa miaka mitatu, japo mimi naona kwa watanzania hawa inapaswa iwe ni miaka minne ya elimu ya katiba ndio wataelewa vizuri.


Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Unaandika hoja kuhusu katiba bila kunukuu hata kipengele cha katiba kinachojenga msingi wa hoja yako? Ulisoma wapi wewe mjinga?
Unajua maana ya chama kushika hatamu ? Hiyo ilikwisha 1992 na sasa tunakatiba yenye kufuata misingi ya kidemokrasia?
Wambie waliokutuma huyo MAKONDA WAKO HANA UWEZO ANAOJIPA
 
Unaandika hoja kuhusu katiba bila kunukuu hata kipengele cha katiba kinachojenga msingi wa hoja yako? Ulisoma wapi wewe mjinga?
Unajua maana ya chama kushika hatamu ? Hiyo ilikwisha 1992 na sasa tunakatiba yenye kufuata misingi ya kidemokrasia?
Wambie waliokutuma huyo MAKONDA WAKO HANA UWEZO ANAOJIPA
Acha kukurupuka wewe.ndio maana nimesema sisi watanzania ni wavivu sana kusoma na kuelewa.kwani hujaona hapo nimeweka ibara za katiba katika kujenga hoja yangu? Kwa hiyo ukiwekewa hadi ibara za katiba unataka upewe nini ewe mvivu wa kusoma na kuelewa? Unataka ulishwe na kutafuniwa kila kitu kama kinda la Ndege? Acha ujinga na kulemaza akili yako hiyo mgando.
 
Unaandika hoja kuhusu katiba bila kunukuu hata kipengele cha katiba kinachojenga msingi wa hoja yako? Ulisoma wapi wewe mjinga?
Unajua maana ya chama kushika hatamu ? Hiyo ilikwisha 1992 na sasa tunakatiba yenye kufuata misingi ya kidemokrasia?
Wambie waliokutuma huyo MAKONDA WAKO HANA UWEZO ANAOJIPA
Huyu ni PS kitabu chenyewe cha katiba hajawahi hata kukuiona, yeye anadhani Ilani ya CCM ndiyo katiba ya nchi.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitaka kumficha jambo mtanzania basi wewe weka jambo husika katika mfumo wa maandishi halafu kaa pembeni na utulie tu uone atakachokifanya. Ndio maana namuunga mkono Rais samia aliyesema watanzania

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Toa upuuzi wako....!!
 
Back
Top Bottom