Shy-Rose Bhanji awapa makavu CCM

Shy-Rose Bhanji awapa makavu CCM

Huyu Naye sijui anachujaga maneno kabla ya kuongea, kwa hiyo kosa la magu ni kumkata sio? Je aliyepata badala yake anasemaje kuhusu Magu? Hesabu zingine ni Plus na minus so afikirie zaidi. Yeye anamuuliza magu kama angekatwa ingekuweje je ameshawahi kujiuliza je edo alipokatwa bila huruma na rafiki yake kipenzi alijifikiriaje.
Na anaposema alikuwa anafanyakazi nzuri je ni ipi na ninani alimpa hizo credit
Huyu alianza kuchafua bunge la eala na kuanza kupamvana na wenzie kqa kuvunja sheria..Inawezekana pia mavazi yake hayakuwa na nidhamu..
 
wote waliofanikisha kuiweka awamu hii madarakani mimi binafsi sina huruma nao hata chembe.

badala yake ninajawa na furaha sana ninapoona wanalialia kama huyu c-h-a-n-g-u!!
 
Maelezo yake yanaukakasi kwa mbaaaaaaaliiii.....hebu yasome tena mdau ujionee kaukakasi nilikokaona mimi....
 
Basi kwakuwa anaumia sana na bahati mbaya walimyan'ganya tonge mdomoni, atapewa tena, wameshamsikia...
 
Shy-Rose Bhanji

Imekuwa ni desturi kwa baadhi ya WanaCCM kwamba kila ninapotoa maoni yangu ya kukikosoa chama changu au serikali wamekuwa wananishambulia kuwa ni sababu ya kukosa ubunge wa Afrika Mashariki. Sina chuki ya kukosa ubunge na hii naisema kutoka moyoni. Siku zote nimekuwa mkweli kwamba pale panapotakiwa kukosoa sijasita kufanya hivo na pale panapotakiwa kupongeza sijasita kufanya hivo. Kwa vile ninanyanyaswa sana ni vizuri nilitolee ufafanuzi: Huo ubunge siyo kwamba nilikosa lakini ni kutokana na majungu, fitna na roho mbaya ya baadhi ya watu....vita niliyopigwa ni kubwa sana na Mungu tu ndo anajua. Ni kweli kwamba niliumia sana sana kwasababu sikujua nimemkosea nini Rais Magufuli mtu ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote. Isitoshe kazi yangu ya ubunge niliifanya kwa kujituma na kwa moyo wangu wote. Ulikuwa huniambii kitu pale lilipotajwa jina lake...nilifunga safari mpaka mikoani kumfanyia kampeni kwa pesa zangu mfukoni siyo kwamba anipe cheo, hapana ni kwasababu nilimwamini. Na Naomba niwaulize hivi JK angemkata jina Magufuli baada ya kushinda kura za maoni ndani ya chama angejiskiaje? Hakika angeumia lakini nina imani angemsamehe kama vile mimi nilivomsamehe. Hizi ni nafasi leo zipo na kesho hazipo. Ni sawa na kuja duniani na kesho tunaondoka. Naomba sana sana msininyanyase kwasababu mnaniumiza moyo wangu

Mbona maana binafsi huwa sipendi mambo ya siasa...yaani machungu bado yapo???
 
Unasema amani na utulivu vimepungua halafu uko kwako una chart hahaha unajua maana ya amani na utuluvu kupungua? Huu wasaha wa kujadili na kuchati umeupata kama hakuna amani?
Elewa mahana ya neno " kupungua" . Narudia tena matukio ya utekaji, upoteaji,kupiga risasi hadharani, raia kukimbia nchi kwatishiwa kuuwawa vimeshamiri kipindi cha magufuli.... Ukiwa mbinafsi huwezi kuliona hilo.
 
Huyu Naye sijui anachujaga maneno kabla ya kuongea, kwa hiyo kosa la magu ni kumkata sio? Je aliyepata badala yake anasemaje kuhusu Magu? Hesabu zingine ni Plus na minus so afikirie zaidi. Yeye anamuuliza magu kama angekatwa ingekuweje je ameshawahi kujiuliza je edo alipokatwa bila huruma na rafiki yake kipenzi alijifikiriaje.
Na anaposema alikuwa anafanyakazi nzuri je ni ipi na ninani alimpa hizo credit
Kama Machungu ya Kukatwa najua anayajua Lowasa.Hawa akina Banji hawana lolote.Kama alipata kura nyingi Kwa rushwa kwanini asikatwe?
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Shida si kukatwa na magufuli shida yake ilikuwa ni namna alivyokuwa akiwa kwenye ubunge....alikuwa ni mtu wa skendo za ajabu ajabu tu..hata mimi ningemkata maana alikuwa analiabisha taifa...hata kama alimpigania kwa pesa yake lakini siyo tiketi ya yeye kupewa huo ubunge
Ye alimpigania Magufuli siyo kutoka moyoni Ila alitegemea malipo.Waliompigania Magu ni maskini tu ambao wao hawakuwa na cha kupoteza.Naona watu wanaisoma namba
 
Wanaccm wengi wakishatumbuliwa ndo akili zao zinarejea kichwani kutoka zilipokuwa awali maTT@k0ni.mfano
1.nape nnauye
2.makatibu ccm wilaya waliotumbuliwa
3.Y.Makamba
4.Shyrose
5.prof. mwandosya
6.n.k
 
Hawaja hack account yake?Maana anaandikaga halafu anasema hakuwa yeye, atulie dawa imuuingie si wote Ccm
 
wote waliofanikisha kuiweka awamu hii madarakani mimi binafsi sina huruma nao hata chembe.

badala yake ninajawa na furaha sana ninapoona wanalialia kama huyu c-h-a-n-g-u!!
Kwenye hilo kundi wapo wengi akina Mange Kimambi
Chahali ,Banji na wengine wengi Sasa hivi wanalialia tu
 
CCM ina taratibu zake za kukosoa... Ukitaka kukosoa na iingie kwenye kumbukumbu na upate mrejesho wa kile unachoongelea yakupasa kukosoa kwenye vikao vya kikanuni.

Shyrose ana access na vikao vingi tu, ni kwanini asiende kulalamika huko analalamikia kwenye instagram?
 
Kuna baadhi ya watu wanasoma vizuri.....au wanakuwa na kipaji fulani ....cha kuongoza au kuongea......wanakuwa mashuhuri....... Ila kuna tabia za mtu ambazo ni za asili zinakwamisha maendeleo yako..........1. Ulevi......2.Mahusiano.......3.Majungu......., unapotumwa kazi yoyote ya kuwakilisha nchi yako kumbuka kwamba yale watu wa mataifa mengine wanainangalia nchi yako kupitia kwako...kupitia matendo yako ndio watajua kama wananchi wa nchi fulani ni wastaarabu ama sii wastaarabu....Hakuna wananchi wanaopenda nchi yao iwe inatajwa tajwa kila siku kwa tabia binafsi za mwakilishi mliomtuma awawakilishe"" Huyu dada wakati akiwa mbunge vimbwanga vilizidi kumbe alikuwa bado anautamani??
 
Back
Top Bottom