Shule zinazosemekana kukarabatiwa ni zipi haswa, au ni mtaji wa kisiasa?

Jul 25, 2020
65
125
Hii nimekuwa nikijiuliza sana, ukimsikiliza kiongozi yeyote hasa Mawaziri wa TAMISEMI wanajinasibu kuwa shule zote zimepokea pesa ya ukarabati na wanajinasibu kwa kudai kuwa hakuna shule ambayo haijapata pesa za kujenga madarasa mapya au kukarabati yaliyopo lakini kuna shule kongwe hazijawahi kuguswa kabisa zipo ukipita baadhi ya shule utawaonea huruma hasa sekondari za kata na shule za msingi za vijijini shule zina hali mbaya sana.

Madirisha kama milango na baadhi ya shule madarasa yameshikiriwa na nguzo za miti ili kuta zisianguke ila ni ajabu waziri wa tamisemi na watendaji wake wanasema wamejenga nchi nzima.

Mbaya zaidi ni kila ukijaribu kufuatilia kuwa hizi shule kwanini hazikarabatiwi ukiachana na watoto kukaa chini kwa sababu ya kukosa madawati ila tu hata kupiga sakafu angalau watoto wasikae kwenye mchanga na vumbi au kwenye mawe unaambiwa kuwa hili jambo liache kama lilivyo au wanasema utoe taarifa wewe kama nani.

Nitakuja na taarifa fupi ya research ilofanywa na taasisi fulani na ushahidi kuanzia mwakani maana kuna mahali shule madarasa mengi yamejaa vumbi na watoto wanakaa juu ya mawe na wadau walijaribu kupendekeza kuwa kwanini tusiombe kuitisha harambee ili waalikwe wadau mbalimbali ili wachangie shule angalau ipate mifuko hata 200 ya cement ili angalau vyumba vya madarasa vikarabatiwe.

Ila jambo la ajabu ni kwamba, unaambiwa mbunge au diwani wa eneo husika anakasirika ikionekana kuna mtu nje ya chama amepeleka hata mifuko ya cement bila yeye kuhusishwa na hata ukimhusisha kuwa tukualike kwenye harambee kuchangia ujenzi wa shule kalenda zinakua nyingi na kupiga chenga kwa sababu hawataki kuchangia maendeleo.

Kwa maana kwamba ili mdau yeyote akitaka kufanya jambo lazima wanasiasa hawa wahusike ili nao waonekane wako kwenye chain wapate fagio.

Mbunge yeye kaamua kukaa dar au dodoma ila mtu akianzisha alambee eneo lake kuchangia maendeleo hata kama ni ujenzi wa shule anaonekana adui wa mbunge anataka kupoka jimbo.

Kuna wadau wengi wako nje wanatamani kuchangia maendeleo ila yanakwama kwa sababu ili utoe pesa yako lazima ipitie kwa wanasiasa wapate kujioshea ili waonekane na wao wamehusika hata kama alishasahau kabisa eneo lake.

Kwa mtazamo wangu mambo kama haya yanavunja moyo wadau walio tayari kuchangia maendeleo na kuchelewesha maendeleo pengine kusingekua na huu ukiritimba maeneo mengi sana yangekua na maendeleo hasa kwenye haya maeneo ya shule za watoto zetu.

Kero yangu | mtazamo wangu | mjumbe hauwawi.
 
Kiongozi nchi kubwa hii, na kama mwakilishi wako bungeni ni mtu wa kupiga makofi ahoji asumbui mawaziri basi utaendelea kusikia hivyo hivgo wakati maeneo mengine watu wanafaidi matunda ya nchi

MY TAKE
Mwaka 2025 achana na uyo mbunge wako kwani kuna halmashauri p3sa za miradi ya maendeleo zinapishana kila idara afya, elimu nk
 
Kiongozi nchi kubwa hii, na kama mwakilishi wako bungeni ni mtu wa kupiga makofi ahoji asumbui mawaziri basi utaendelea kusikia hivyo hivgo wakati maeneo mengine watu wanafaidi matunda ya nchi

MY TAKE
Mwaka 2025 achana na uyo mbunge wako kwani kuna halmashauri p3sa za miradi ya maendeleo zinapishana kila idara afya, elimu nk
Asante Sana ila sasa kwanini Wanakua wanawekea uzibe kama Ikitokea Inaitishwa Alambee Huwa wanawaka na pengine kama ni mkuu wa kituo unaitwa ofisi ya Wilaya kuhojiwa kwanini Hujafata Protocol unaonekana unadhalilisha Wilaya nzima kwa shule kukosa madawati na kuwa chakavu Manake Ukiona Vumbi unyamaze kimya Ukitoa Taarifa Ofisi za Wilaya na Wabungs wanakushughulikia Haraka Sana
 
Nenda kwenye shule zilizotajwa na wizara kwamba zimekarabatiwa then uje na ushahidi badala ya kuhoji kiholela hivi. Mwisho wa siku utaonekana kijana wa hovyo.
 
Asante Sana ila sasa kwanini Wanakua wanawekea uzibe kama Ikitokea Inaitishwa Alambee Huwa wanawaka na pengine kama ni mkuu wa kituo unaitwa ofisi ya Wilaya kuhojiwa kwanini Hujafata Protocol unaonekana unadhalilisha Wilaya nzima kwa shule kukosa madawati na kuwa chakavu Manake Ukiona Vumbi unyamaze kimya Ukitoa Taarifa Ofisi za Wilaya na Wabungs wanakushughulikia Haraka Sana
Shule gani hiyo inawekewa kauzibe ili Wananchi wasichangie? Taja jina la Shule,Mkoa,Wilaya ikibidi hata Kata na utuambie hiyo shule ina hali gani kwa sasa ili nasi tukusaidie kupaza sauti
 
Asante Sana ila sasa kwanini Wanakua wanawekea uzibe kama Ikitokea Inaitishwa Alambee Huwa wanawaka na pengine kama ni mkuu wa kituo unaitwa ofisi ya Wilaya kuhojiwa kwanini Hujafata Protocol unaonekana unadhalilisha Wilaya nzima kwa shule kukosa madawati na kuwa chakavu Manake Ukiona Vumbi unyamaze kimya Ukitoa Taarifa Ofisi za Wilaya na Wabungs wanakushughulikia Haraka Sana
Sasa utanzishaje harambee kwenye tasisi ya umma pasipo kufuata utaratibu lazima uongozi ujue, usije enda changsha ndoo za kunawia wakati uwezo wa kununua upo
 
Shule gani hiyo inawekewa kauzibe ili Wananchi wasichangie? Taja jina la Shule,Mkoa,Wilaya ikibidi hata Kata na utuambie hiyo shule ina hali gani kwa sasa ili nasi tukusaidie kupaza sauti
Ajui kuna wahuni wanaitaga watu wachange kisa wanapita na michango
 
Kiongozi nchi kubwa hii, na kama mwakilishi wako bungeni ni mtu wa kupiga makofi ahoji asumbui mawaziri basi utaendelea kusikia hivyo hivgo wakati maeneo mengine watu wanafaidi matunda ya nchi

MY TAKE
Mwaka 2025 achana na uyo mbunge wako kwani kuna halmashauri p3sa za miradi ya maendeleo zinapishana kila idara afya, elimu nk
Kuna Jimbo Kanda ya ziwa Lina mbunge muhindi anajiita mbunge wa vitendo alichobakiza ni kuja na mafuta tu ajilie ndogo maana wananchi ni ze nyumbuz anaonekana Kila baada ya miaka5 akiwa na majembe na chumvi ya mawe hapo ni makofi na vigelegele mixa ahadi mingi kwa Hawa maku
 
Hii nimekuwa nikijiuliza sana, ukimsikiliza kiongozi yeyote hasa Mawaziri wa TAMISEMI wanajinasibu kuwa shule zote zimepokea pesa ya ukarabati na wanajinasibu kwa kudai kuwa hakuna shule ambayo haijapata pesa za kujenga madarasa mapya au kukarabati yaliyopo lakini kuna shule kongwe hazijawahi kuguswa kabisa zipo ukipita baadhi ya shule utawaonea huruma hasa sekondari za kata na shule za msingi za vijijini shule zina hali mbaya sana.

Madirisha kama milango na baadhi ya shule madarasa yameshikiriwa na nguzo za miti ili kuta zisianguke ila ni ajabu waziri wa tamisemi na watendaji wake wanasema wamejenga nchi nzima.

Mbaya zaidi ni kila ukijaribu kufuatilia kuwa hizi shule kwanini hazikarabatiwi ukiachana na watoto kukaa chini kwa sababu ya kukosa madawati ila tu hata kupiga sakafu angalau watoto wasikae kwenye mchanga na vumbi au kwenye mawe unaambiwa kuwa hili jambo liache kama lilivyo au wanasema utoe taarifa wewe kama nani.

Nitakuja na taarifa fupi ya research ilofanywa na taasisi fulani na ushahidi kuanzia mwakani maana kuna mahali shule madarasa mengi yamejaa vumbi na watoto wanakaa juu ya mawe na wadau walijaribu kupendekeza kuwa kwanini tusiombe kuitisha harambee ili waalikwe wadau mbalimbali ili wachangie shule angalau ipate mifuko hata 200 ya cement ili angalau vyumba vya madarasa vikarabatiwe.

Ila jambo la ajabu ni kwamba, unaambiwa mbunge au diwani wa eneo husika anakasirika ikionekana kuna mtu nje ya chama amepeleka hata mifuko ya cement bila yeye kuhusishwa na hata ukimhusisha kuwa tukualike kwenye harambee kuchangia ujenzi wa shule kalenda zinakua nyingi na kupiga chenga kwa sababu hawataki kuchangia maendeleo.

Kwa maana kwamba ili mdau yeyote akitaka kufanya jambo lazima wanasiasa hawa wahusike ili nao waonekane wako kwenye chain wapate fagio.

Mbunge yeye kaamua kukaa dar au dodoma ila mtu akianzisha alambee eneo lake kuchangia maendeleo hata kama ni ujenzi wa shule anaonekana adui wa mbunge anataka kupoka jimbo.

Kuna wadau wengi wako nje wanatamani kuchangia maendeleo ila yanakwama kwa sababu ili utoe pesa yako lazima ipitie kwa wanasiasa wapate kujioshea ili waonekane na wao wamehusika hata kama alishasahau kabisa eneo lake.

Kwa mtazamo wangu mambo kama haya yanavunja moyo wadau walio tayari kuchangia maendeleo na kuchelewesha maendeleo pengine kusingekua na huu ukiritimba maeneo mengi sana yangekua na maendeleo hasa kwenye haya maeneo ya shule za watoto zetu.

Kero yangu | mtazamo wangu | mjumbe hauwawi.
FB_IMG_17018049790764977.jpg
 
Back
Top Bottom