Shule Binafsi za Sekondari zipo hoi

Shule Binafsi za Sekondari zipo hoi

Mdanganywa

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2009
Posts
620
Reaction score
343
Mambo yamebadilika. Miaka sita iliyopita watu walikuwa wanazikimbia shule za serikali wanagombania shule za private.

Hali imekuwa kinyume miaka hii na hasa mwaka huu. Sasa shule za serikali zimefurika wanafunzi wakati sekondari za private zina wanafunzi kiduchu.

Ukizingatia kwamba sekondari za private zina wawekezaji wababaishaji yaani hawaja invest wanategemea mapato kutoka kwenye ada ya wanafunzi.

Sasa kama una wanafunzi hawazidi 20 darasani maana yake hiyo shule inasuasua hata kama wanafunzi wanalipa ada kwa wakati.

Sasa huwa hawalipi kwa wakati na hivyo kuongeza tatizo.

Matokeo yake shule haziendesheki na hata kulipa mishahara walimu ni tabu tupu.

Matokeo yake ni kufeli wanafunzi na shule kukosa mvuto kabisa.

Hali ikiendelea hivi miaka miwli ijayo basi private secondary schools zitafungwa na zitabaki za kanisa tu.
 
Shule za private chache Sana zinazosurvive na ambazo zpo well organised....nyingi zinapumulia mashine , walimu wanakopwa mwanzo mwisho, kuacha hawawez mana wakija huku hata hcho watakosa mana jiwe kafunga .lango la Ajira
 
Upo wapi wewe? Weka idadi katika shule hizo na majina yao!!

Jaribu kutembelea Jitegemee na St Francis utuwekee idadi ya mwanafunzi.
 
Wewe jichekeshe eti unasomeshewa mtoto Bure !!!

Wengi waliokuwa wanasomesha watoto wao private wameshindwa kwa sababu vyuma vimekaza, watu wamefilisika!

Lakini najua baada ya muda watu watasimama tena! huu upepo mbaya utapita!
 
Kweli nimeamini mbwa mpe jina baya Hili jamaa tangu lijibandike jina la "Mdanganywa" kweli linadanganywa! Shule gani ya Private imekosa wanafunzi?
 
Siyo kwelii, we unataka mtoto wako wakimaliza hiyo shule waendee English course tenaa??sisi watoto wetu tunataka wanyosheee moja kwa moja.
 
Shule za serikali zimerudisha hadhi yake,nakumbuka kipindi nasoma Weruweru, enzi hizo shule za serikali zilikua juu sana
 
Kuna ka ukweli hapa.
Hali hii imetokana na wanafunzi wanaopata mikopo ya elimu ya juu ni wale waliosoma shule za Serikali, Pia ukata mkali huku mtaani nao unachangia wazazi kuwaacha watoto wao wasome shule za kata.
 
Pole sana. Hali ngumu ya maisha imefanya wazazi kukosa pesa za kusomesha private kwenye ada kubwa hivyo wengine wamepeleka watoto shule za serikali au za private zenye ada nafuuu.

Kimatokeo kidato cha Pili na cha Nne bado shule binafsi ndiyo zinaongoza. Ninaamini hata matokeo taliyosomewa juzi shule 10 bora za serikali ni ngapi zote kwa darasa la 4, Kidato cha 2 na kidato cha 4? Ukitaka kuleta hoja uwe na data hivyo ungepitia kwanza matokeo toka 2015 ufanye analysis ndiyo uongee.

Na pia bado wako wazazi ambao bado wanaosomesha private bila wasiwasi. Ukiona shule ya private inakimbiwa ujue performance na mazingira ni hovyo. Wanakosomeshewa wajukuu ZANGU watu wanaomba kuhamia na hawaruhusiwi maana ni principle hakuna kupokea wahamiaji. Rudi wafanye short research halafu uje ubadilishe bandiko lako hili.
 
Back
Top Bottom