mimi43
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 411
- 422
Asanteni sana wadau, mnamo wiki chache zilizopita nilikuja hapa kuomba msaada juu ya rafiki angu aliyekuwa na tatizo ambalo mliliita BAWASILI (au HEMORRRHOID kama wengine mlivopenda kuita kwa kitaalamu zaidi).
Lengo ni kuleta mrejesho kuwa aliyekuwa mgonjwa amepona kabisa na amenipa shukrani za kipekee, kwa hiyo nikaona sio vema kubaki nazo mwenyewe hizo shukrani bila kushiriki nanyi. Hii yote ni ule ushauri wenu niliuchukua na kumpatia kama ulivo na yeye alizingatia ipasavyo huku akihimizwa na mimi.
N.B: Mwenye tatizo sio mimi, na mimi ni ME ila mwenye tatizo alikuwa jinsi tofauti na mimi, maana hamkawii kunilazimisha niwe mimi mkidai watu wa-Jf hawaumwi ila ni rafiki zao . AhksanteSana.