Wiki tatu zilizopita, niliandika humu Jamii forums, juu ya kuishauri serikali kufungua mpaka wa Mozambique na Tanzania ( Mto Ruvuma). Ili kuruhusu korosho ya Mozambique kuingia Tanzania, nikaeleza kinaga ubaga sababu ya hoja zangu. Nashukuru wenye mamlaka wamechukua maamuzi, mpaka umefunguliwa, Tena sio kilambo na Mtambaswala, Bali ni Chihanga Newala, ambapo ni eneo sahihi na Karibu hasa na maeneo yanayolimwa korosho. Vijana wengi Leo wanaelekea Mozambique kununua korosho kwa bei poa na kuziketa Tanzania. Ahsante jamiiforums