Ruge Opinion
JF-Expert Member
- Mar 22, 2006
- 1,838
- 707
Hiyo article ya Deitric Muhammad ina mantiki sana. Wengine wanaweza kui-trash lakini anachokisema ndicho kinachotokea. Chumi za nchi za Magharibi zimekuwa imara kwa sababu ya kufyonza kutoka nchi kama zetu. Ujiyo wa China na nchi zingine zinazoitwa "emerging economies" umetikisa mfumo. Matokeo yake ni hizi financial/debt/recession/unemployment crises tunazoziona US na European countries. The cancer is still spreading and is going to get worse. US kwa kujihami itaendelea kuanzisha na kupigana vita kila pembe ya dunia (kama mazoea). Mwisho wa siku vita haitaiimarisha US na mashoga zake bali itawadhoofisha kwa sababu watakuwa wana-misdirect scarce resources. Nionavyo mimi a new world order itazaliwa kutokana na vurugu hizo kama ilivyotokea baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia ambapo US iliibuka kama a new superpower. Siyo ndoto kusema kuwa Vita Kuu ya Tatu ya Dunia inakaribia. Swali ni, je, Afrika itaendelea kuwa uwanja tu wa wababe na wajanja au na yenyewe itakuwa mchezaji? Sioni matayarisho.