Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Tunduma umeiacha wapi kwa hivyo vigezo hapo juu vinavyoihusu Kahama?
 
Sababu wanalala mapema,saa moja unusu,kuondoa stendi pale mjini Kati kumechangia kuua mji wa shinyanga ,hakunaga Tena amsha amsha Kama zamani,
Nilikuwepo juzi yaani hata gharama za maisha kwa mgeni ni rahisi hasa kama upo kwa sababu maalumu, yaani niliuma bodaboda kutoka pale Ushirika kuingia mjini kati ndani kidogo yaani kuna kaumbali kidogo yaani nimetoa buku 5 nikarudishiwa buku 4 wakati kisaikolojia nilikuwa nimejiandaa kuambiwa buku 2
 
Well said,Shy ina hasara imeshamezwa na Mwanza,Kahama na Bariadi/Maswa yaani kitu pekee wamebaki nacho ni ardhi tambarare ya viwanda
 
Hadithi za kufikirika,eti roho ya umaskini...nyie ndo mnaua albino..kwamba Tabora hakuna makazi yenye hadhi kama huko kwingine na kama yapo wanaojenga wametoa wapi pesa?
 
Shinyanga sehemu gani ni kame?
Au ulikuwa umepitiwa ukadhani Igunga ni Shinyanga?

Wanaidharau sana shinyanga kwakuwa wanaoishi ni wasukuma,,,,Shinyanga + wilaya zake zimeenderea kuliko tabora yenyewe na wilaya zake,,,,pengine ata mikoa mingine ndani ya tz na wilaya zake.


Tabora kazidiwa na kahama

Sikonge labda 2ipe wilaya ya kishapu wataendana sawa

Nzega 2ipe maswa

Igunga 2ipe Meatu
 
Rudi kwenye kudesa upya mkuu,Wilaya zenye mzunguko mkubwa wa Pesa Tabora ni Urambo na Kaliua hizo nyingine zinafuatia,pitia tu takwimu za halmashauri husika uone makusanyo ya Ndani
 
Kwanza cha bati kitoe maana hakipo hapo Shai, kwaulivyo kilaza aliekuambia kila mji hujengwa na viwanda nani?
Mbona sasa nyie mmezidiwa na wilaya yenu ambayo viwanda ni vidogo kahama.
Haya sikia nikwambie unaweza ukawa na viwanda ila mzunguko wa pesa ukawa ziro unategemea utaenda wapi.
Tabora hakuna viwanda vingi lakini mbona mji mzuri, maisha yapo fresh sana, vyakula vingi sana nanyie ni mashahidi maana bila kuja kununua huku hamuwezi survive sababu unaijua kuwa shinyanga palisha kuwa Sahara, haya pamoja na kuwa Shinyanga ipo kanda ya ziwa lakini pakame kinoma na sababu niileile ya ukataji miti.
Sasa kama unasema barabara hamsini wakati wenzio hakuna barabara ya vumbi town. Kama ukisikia Toronto jua Tabora {mboka manyema}.
Hakuna viwanda lakini patamu kinyama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shy inategemea kahama siyo tbr acha uwongo
 
Vyote umeongea point kasoro udini.
Acheni vitu hivi, hivi unaushihidi gani kuwa kudorora kwa maendeleo sehemu huchangiwa na uislam?
Acha ujinga mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa mbona mnahama kutwa utafikiri wakimbizi mnakimbia nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…