Shindano la MO Mjasiriamali - fikia ndoto zako

Ashura9

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
739
484
Aise umesikia fursa hii ya shindano kwa wewe ambaye unayependa kuwa mfanyabiashara mkubwa? MO Entrepreneurs Competition ni mradi ulioandaliwa na Mo Dewji Foundation na Darecha Limited ili kutambua na kuendeleza juhudi za vijana wajasiriamali katika kukuza biashara zao hapa nchini Tanzania. Mkurugenzi wa makampuni ya METL na Mwenyekiti wa Mo Dewji Foundation, Mohammed Dewjii ,atawasaidia vijana kufikia ndoto zao kwa kuwapatia mitaji, na ushauri wa namna ya kukuza biashara zao.

Ukitaka kushiriki na kuwa mmoja wa vijana watakaonufaika na fursa hii unaweza kutuma maombi kwa kutembelea tovuti ifuatayo:

www.modewjifoundation.org/mo-entrepreneurs-competition/

Pia tembelea kurasa hizi za mitandao ya kijamii kwa habari zaidi:

Facebook: Mo Entrepreneurs
Twitter Mo Entrepreneurs (@MoEntrepreneurs) | Twitter

SHARE na wengine pia wanufaike na fursa




Chanzo: EATV
 
Back
Top Bottom