Inawezekana.
Ila kinachokuza uchumi ni uzalishaji. Si thamani ya hela.
Tukienda soko la dunia mafuta yanauzwa kwa dola za Kimarekani. Wajapani wanapinunua mafuta kutoka Saudi Arabia wananunua kwa dola za Kimarekani. Hawatumii Japanese Yen au Saudi Riyals.
Dola ya Kimarekani ndiyo hela inayotumika sana katika biashara ya kimataifa.
Sasa kama leo dola moja ni Sh 2500, kesho dola moja iwe nusu Kidaka, basi hiyo Kidaka moja itakuwa inabadilishwa kwa shilingi elfu tano za zamani tu.
Zaidi, kuwa na hela yenye thamani kubwa si automatically kuwa na uchumi mzuri.
China kwa miaka mingi wamejitahidi sana hela yao isipande thamani.
Ndiyo. Nchi inaweza kujitahidi hela yao isipande thamani. Tena wamefanya hivyo mpaka Marekani wamelalamika sana kwamba Wachina wanaishusha hela yao thamani makusudi. Waziri wa Fedha wa Obama Timothy Geithner alilisema hili. Donald Trump amekuwa akilisema hili miaka mingi sana na mpaka leo analisema.
Kwa vipi nchi itake hela yake isipande thamani?
Hela ya nchi ikipanda thamani, kuuza bidhaa za nchi hiyo nje inakuwa vigumu sana. Nitakupa mfano.
Ki hamburger cha Marekani ni rahisi sana kufika $2 Marekani. $2 Marekani kutoa kununua hamburger, na $2 nyingine kutoa kununua juisi ukapata lunch ya kujibana actually umekula mlo cheap sana hapo. Kwa wastani unaweza kula lunch ya $6 na kama unataka kutanua unaweza kufikisha hata $30. Sasa fanya hesabu za mtu wa kawaida bongo ki humburger karibu sh 5,000 na kijuice karibu sh 5,000 nyingine. Hiyo hapo ni very cheap lunch ushaondoa sh 10,000. Comparison nikiendeleza unakuta $6 ni karibu sh 15,000 na $30 ni karibu sh 75,000
Ndiyo maana McDonalds ya Marekani haiwezi kuanzisha franchise Dar na kuuza vitu kwa bei za Kimarekani. Hawatafanya biashara kwa sababu dola ina nguvu sana.
China wanakataa kupandisha Yuan kwa sababu China ni a giant exporter. Moja ya sababu unaona kila kitu ni "Made in China" ni kwa sababu Dola moja ni 6.78 Yuan. Wakiipandisha sana thamani Yuan iwe karibu aubiizidi dollar, watashusha exports uchumi utadorora.
Wao kuuza vitu nje kwa urahisi ni muhimu kuliko thamani ya hela yao kuwa kubwa sana.
Kwa hiyo, kuwa na hela yenye thamani sana kunaweza kuharibu uchumi.
Kinachopandisha uchumi si thamani ya hela, ni uzalishaji na kuuza vitu nje.
Nchi inaweza kuwa na hela ambayo haina thamani sana ikawa na uchumi mzuri kuliko nchi yenye hela yenye thamani sana.
Ila, tatizo letu ni kwamba, tuna hela isiyo na thamani, halafu hatuna uzalishaji wa ku export kwa sana. Hii wanaita "the worst of both worlds". Tunapigwa kwa kuwa na hela isiyo na thamani, halafu tunapigwa tena kwa kukosa uzalishaji.
Tungepigwa kumoja tu kwa kuwa na hela isiyo na thamani wakati upande wa uzalishaji tuko fiti, tungeweza ku revenge kwa kutumia hela isiyo na thamani kuongeza exports kama wanavyofanya China. Mpaka tufanye kuwa na hela isiyo na thamani kutusaidia kiuchumi.
Lakini hatufanyi hivyo. Nchi ambayo ina hela isiyo na thamani halafu haina uzalishaji mzuri, inapata matatizo sana inapoagiza vitu kutoka nje. Kwa sababu hela yake haina thamani. Ikienda kununua dola dola zinakuwa za bei ya juu sana. Ikienda kununua mafuta mafuta yanakuwa ya bei ya juu sana. Na kwa vike haina uzalishaji sana, ikitegemea imports, uchumi unashuka.
Geithner Hints at Harder Line on China Trade
Exclusive: Trump calls Chinese 'grand champions' of currency manipulation
Sent from my Kimulimuli