Shigongo amvaa Tundu Lissu

Shigongo amvaa Tundu Lissu

Njaa nuksi bana usiombe.. Amegeuka leo kuwa pambe na yeye.. Si alisema ccm wamemzurumu huyuu???
 
Shigongo ni msukuma mnafiki sasa kaamua kuwa mpiga debe wa msukuma mwenzake baba Jesca apate kupewa vicent kidogo,njaa mbaya huzaa ukabila
 
Shigongo anajielewa sana. Huyo Lissu hana uzalendo hata chembe. Kabaki kumshangilia Lowassa tu!
Uzalendo upi? Lisu tokea 1998 anapigania haya makinikia iweje useme Hana uzalendo? Bunge la ndiyooo lililipitisha mikataba mibovu magufuli alikuwa ni mmojawapo leo hii kaja na blackmail apige pesa za wazungu kama mkapa mnajidai kumshangilia, kuna nini jipya? Malalamiko yapo tokea siku nyingi sana.
 
Kumbukeni Shigongo ni PhD holder!
PhD za kuiba mitihani kisha kukosa Akili kama Lipumba hazina maana bora kujinadi kuwa ni darasa la saba kama Mbunge wa Geita kuliko kujinadi usomi wakati vichwani hakuna Taaluma wala maarifa kuliko wa darasa la 7.
 
Kwan ni lazima binadamu wote tufikiri sawa??? Kila mmoja anatakiwa kusimamia kile anachokiamin iwe ktk siasa au maisha tu ya kawaida....hvyo sion haja au sabbu ya bwana shigongo kujitesa kujua kwann mh lissu hayupo km wanavyotaka wao.....kina lissu wangesema wawe km kina shigongo wanavyotaka miaka ya 90's bas hata hili la makinikia leo tunaloongelea tusingelijua.....utofaut wa mawazo ni kitu muhimu sana na binafs naamin hta mh rais yapo mambo ambyo akisikia kutok kwa wapinzan mf kwa lissu anayakubali na kujua umuhm wake ila anakubali kimya kimya(kimoyo moyo) ili isionekane kafundishwa au kapewa mwanga na wapinzan....vivyo hvyo ht kwa wapinzan mf huyo lissu najua ypo mambo mh rais anayafnya kimoyo moyo wanaunga mkono ila ni ngumu kuyasema adharani kwasabb ya kuepusha kubweteka kiutendaji lakin pia kichama ni changamoto.....

Ila sio muhim kufoc watu wakuunge mkono pasipo wao kuamua...tena ni bora ichukue mda mrefu kwa mtu kufikilia kuunga mkono mana akisema akuunge mkono au awe upande wako bas jua kua umemshawish vya kutosha na atakupenda zaid than yule mtu anaekurupuka kuunga mkono kitu bila kutafakar kiundan akijapata uelewa akagundua ulidangany bas tambua mtu wa aina hi utampoteza kirahis sana

Kufata mkumbo hakufai bora uwe peke ako ila uwe fresh na unachokiamin
lisu kaanza zamani tokea 1998 kupinga huu wizi wa madini cha ajabu magufuli kaja 2017 kupinga kapewa sifa zote wakati kipindi cha kupitisha mikataba mibovu alikuwa ni mmojawapo wa wabunge wa CCM wasema ndiyooooo...
 
shigongo huyu. kwenye stori ya maisha yake alisema hawezi kua na akaunt kwenye mitandao ya kijamii
 
Lissu niwakuogopwa kama Ukoma
huyu Ni msaliti
unachomuogopea lissu ni nini, kaiba au kafanya nini, wa kuogopa ni hao waliotufikisha hapa mpaka sasa, uozo mfanye nyie mnaopiga na kuwaburuza viwete mnakuja kulaumu lissu, kila iitu ndio ndio, hatimae mnalaumu upinzani, kwani wao ndiobwaliosign uozo mliotufanyia, kajambe huko
 
Shigongo yuko sawa. Kujua sheria na kujua siasa ni vita viwili tofauti sana. Wote tulisikia jinsi Lissu alivyokuwa mwongeaji mzuri kwenye kampeni za Katiba pendekezwa na uchaguzi mkuu. Lakini ni wazi usiopingika kuwa, ukimlinganisha Lissu na DJ ambaye ndiye Mwenyekiti wao utakuta Lissu Hana ubavu wa kumzidi hata Mbowe. Mteueni Lissu akutane na Magufuli 2020 mtaona jinsi VITA YA KUPINGANA NA MAGUFULI HAITAMWACHA LISSU SALAMA 2020.
nikwambie kitu, kijani kupita 2020 lazima roho za watu zipotezwe, na demographic itokee, manake ninavyoona kupita kwa hawa watu 2020 lazima waue na damu imwagike, hivi hivi, tukienda kihalali kijani mbona chali mapema, mtatumia ubabe wenu muue raia hapo mtaingia, omba uhai na uzima na mark my words
 
Binafsi sijawahi kumuheshimu Lissu, namlinganisha na Mchungaji Mtikila....yaani wanalazimisha kusikilizwa na watu hata kama kuna ukweli wao watapinga na kuleta hoja tofauti ili tu wapate watu wa kuwasikiliza. Huyu kijana kajimalizia ushawishi kwa jamii.
 
Mbona anajipendekeza kwa ccm? Mbona amekuwa MTU wa kutafuta kiki kwa mlango wa ccm? Ajipange upya kwani hawezi kumchalenge Lissu
 
Huyu si ndiye alikuwa anaililia CCM imlipe madeni yake. Hawezi kuwa na nongwa nao
 
Shigongo, naye anajaribu bahati yake anaweza kupata chochote.
 
Mfanyabiashara na kada wa Chama Cha Mapinduzi, Erick Shingongo amemnyoooshea kidole Tundu Lissu na kusema anashindwa kuelewa kwanini Mwanasheria huyo amekuwa ni mpingaji wa mambo mazuri na kusema jambo hili linamshushia heshima.

Erick Shigongo amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Facebook na kusema yeye kwanza anapongeza hatua alizochukua Rais Magufuli juu ya sakata la madini na kudai kuwa limekuwa na matokeo chanya kwani kiongozi wa Barrick amelazimika kuja Tanzania na kubembeleza yaishe.

"Namheshimu sana Lissu, sana tu. Ni msomi wa sheria, tena mzuri tu! Lakini namshangaa, nashindwa kumwelewa kwa kitu kimoja kwamba kwa nini hawezi kukubali pale jambo jema linapofanyika? Mimi nadhani ni kujijengea heshima kubwa sana kuonyesha uzalendo pale nchi inapopambana na wizi wa maliasili ambazo hata hao Acacia wenyewe wameukubali, sasa kwa nini Lissu anaendelea kubeza kile kinachofanyika? Hakika hili linamshushia heshima" alisema Shingongo

View attachment 525174
Shigongo asiye na hata MB moj a ya kisheria ya mikataba ya madini anajilinganisha na Lissu nimwambie tu kuwa" tumefika hapa kwa sababu ya ccm,Waliofunga mikataba hii niccm,waliwachagua kuongoza wizara nic ccm Leo wanajivua gamba au wanafunua nyeti zao?


Wizi ,ubadhirifu Wa makada Wa ccm haujaanza leoWaziri Mkuu Mstaafu na Marehemu Ndg Edward Moringe Sokoine akiwa kwenye mkutano Wa ccm(chini ya chama kushika hatamu anasema"


....." Vijana wengi Leo wanamali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka therathini hadi arobaini. Lakini wanaiuliza serikali iwaulize hiyo Mali wameipata wapi,hivi kwa nini mzazi asimuulize mwanae Mali hii umeipata wapi?" 23/10/1983

Aliendelea kuonya zaidi kada huyu

*...ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta kiongozi Wa siasa hana usalama Wa aina yeyote,usalama wake nikuomba kudra za mwenyezi Mungu na wananchi peke take,viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu Siku zao". 26/3/1983

Kipindi hiki kuna chama kimoja ccm hakukuwa na Lisu makosa haya yameendrlea hadi Leo nyumba kuuzwa,Bank kuuzwa,na Viwanda vyetu kuuzwa.Ni tangu hapo hadi leo makosa yanafanywa na wanaccm waliopewa dhamana na wananchi.

Anawezaje Shigongo kuja na hoja dhaifu hizi?

Wakati Mnyika na Zitto anatimuliwa Bungeni ,serikali ya ccm ilikuwa ughaibuni na sasa imetudi kuona tunaibiwa?

Ikiwa kweli ccm imedhamilia ,leteni mikataba Bungeni ya gesi na madini tuone unaowatetea kama watatoka!
 
Back
Top Bottom