Shibuda si riziki CHADEMA

Shibuda si riziki CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Hujui unachokisema maana mawazo yako yanakomea katika mipasho na si ajabu hata kucheza mdundiko! Ungejua anayeongea ni nani ungejua maana ya wachina kutengeneza substandard kwa ajiri yako na waa si mwingine regardless kwenda wewe mwenyewe! Nisingependa kueleza zaidi kwani possibly wewe ni hao mnao tumiwa kama middle woman/man ktk kufanya haya mambo ya kuficha UCHAFU WA HAWA WATU!

= ajili

Mchina hakulazimishi kununuwa chake. Unanunuwa wewe mwenyewe.

Wewe ni nani zaidi ya kuwa"substandard" aka punguani tu mwenginewe? Unanshangaza!
 
Huyu naye anatafuta nitoke vipi. Shibuda kwa Chadema ni kama nyuki wa mashineni au nyoka wa kisimani

sio nitoke vipi hebu reason kwanza allegations hizo kabla hujamuona anataka umaarufu. He is reasonable tujifunze ku weigh mambo.
 
Mimi huwa nina mzarau sana huyu Mzee shibuda, nimropokajisana maranyingi anapopewa nafasi ya kuchangia hoja flani bungeni huwa ni mtu wa kuropoka ropoka maneno yasio na tija huwa simuelewagi kabisa.

Hajielewi, kama chama kinakasoro yeye anasubiri nini kwenda kusiko na kasoro.
 
Mpuuzieni huyu kubwa J,anatafuta cheap popularity,cha msingi asipojiengua mwenyewe msubirini kwenye ubunge msipitishe jina lake,sidhani kama CCM watampokea,hakuna chama kinachoweza ku-take risk ya kuchukua mtu kama Shibida,kwa kauli zake ni kama anataka Zito amfikirie kumuingiza ACT.Zito hawezi kufanya kosa ilo.
 
Sijaelewa anataka Chadema kife au anataka nini?

Hata CCM makini wangependa upinzani uwe na nguvu ili wakikosolewa wanajua jinsi ya kujipanga. Sasa huyu haelewek ni chama gani! Undumilakuwili mbaya kabisa huu?

Labda wewe hujamwelewa ameona alichotendewa zitto sio jambo la kiungwana ndipo aka analyse hizo weaknesses
 
Aha haa! Shibuda na hadithi ya Mbichi Hizi!!
Kichaa akikukuta unaoga mtoni akachukua nguo zako akakimbia; na wewe unatoka mtoni mtupu kumkimbiza au unachutama na kupiga ndulu wasamaria wakurushie kanzu au shuka?! Wahenga walisema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Zitto ana akili na ni mweledi; kateleza ndio; kosa kubwa ndio; lakini sio vibaya kukabiliana na mtu mwenye akili mkabishana ukijua mtafikia mahali mkubaliane japo kutokubaliana; Lakini Shibuda John Magalle; hapana yule ni vumbi tupu! kubishana naye ni kukimbiza kichaa mtoni; ni dwanzi; domo kaya; debe shinda kutika haliachi; wazungu wanasema "Never argue with a fool 'cause people will not notice the difference" baina yako mweledi na mjinga kama JMS!
Mwacheni atambe CDM wanamuogopa; lakini namshangaa! kama CDM wanamuogopa why has he been the first to thrown in the towel kabla hajafukuzwa?! si akae akoma; awatishie; tuone ubavu wake?!
 
Shibuda ni mwepesi kama pamba. Mimi sioni sababu za kutenga muda kushughulika na watu kama hawa. CHADEMA kina mambo mengi ya kufanya.
 
Ndo mkome kuchukua makapi ya Ccm ona sasa

Well said! Kwa Shibuda amesha accomplish mission yake. Muhimu chama kiwe makini hata kama ni kweli kwamba kilianzia chumbani kwa Mzee Mtei kikiweza kujitambua na kubadilika sio ajabu kuamniwa na kupewa dhamana ya kuiongoza nchi. Mawazo mazuri yote huanzia kwa mtu mmoja na baadae kumilikiwa na taifa. Shibuda alitumwa, na kazi yake ni kama kasuku. Ameamua kuimba alichokariri sio vizuri kubishana nae. Na kwa jinsi alivyokariri ni single ya muda mfupi itachuja tu.
 
Nakumbuka hotuba ya Mh. Shibuda pale Jangwani wakati wa kufungua kampeni mwaka 2010,,nikiona na hizi kauli zake za sasa nakubaliana na Zito Zubeir Kabwe kwamba usiwaamini WANASIASA hata wa upinzani......All by all CDM ni kijiwe cha wachaga hilo halitaki tochi wala utafiti wa kina
 
Kwa mara nyingi tena mbunge wa maswa mashariki mhe. John M. Shibuda amesema ninawaomba chadema wanifukuze na mimi kwenye chama cha mzee Edwin mtei nawaomba wafanye hivyo.

Mhe. John shibuda amesema sijawahi kuona katika maisha yangu ya siasa kuona katiba mbovu ya chadema katiba hiyo ni katiba ya familia ya mzee Edwin Mtei na baba mkwe wake freman mbowe.

Mhe. John shibuda amesema wakati naingia chadema sikuisoma vizr katiba ya chama hicho niliisoma tayari nimeshakuwa mbunge baada ya kuisoma katiba ya chadema niliichana na kuchoma moto-

Mhe. Shibuda amesema nilishangaa sana kuona chama hicho kinamilikiwa na familia ya mzee edwin Mtei na mbowe aliyemuoa mtoto wa mzee Mtei mbowe yuko kwa kulinda masilahi ya familia hiyo kwa gharama yeyote.

Mhe. John shibuda amesema baada ya kuona katiba hiyo iko hivyo niliidharau sana katiba hiyo chadema ni chama cha familia ya mzee mtei pia chama cha kikabila asilimia 85 ya Ruzuku inaenda kwenye familia ya Mtei.

Mhe. John shibuda anesema chama hicho sio chama ni chama cha kuweka na kukopa SACCOS hata yalipo sasa makao makuu ya chadema kinondoni nyumba waliyopanga ni nyumba ya mzee Mtei.

Mhe. John shibuda amesema malipo yote ya pango yanaingia kwenya akaunti ya mzee Mtei kila mwisho wa mwezi baadhi ya wanachama hawajui wamevikwa blaketi ni aibu aibu sana.

Mhe. John shibuda amesema hata rafiki yangu Mhe. Zitto kabwe alipotangaza kugombea urai mwaka jana alifuatwa na mumiliki wa chama hicho mzee mtei aliambiwa aache kugombea urais amwachie tena Dk. Slaa.

Mhe. John shibuda amesema hata mhe. Zitto kabwe alipotaka kugombea umwenyekiti wa chadema aliambiwa msaliti wa chama ndio matatizo yaliapoanzia hadi amefukuzwa ndani ya chama kwa kuitwa msaliti.

Mhe. John shibuda amesema tangu chadema ianzishwe na mzee mtei aliyeshika nafasi ya umwenyekiti ni mmoja tu mzee Bob makani hakuna mwingine tena aliyewahi kuwa mwenyekiti ni aibu aibu.

Mhe. John shibuda amesema tangu mzee Mtei akianzishe chama waliowahi kushika nafasi ya mwenyeki ni hao hapo chini-

Angalia hapa chini.


1992-1998 mwenyekiti - edwin Mtei
1998-2003 mwenyekiti -Bob Makani-
2003-2008 mwenyekiti - Freeman mbowe
2009-2014 mwenyekiti - Freeman Mbowe
2015 -2020 mwenyekiti -freeman Mbowe

Mhe. John shibuda amesema uwiano huo unafuatiwa na mhe. Ibrahim Lipumba vinala wa UKAWA hali hiyo ni hatari sana siku ikifika nitawaambia watanzania jinsi chadema ilivyo.

Mhe. John shibuda amesema safari hii tutawakimbiza mchaka mchaka mpaka watanzania wajue ni chama cha ovyo hakifai kuongoza Dola hivi tangu lini chama cha kuweka na kukopa SACCOS kikaongoza nchi ?-

Mhe. John shibuda amesema chama hicho kinaongoza kwa maadamano hakina sera yeyote.

Mhe. John shibuda amesema mumiliki mkuu wa chama hicho ni mzee Mtei huyo hapo chini na baba mkwe wake wako pamoja mbowe ni mlopokaji hana hana uwezo wa kuwa kiongozi-
Asanteni sana-
John Magalle . Shibuda.

Shibuda iwe isiwe lazima uondoke chadema msaliti mkubwa wewe na pia pandikizi kubwa la ccm kafie act huko kwa shoga yako ztto.hatutaki mamluki chadema kama weww na zitto
 
Sijaelewa anataka Chadema kife au anataka nini?

Hata CCM makini wangependa upinzani uwe na nguvu ili wakikosolewa wanajua jinsi ya kujipanga. Sasa huyu haelewek ni chama gani! Undumilakuwili mbaya kabisa huu?
Ukweli utabaki kua ukweli matatizo ya kiuongozi chadema ni makubwa kuliko tunavyofikiria haiwezekani chama kama hiki kua na mfumo wa kifalme eti wote mamluki isipokua wanaotka kaskazini tu?
 
Kama kuna ukweli kuhusu mauaji ya alibino nikwasababu ya wanasiasa wanaofanya ndumba ili wachaguliwe. basi nitakwambia Shibuda ni miongoni mwao maana sielewi mtu kama huyu sijui watu wanamchagua kwasababu gani zaidi yakuwa wamepgwa ndumba.
 
Jinsi alivyoandika tu inaonekana ni kilaza kiasi gani. Anataka apewe promotion. CDM wamefanya vizuri sana kumkaushia. Nafikiri hilo linamtesa sana. Maana kwa akili yake yeye ni Presidential material ........ ndiyo maana alitaka kugombea against Kikwete.

So far amekuwa overlooked kila upande CDM, CCM na hata mtaani. Hiyo imemtesa sana.Kila anachojaribu kufanya, hakuna mtu anayempa attention. Hata magazeti wanajua hilo, hawawezi kuuza with Shibuda's headline!
 
Kwa nini aombe afukuzwe badala ya kujiondoa mwenyewe kama anaona Chadema hakimfai??!!

Mpuuzi sana huyu!
 
Chadema hvi ni kwli kua ili uwe mwenyekiti ni lazima utoke kaskazini?na nikweli kua hakuna mwenye uwezo wa kua mwenyekiti zaidi ya mboe?na hakuna kikomo cha kua mwenekiti na ni kweli huwzi kua mwnyekiti mpaka mtei atake na kweli mliomtendea zitto ni sahihi?
 
huyu mzee shibuda huwa namuona km ana upungufu wa akili, hata hao watu wa maswa waliomchagua kuwa mbunge sijui walimpendea nini, nafikiri labda hawakuwa na chaguo mbadala!

Ni mpumbavu pekee atakaeingia kwny chama fulani bila kusoma katiba ya chama husika....

Ni mwendawazimu pekee atakaesoma katiba ya chama fulani na kuiona haifai halafu akaendelea kubakia ndani ya chama hicho tena kwa miaka mingi!

Chadema walikosea sana kumkaribisha huyu mzee shibuda ndani ya chama, tangu mapema alionekana ccm wamempandikiza aje kukivuruga chama???
hiki chama nilikuwa nakichukia kutokana na ubaguzi wake kumbe kuna mengine maovu makubwa hongera shibuda wewe ni msema ukweli siku zote
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom