Jambo mkuu! Tunaomba utuwekee data za ufisadi katika kanisa tafadhali. Umefanya utafiti wa kina kwamba maaskofu wanapokemea uovu wanabagua watu kwa misingi ya dini? Tupe data za kina kuhusu ajenda yao siri! Kikwete aliposemwa kuwa ni chaguo la Mungu mbona hatukusikia ubishi? Kwa maoni yako hata akiharibu aendelee tu kusujudiwa? Hitimisho lako lingekuwa na utafiti, hiyo hoja yako ingekuwa na mantiki! Lakini hoja hasi zisizokuwa na utafiti wa kina, mara nyingi huwa ni uzushi, udini, umbeya na chuki binafsi. Kuwa mwangalifu kwa kile unachokisema!Mie mwenyewe nawashangaa sana maaskofu badala ya kukemea ufisadi ndani ya makanisa yao ambapo mafisadi wengi ndimo wanamo tokea na wao kuwakumbatia wanamwandama Rais. Hii yaonyesha maaskofu wana ajenda ya siri kwani kipindi cha BWM hatukuwasikia kabisa. Maaskofu fanyeni kazi yakuwafunza mafisadi ndani ya makanisa yenu waache uovu huo, kwani mafisadi wengi ni wakristo.