Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

Jamani kumjadili Shibuda ni kupoteza muda, kwa sisi wengine tunaomfahamu wala hatutii presha, Chadema wameshamtumia shibuda kama yeye alivyoitumia chadema kurudi bungeni, ila kwa sasa aliyeshika mpini ni Chadema, kama wanaweza kumfukuza uanachama inamaana hata ubunge kakosa na kitakachotokea ni uchaguzi wa ubunge kurudiwa na ninauhakika kwa moto ulivyo sasa chadema wakisimamisha mtu anaekubalika watachukua tena jimbo hilo kwa tayari wameshajulikana huko na watu wamebadilika kiukweli, watu kama Shibuda, Mrema, Cheyo ni watu wa kuangalia tu ni wanafiki na wanaangalia maslahi yao binafsi.

Mimi naushauri uongozi makini wa Chadema kuangalia uwezekano wa kisheria kuondoa watu kama shibuda ndani ya chama, hao wapo kwa maslahi ya ccm ili kuanzisha vurugu ndani ya Chadema, au kutoa picha kwamba chadema sio shwari wakati tuliomakini tunafahamu kwamba Chadema wapo imara na wanaelekea kwenye njia sahihi.
 

Mkuu think big and stop this myopic kind of thinking.Hivi kila hoja lazima kuitazama kwa ukabila/udini kwa nini unapenda kufikiri akirahisi hivyo.Kwa mtazamo wangu sioni uhusiano wowote na hayo maoni ya Shibuda,wanaosapport/kupinga na usukuma na uchagga.Labda kamulikuwa na nia ya ku-stir up mjadala
 
hivi wewe na walevi wenzio hua mnakutana wapi?
 

MAGWANDA huwa hawapendi kuambiwa ukweli, wanachama wao na viongozi wao. Hiki si chama ni kikundi cha wahuni wachache wenye maslahi yao binafsi . MAGWANDA si chama wao ni wanaharakati
 
hapa ndio tunapima mwenye hakili timamu na mwenye mtindio wa ubongo
 
Naomba ni shauri kitu kidogo ambacho ni kwa manufaa ya CDM na wapenzi wa Demokrasia, nakubaliana kwa asilimia mia moja kwamba anao uhuru wa kutoa maoni yake na kwamba katika mfumo mzima wa ujenzi hoja za chama hawezi kukidhuru chama kama mambo yake yataonekana hayana maana na hakuna wa kuyashughulikia. Hata hivyo kinyume chake ni hatari zaidi kwa chama. Kumshughulikia kwa kosa ambalo chama hakijafanya maamuzi ya pamoja ni kosa la jinai kisiasa. Kwa nini tunataka Shibuda awe ajenda humo ndani? kwa manufaa ya nani? nimewahi kuona serious bypartisan politics in developed demokracy na nikashuhudia mbung mmoja kwa wakati fulani akipigia agenda ya chama kingine kwa wenzetu it has never been an issue, ndiyo maana ya uhuru mpana wa kutoa maoni kwa wabunge. Iwe marekani au Uingereza chama kimoja kujaribu kulazimisha Wabunge kufanya maamuzi kinyume na maono yao ni kuminya demokrasia. Chama kinahitaji kwaelewesha wabunge wake kusimamia yale ambayo chama kinayapigania ikitokea ana mani tofauti that diffrences must be respected and encouraged by every advocate of freedom of expression.
Hili la Shibuda siyo issue kwa cdm
achana naye
 
Imefika muda sasa Wasukuma kutoka kanda ya ziwa kuachana na CDM chama cha kikanda na kikabila, Shibuda ananyanyashwa kutoka na Usukuma wake angekuwa ametoka kaskazini wala usingesikia maneno yoyote ya kashfa!
Waswahili wansema wasifu wa ndani mara nyingi unaakisi wasifu wanje! Haikosi kabisa hata avatar inashabihiana na kufikiri kwako. Hivi watu wengine mnajisikiaje mnapojenga hoja zanu kwenye udini, ukabila jinsia n.k? By the way, Watanzania wa sasa sio wa jana, wanauwezo wa kuchambua mbichi na mbivu!
 
Siasa ya Tanzania ina mambo ya ajabu sana,kwani alitegemea nini kukiuka msimamo wa chama chake
 
Si kosa kwa Shibuda kueleza mawazo yake na ndiyo maana siku zote tunawaandama wabunge wa CCM kwa kukaa kimya hata pale wanapohisi chama kinatenda ndivyo sivyo!

Lakini nami nitaungana na watanzania wengine kuwa Shibuda si mtu anayestaili kuwa mwakilishi wa watanzania kwa mtizamo wake na matamanio yake. Ebu angalia hii kauli yake " Mimi kwanza naona huo ujira wa ..... (yaani posho) haitoshi na ingepandishwa na kuwa 500,000/= kwa siku"

Je kwa mtu mwenye fikra hizo anastahili kuwa mwakilishi wetu watanzania?
 
Swali la msingi hapa ni je, kufuta posho kupo kwenye Ilani ya uchaguzi ya Chadema?

Kama ndio, Kwanini Shibuda akubali kugombea ubunge kwa kutumia hiyo ilani na kisha kuja kuikana bungeni? Kama ni hivyo anatakiwa kuvuliwa gamba haraka sana.

Ila kama suala hilo halipo kwenye Ilani ya uchaguzi ya CDM basi Shibuda ana haki kabisa ya kutoa maoni aliyo yatoa Bungeni. Na CDM hawatapaswa kumchukulia hatua yoyote kweni ni kawaida kutofautiana kimtizamo. HATA HIVYO, KWA MAONI YAKE YALE HATUFAI KABISA SHIBUDA.
 
Sipendi saaaaana kurudia maneno ila napenda kuwakumbusha tu kwamba............
TULIPOSEMA,
WOTE WALIOTOKA SISIEMU NA KWENDA UPINZANI SI WAPINZANI WA KWELI,
TULIONEKANA TUNATENGENEZA MAJUNGU... TUKAONEKANA TUNAWAPINGA WANAMAPINDUZI,
WALICHOKISAHAU WAPINZANI WA MAONI YETU NI KWAMBA SOTE HATUWEZI KUWA NA UONI SAWA!!
NDIO MAANA WAO WALIONA UJAJI WA WAJAJI WALE NI WA MANUFAA KWA CHAMA NA HALI SISI TULIONA NDIO WAUWAJI WA CHAMA!
NAWAKUMBUSHA TENA SI SHIBUDA PEKE YAKE BALI NI WOTE WALIOTOKA KULE...
WANGALI NA FIKRA NA MAWAZO YA KULEKULE WALIKOTOKA...
KWANI KWA KAWAIDA "MAJI HUWA HAYASAHAU BARIDI"
Ahsanteni sana.
 
Me naona tatizo siyo shibuda,bali ni udikteta wa chadema na mbowe wake! Wabunge wa chadema hata mbowe akiwachukulia wake zao watamshangilia tuuu! Uoga gani huu?
 
It is better kumpoteza shibuda kuliko kuacha taifa kuangamia, CDM ni taifa kuanguka kwa CDM ni kuanguka kwa wanyonge; AFUKUZWE CDM!
 
Nilipotabiri baada ya Uchaguzi...
Si kwamba nilitumia mbinu za KINAJIMU laa hasha...
Nilizitazama akili zetu za kitanzania na ushabiki uliopindukia mipaka tulionao...
nikautazama mustakabali wa kutaka mambo tulionao pasipokuwa na malengo...
ndipo nikahitimisha kwa kuwaelezea miaka mitano hii ya siasa za mageuzi na uchaguzi wa 2010 zitakakopelekea vyama tunavyoita vya mageuzi kuelekea kaburini kama si kubaki mahututi!!
Sishangai na wala haya yanayotokea sasa siyaoni kuwa ya ajabu...
Bado yapo yaliyojificha yanakuja...
KWA SABABU KILA MMOJA ANA MASLAHI YAKE...
WANATUMIANA...
Kila mmoja ana lengo lake... hawafuati malengo ya chama... hakuna anaetaka kumsikiliza mwenzake...
hawasizani bali wanataka kusikiwa...
NDIO MAANA KUNA MAKUNDI kwenye KILA CHAMA!!!
Ngumi tayari! Maneno yanaendelea... MALUMBANO NDIO KWANZA YANASHAMIRI..
Mwaka mmoja tu kasoro baada ya UCHAGUZI!!!!!!!
 
shibuda bi msaliti,
shibuda ni chizi
shibuda si mtu wa kuwa chadema
shibuda hajui siasa za chadema
shibuda haiwezi chadema
sasa shibuda afukuzwe chadema aende kwa mafisadi na wezi wenzake ccm

what has he done this time?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…