Sheria zetu zimeshindwa kuwathibiti matapeli wa ardhi?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
5,406
7,386
Haya ni miongoni mwa "mauozo" machache:

1. Kiwanja kimoja kumilikishwa kwa watu zaidi ya mmoja

2. Wamiliki halali wa rdhi kupokonywa maeneo yao kinyemela

3. Shamba au kiwanja kimoja kuuzwa kwa zaidi ya mtu mmoja.

4. Watu kuuziwa mashamba/viwanja hewa

Wauzaji wa viwanja hewa, kwa mfano, hujitapa kuwa hata wakishtakiwa, kesi itakuwa ya madai na kwamba kesi ya madai haimfungi mtu. Hujidai kuwa hata wakiamriwa na mahakama kurejesha fedha walizotapeli, wanaweza watajipangia kurejesha kwa awamu, na kila awamu itakuwa ni kiasi kidogo sana. Ndiyo kusema, atahakikisha anarejesha kiasi ambacho hakitamwathiri sana (tapeli) na hakitamnufaisha anayelipwa.

Hiyo inatoa picha gani? Sheria ni dhaifu? Hali ikoje kwa nchi zingine kama Rwanda, China na Botswana?
 
Utapeli unaazia juu ukuchini watu wameambiwa wavunje jumba zao ili upite mladi wa leli nao awajalipwa wanazungushwa
 
Haya ni miongoni mwa "mauozo" machache:

1. Kiwanja kimoja kumilikishwa kwa watu zaidi ya mmoja

2. Wamiliki halali wa rdhi kupokonywa maeneo yao kinyemela

3. Shamba au kiwanja kimoja kuuzwa kwa zaidi ya mtu mmoja.

4. Watu kuuziwa mashamba/viwanja hewa
Nchi yenye ardhi ya kutosha, na watu wachache lakini ina migogoro mikubwa ya ardhi.
Na usisahau kesi za ardhi uchukua mpaka miaka 20!
Sasa hivi waziri wa ardhi anapambana yeye kama yeye kutafuta ufumbuzi.
lakini hakuna mfumo wala watumishi wenye kuleta ufumbuzi,zaidi wao ndio wasababishaji.
Sina hakika kama ni moja wapo ya mafanikio ya utawala wa ccm tangu uhuru.
 
Back
Top Bottom