Hapa unamaanisha kama kuna mali yoyote iliyonunuliwa na mwanandoa wa kiume na akawa kaziandikisha kwa majina ya watoto wao bado mali hizo zitatakiwa kugawanywa wakati wa kupeana talaka bila kujali kwamba mali hizo haziko katika majina ya wanandoa wenyewe?Mkuu High Vampire,kwenye ndoa hakuna mali ya mtoto/watoto. Kuna aina mbili za mali: mali binafsi ya mwanandoa na mali ya pamoja ya wanandoa. Hivyobasi,ni busara kuepuka varangati juu ya mali kwa kuweka mali katika mifumo/aina hizo zinazotambulika kisheria.
HakikaHapa unamaanisha kama kuna mali yoyote iliyonunuliwa na mwanandoa wa kiume na akawa kaziandikisha kwa majina ya watoto wao bado mali hizo zitatakiwa kugawanywa wakati wa kupeana talaka bila kujali kwamba mali hizo haziko katika majina ya wanandoa wenyewe?
1. Na je, kama mali hizo ziko katika majina ya watu wengine ambao ni ndugu wa mme na wakati huo nyaraka zikionyesha huyo mme alikuwa ni mlipaji tu aidha kwa kutoa pesa yake mwenyewe au kwa kupewa pesa hiyo na huyo ndugu yake ambaye jina lake linaonekana kwenye hati ya mauziano nako zitatakiwa kugawanywa kwa mtalaka wake?Hakika
Nitakutumia kesho pdfHabarini za mda huu wakuu!
Ninashida na sample ya talaka ya ndoa ya kikristo ambayo imetolewa ma mahaka. Yoyote mwenye sample ya talaka ya namna hiyo naomba anisaidie. Natanguliza shukrani!
Hoja kuu ni je hiyo nyumba ulijenga ukiwa na huyo mwanamke?1. Na je, kama mali hizo ziko katika majina ya watu wengine ambao ni ndugu wa mme na wakati huo nyaraka zikionyesha huyo mme alikuwa ni mlipaji tu aidha kwa kutoa pesa yake mwenyewe au kwa kupewa pesa hiyo na huyo ndugu yake ambaye jina lake linaonekana kwenye hati ya mauziano nako zitatakiwa kugawanywa kwa mtalaka wake?
2. Kuna scenario nyingine ambapo mwanaume alinunua kiwanja na kupewa offer ambayo hadi leo hii imepita miaka minane bado ipo katika jina la mmiliki wa awali lakini wakati wa kuuziana muuzaji alisainishana mkataba wa mauziano na mnunuzi ambaye ni mwanaume. Kiwanja hicho kikaja kuendelezwa kwa kujenga nyumba ambapo mtoa pesa yote ya ujenzi alikuwa ni mwanaume hadi nyumba ikakamilika na hatimaye wanandoa wakahamia na wakaweza kuishi ndani ya nyumba hiyo kwa miaka mitano (bila kubadili jina la umiliki kwenye offer ya kiwanja hicho hadi hii leo na hata hati yenyewe bado). Je, katika mazingira hayo bado mahakamani wanaweza kutaka nyumba iuzwe wakati offer ya kiwanja bado inasomeka katika jina la muuzaji wake na siyo katika jina la mwanandoa wa kiume? Au mwanamke atastahili kupata haki gani hapo?
Wanawezaje kugawana mali wakati kila mmoja alikuwa akiishi kivyake, kwa miaka zaidi ya mitatu bila mke kwenda kwa mumewe ?Mkuu TheMnyonge, ndoa ndiyo msingi wa kutolewa kwa takala na kufanyika mgawanyo wa machumo. Kuna ndoa ya kidini, ya kiserikali na kimila. Kwa ulivyoeleza, hapo hakuna ndoa. Lakini, hapo kuna dhanio la ndoa. Hivyobasi, lazima kutakuwa na mgawanyo wa machumo na matunzo ya watoto ikiwa wataishi na mwanamke.
MAAMUZI ya Mahakama ya Upeo ya Kenya imeonesha njia Kwa waamuzi Wetu wa Tanzania wachukulie MAAMUZI hayo kama authority persuasive.KANUNI YA KUGAWA MALI 50-50 BAADA YA TALAKA HAITATUMIKA TENA! MAHAKAMA YA UPEO
Katika kesi ya talaka, kila mhusika anapaswa kuacha ndoa na mali aliyoipata wakati wa muungano" - Mahakama.
Muhtasari
• Majaji wakuu waliamua kwamba masharti ya Ibara ya 45(3) ya Katiba kuhusu usawa katika ndoa hayaruhusu mahakama yoyote kubadilisha haki za umiliki zilizopo za wahusika.
• Majaji wakuu waliamua kwamba masharti ya Ibara ya 45(3) ya Katiba kuhusu usawa katika ndoa hayaruhusu mahakama yoyote kubadilisha haki za umiliki zilizopo za wahusika.
Wenzi wa ndoa hawana haki ya moja kwa moja ya asilimia 50 ya sehemu ya mali ya ndoa baada ya talaka, Mahakama ya Juu imeamua kusuluhisha mojawapo ya masuala yenye utata katika Sheria ya Familia.
Ikitangaza kuwa kanuni ya 50:50 haitumiki kabisa, mahakama ya juu ilisema kwamba katika kesi ya talaka, kila mhusika anapaswa kuacha ndoa na mali aliyoipata wakati wa muungano ingawa mwenzi anaweza kupata zaidi kulingana na mchango wake katika ndoa na upatikanaji wa mali ya ndoa.
Mahakama ya majaji watano ikiongozwa na naibu jaji mkuu Philomena Mwilu pia ilishikilia kuwa kila mwenzi katika ndoa lazima athibitishe mchango wake katika utajiri wa familia ili kuwezesha mahakama kuamua asilimia inayopatikana kwake katika ugawaji wa mali ya ndoa.
Mahakama ilisema kuwa mtihani wa kuamua kiwango cha mchango wa mhusika ni mojawapo ya msingi wa kesi.
Uamuzi huo unatarajiwa kutoa sura ya ugomvi wa kisheria kati ya waume zao wa zamani na wake wa zamani kuhusu kugawana mali baada ya ndoa zao kusambaratika.
Majaji wakuu waliamua kwamba masharti ya Ibara ya 45(3) ya Katiba kuhusu usawa katika ndoa hayaruhusu mahakama yoyote kubadilisha haki za umiliki zilizopo za wahusika.
Masharti hayo yaliyotajwa kufanya kazi tu kama njia ya kutoa usawa wakati wa kuvunjika kwa ndoa huku kila mhusika akiwa na haki ya kupata mgao wao wa haki wa mali ya ndoa, ilisema mahakama.
Madhara yapo.
1. Let say Bro wako sasa anaamua anataka kufunga ndoa ya kikristo/kiserikali huyo mama watoto anaweza kuweka zuio hivyo ita-delay mchakato au kupelekea huyo bi harusi mtarajiwa na yeye kughafilika na kukataa kabisa kuolewa.
2. Kuhusu talaka. Kisheria talaka hutolewa inapokuwepo ndoa. Kwa maelezo yako hapo juu, hicho kilichopo ni dhana ya ndoa ( presumption of marriage) sasa huyo mama watoto anaweza kwenda mahakamani kuthibitisha uwepo wa dhana ya ndoa. Akifanikiwa kuthibitisha hilo na kuthibitisha mali zilizochumwa kwa pamoja wakati wa hiyo dhana ya ndoa, basi mahakama itaamuru mgawanyo wa mali hizo ufanyike kwa namna itakavyoona inafaa, na pia itatoa amri ya matunzo na custody ya watoto kulingana na mazingira na facts zitakazothibitika.
Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
Kujua km kuna dhana ya ndoa kwanza kusiwe na ndoa.Lakini pili, lazima kuwe na ushaidi utaothibitisha kwamba wawili hao, yaani mwanaume na mwanamke wameisha pamoja kama mume na mke kwa kipindi kisichopungua miaka miwili na watu wanaowazunguka wakawatambua wawili hao kama ni mume na mke.Uwepo wa dhana ya ndoa unathibitishwa kwa vithibitisho kama vipi mkuu?
Nadhani ni case ya D Vs A.. walisema penetration must be full penentration na no need to consider end results...Hivi wanathibitisha vipi kuwa ndoa haipo consummated?