Sheria ya Ndoa inasemaje pale Cheti cha Ndoa kinapokuwa hakijafafanua kama ndoa ni ya mke mmoja au zaidi?

Nyaka-One

JF-Expert Member
Oct 27, 2013
4,315
5,986
WanaJF hasa wajuzi wa sheria ya ndoa nina jambo naomba kupata ufafanuzi.

Majuzi niliona cheti cha ndoa cha mme na mke waliofunga ndoa ya kikristo miaka kadhaa iliyopita.

Kwenye cheti niliona kuna sehemu kimeandikwa ndoa imefungwa kwa madhehebu ya kikristo lakini ile sehemu ambapo cheti kinatakiwa kufafanua kama ndoa ni ya mke mmoja, wawili au zaidi hakuna sehemu mojawapo iliyofutwa kuonyesha kwamba moja kati ya hayo machaguo matatu ndiyo inayotakiwa kubaki.

Kutokana na hali hiyo swali langu linakuja hivi:
Je, kwa mujibu wa sheria ya ndoa ya Tanzania (iliyotungwa na serikali) inatoa mwanya kwa mwanandoa wa kiume aliyefunga ndoa ya kikristo na kupewa cheti cha ndoa (cha serikali) kuoa zaidi ya mke mmoja hasa pale inapotokea kwamba kwenye cheti hicho kwa bahati mbaya au makusudi hakuna sehemu yoyote iliyobainisha kwamba ndoa iliyofungwa na kutajwa kwenye hicho cheti ni ya mke mmoja au wengi?
 
Kile cheti ni kwa ajili ya madhehebu yote hivyo kitajazwa kulingana na matakwa ya dini yako.
 
Alafu kwanini kwenye cheti cha ndoa hawaweki slogan ya NDOA MWISHO KANISANI/MSIKITINI
mbona kwenye bia kuna slogan TINGISHA KAMA IMEKWISHA WEKA NYINGINE
 
Wengine ndoa imekamilika kwa matamshi tu, kumbe ninyi wengine hadi vyeti mnavyo. Mna siri sana
 
Umeshasema ndoa ya Kikristo
Ndoa ya Kikristo ni ya mke mmoja na mume mmoja bila hata hicho kikaratasi kinachoitwa cheti cha ndoa cha Serikali.
Je, hakuna dhehebu lolote la kikristo ambalo linaruhusu ndoa ya mke/wake zaidi ya mmoja?
 
Kutokana na hali hiyo swali langu linakuja hivi:

Je, kwa mujibu wa sheria ya ndoa ya Tanzania (iliyotungwa na serikali) inatoa mwanya kwa mwanandoa wa kiume aliyefunga ndoa ya kikristo na kupewa cheti cha ndoa (cha serikali) kuoa zaidi ya mke mmoja hasa pale inapotokea kwamba kwenye cheti hicho kwa bahati mbaya au makusudi hakuna sehemu yoyote iliyobainisha kwamba ndoa iliyofungwa na kutajwa kwenye hicho cheti ni ya mke mmoja au wengi?
Ndoa iliyofungwa kwa imani nyingine yoyote isiyokuwa Uislamu ama Umila (ikiwa ni pamoja na ukristo) – itadhaniwa kisheria kuwa ni ndoa ya mke mmoja tu – isipokuwa kama kutakuwa na uthibitisho kuwa ni ya wake wengi; Kwa hiyo hata kama hapakukatwa, ila imeandikwa kuwa ni ndoa ya Kikristo, basi itatambuliwa kuwa ni ndoa ya mke mmoja. ISIPOKUWA kama kuna uthibitisho kuwa ni ya wake wengi, mfano mume awe tayari ana ndoa ya kimila yenye mke zaidi ya mmoja kabla ya ndoa hii ya kikristo, kwa mazingira hayo anaweza kusema kuwa japo hapakukatwa popote ila ndoa yake ni ya wake wengi.
 
Back
Top Bottom