Sheria ya kukataza uhusiano wa mali za umma na majina binafsi itungwe

maramojatu

JF-Expert Member
Mar 16, 2012
1,165
1,529
WanaJamiiForums,

Siku za karibuni kumeibuka wimbi kubwa la watu kuwanasibisha viongozi wakubwa wa nchi hasa Mh. Rais Samia na hata Rais aliyetangulia na hela ya bajeti ambayo inatolewa na hazina kuu ya nchi. Hii siyo sawa kabisa kwa maendeleo ya nchi na uwajibikaji.

Hela zinazotoka Hazina zimepitishwa na Bunge na siyo za Mhe. Rais. Pia natamani pia kuwe na sheria inayokataza miradi kupewa jina la viongozi hasa wakiwa hai.

Hii ni sababu ni wajibu wa kiongozi kusimamia miradi na pia Kuna wengi wamefanya kazi mradi ukakamilika. Mfano shule, madaraja etc. Najua hapa kuna watunga sera na sheria wanaweza kulichukua hili.

Asante
 
Back
Top Bottom