Shemeji ananitaka

Shemeji ananitaka

Habari za muda mrefu wana jukwaa. Iko hivi nina rafiki yangu yeye ana mtoto mmoja yaani single mum, sasa ana mwanaume wake. Huyo mwanaume wake kipindi wanaanza mahusiano hata mimi nilikuwa nawaona mpaka sasa wamefikia kama miaka kadhaa ya mahusiano yao.

Huyu mwanaume siyo baba wa mtoto wake, sasa huyu shemeji kuna siku moja alichukua namba yangu nikiwa pale kwa rafiki yangu, yeye rafiki yangu alikuwa jikoni anapika, mimi nilijua kachukua kwa nia nzuri tu awe anakuja ofisini labda kuniungisha.

Sasa tulikuwa tunawasiliana akawa ananiita mke mdogo, mara ananiambia nimzalie mimi namwambia siwezi kufanya hivyo wewe ni shemeji yangu nakuheshimu, anasema kwani kuna ubaya. Mara kuna kipindi anakuja ofisini ananiambia wameachana na rafiki yangu mara warudiane.

Huyu shemeji nimemuona ni mtu wa ajabu sana kwa kitendo cha kunitaka kimapenzi kwani huko kote hajaona wanawake hadi aje kwangu, kwa rafiki wa mtu wake, wanaume hamna haya kabisa.

Mimi sijawahi kumwambia rafiki yangu na nimekata mazoea nao wote wawili, maana rafiki yangu akijua tu nilikuwa nachat na mtu wake atakasirika mno maana ana wivu balaa.
Cc. holoholo
Nomadix
Shemeji umeamua kuleta swala huku wakati tungeweza kumalizana kule mtaani. Hii thread imefanya nimekosa unyumba kwa Anastasia21 leo na kamvua haka ka Daslaam.
Ila wakati unapokea bundles na vizawadi zawadi hukujua kama nitaomba uhifadhi wa muda kwako.

Wembe ni ule ule tu shemeji mpaka unipe
 
Shemeji umeamua kuleta swala huku wakati tungeweza kumalizana kule mtaani. Hii thread imefanya nimekosa unyumba kwa Anastasia21 leo na kamvua haka ka Daslaam.
Ila wakati unapokea bundles na vizawadi zawadi hukujua kama nitaomba uhifadhi wa muda kwako.

Wembe ni ule ule tu shemeji mpaka unipe
Anastasia21 mpe shemeji aache kunisumbua
 
Acha uchoyo dada, mkubalie huyu mwenye nia ya dhati akuwowe.
Nyakati zinakuja utahitaji hata anayepumua tu 😂😂😂 lakini hutampata.
Kumbuka;Majuto ni mjukuu😭
Nina mtu, japo sijui kama atanioa au lah! Ila ningekuwa sina .tungeweza kufanya jambo
 
"Love defies reason" suggests that love is a powerful, often inexplicable emotion that transcends logic and rational thought, meaning it's felt deeply and unconditionally, not just based on observable qualities or reasons". samahani sina lugha rahisi ya kujibu uzi wako lakini angalao unaweza pata jibu kwa hiyo para ya ngeli, wengi inatutokea mpaka romantically unampenda rafiki/shoga wa beloved wife kuliko wife mwenyewe😀
Huyu alikuwa na tamaa zake tu hakuna upendo hapa mkuu
 
Absolutely 100%. Sio heshima hata kidogo lakini pia itamfanya akudharau, anavyokuchukulia sasa na hapo baadae ukimpa itakuwa tofauti and likely akakuuzia kesi kwa rafiki yake kuwa ulikuwa unamtaka kimapenzi muda mrefu.

Kuwa makini my dear
Asante sana, nipo makini mno ndiyo maana nimeacha mazoea naye kabisa
 
Ukute hata wewe ndio ulimuanza na kumuomba namba, kwahiyo umekata mawasialiano na rafiki ili iwe rahisi kuwa na mwanaume wa mwenzio sio! Hizi mambo za kuchukuliana mabwana mnazo sana mabinti wa siku na wala hujakasirika
 
Ukute hata wewe ndio ulimuanza na kumuomba namba, kwahiyo umekata mawasialiano na rafiki ili iwe rahisi kuwa na mwanaume wa mwenzio sio! Hizi mambo za kuchukuliana mabwana mnazo sana mabinti wa siku na wala hujakasirika
Wala haiko hivyo mkuu, sikumuanza ni yeye alinianza, na huyo rafiki nimekata mazoea maana yupo mbali na ana lifestyle yake ambayo ipo tofauti na mimi na vile vile mimi sihitaji mambo ya marafiki kwasasa
 
Habari za muda mrefu wana jukwaa. Iko hivi nina rafiki yangu yeye ana mtoto mmoja yaani single mum, sasa ana mwanaume wake. Huyo mwanaume wake kipindi wanaanza mahusiano hata mimi nilikuwa nawaona mpaka sasa wamefikia kama miaka kadhaa ya mahusiano yao.

Huyu mwanaume siyo baba wa mtoto wake, sasa huyu shemeji kuna siku moja alichukua namba yangu nikiwa pale kwa rafiki yangu, yeye rafiki yangu alikuwa jikoni anapika, mimi nilijua kachukua kwa nia nzuri tu awe anakuja ofisini labda kuniungisha.

Sasa tulikuwa tunawasiliana akawa ananiita mke mdogo, mara ananiambia nimzalie mimi namwambia siwezi kufanya hivyo wewe ni shemeji yangu nakuheshimu, anasema kwani kuna ubaya. Mara kuna kipindi anakuja ofisini ananiambia wameachana na rafiki yangu mara warudiane.

Huyu shemeji nimemuona ni mtu wa ajabu sana kwa kitendo cha kunitaka kimapenzi kwani huko kote hajaona wanawake hadi aje kwangu, kwa rafiki wa mtu wake, wanaume hamna haya kabisa.

Mimi sijawahi kumwambia rafiki yangu na nimekata mazoea nao wote wawili, maana rafiki yangu akijua tu nilikuwa nachat na mtu wake atakasirika mno maana ana wivu balaa.
Cc. holoholo
Nomadix
Ukijilegeza unaliwa kimasihara!
 
Back
Top Bottom