Ndugu wa Jamii,
Poleni sana kwa Msiba wa Mnajimu Mkuu wa Tanzania na Afrika Mashariki,
R.I.P sheikh Yahaya Hussein,
Watanzania tusiwe na tabia ya kufurahia mtu akifa,vitabu vitakatifu vinatufundisha kulia na kuomboleza,na wafiwa,tuachane na tabia/siasa za chuki,sisi watanzania ni wamoja na wapenda amani.
hakuwa na lolote kuhusu ushindi wa CCM. ccm inapendwa na wananzengo (wananchi) na wala si viNGinevyo..!!! CCM Oyeee..!!
Yeah, kesho ni tarehe 21/05/2011
kuwa mpole kaka, madhehebu mengine hayaamini katika kumuombea mtu aliyefariki, kama wewe inawezekana just muombee ila usilazimishe wenzako.
Nyie mnaonekana ni true watz....kuficha ficha mambo ndio maana miwshowe mnaumbuka kwa matatizo.....nakumbuka Uganda miaka ya 80 ilikupambana na AIDS ukifa na ngoma siku ya msiba unatangazwa kabisa.....manumbu kafariki kwa HIV!!!!....
NYIE tz kila mtu anakufa kwa kisukari.....ndio maana mnazidi kuwa maskini wakubwa kwa kuona aibu kuambiana ukweli......
Nani asiejua yahaya alikuwa mchawi,mwongo na mchonganishi kwa watanzania??......vitabu vinatuambia watu wa namna hiyo hawawezi kufika mbinguni.......suala la marehemu hasemwi imeandikiwa wapi? nipe aya
"Natabiri kuwa Kikwete ndiye Rais mpya wa mwaka 2010 na atakayempinga katika chama chake atakufa ghafla. Natabiri ushindi wa Rais Kikwete mwakani utaleta serikali ya mseto Tanzania Bara na Tanzania Visiwani," alisema Shekhe Yahya.
Alisema kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Dk Lawrence Gama, ni ishara ya ushindi mkubwa wa Rais Kikwete katika uchaguzi wa mwakani. Alisema kifo hicho ni ishara kwa Rais Kikwete kushinda kura za maoni na kupata tiketi ya CCM, ili kugombea urais katika muhula wa pili.
Mnajimu huyo pia alitabiri kutokea kwa kifo cha kiongozi mmoja wa zamani wa kitaifa katika kipindi cha ya kati ya sasa na Aprili mwakani.
Kwa mujibu wa Radio 1 breaking news Sheikh Mkuu Issa Bin Simba ni kweli Sheikh Yahaya amefariki leo na atazikwa kesho2peni News zaidi kwa walio karibu makazi ya kwake,maana Mi sijaamini kweli. Mmmmmh!!
Mwehu ni Shehe mchawi Yahaya mlinzi wako na majini yake....We Mwehu nini? ama dunia imekuteka mpaka ukasahau adhabu ya kabri.Hakuna utani wala kicheko kwenye kifo labda kwa mwenda wazimu ka wewe usiye jua madhambi mangapi unayo na nini hatimayako baada ya kifo.Hiyo jeuri ya kutamka haya umeitoa wapi?Nonsense kabisa.
hapana ndugu mtu amefariki lakini bado wanaendeleza siasa badala ya kumuombea hebu tuache ujinga ndugu zanguni tunapoelekea sio kuzuri