Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,079
- 17,138
Askari wa Jeshi la Polisi nchini, wameuzingira Msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni, ambao awali ilidaiwa aliyekuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Omari Kawambwa, angekwenda kuswali Swala ya Ijumaa.
Katika mitandao ya kijamii kulisambazwa taarifa za waumini kujikusanya katika msikiti huo kwenda kufanya ibada na kumwona kiongozi huyo wa kidini aliyesimamishwa siku nne zilizopita.
Sheikh Kawambwa, alisimamishwa uongozi na Baraza la Ulamaa la Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), pamoja na masheikh wengine wawili wa Mkoa wa Singida na Kigoma, kwa tuhuma za ukiukaji wa maadili.
Tofauti na ljumaa nyingine zisizo ndani ya Mwezi wa Ramadhan, Ibada ya leo ilikuwa na idadi kubwa ya waumini kiasi cha wengine kukosa nafasi ndani na wakaswali nje ya jengo.
Soma: Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Walid Omar Kawambwa atenguliwa kwa kukiuka 'misingi' ya Uongozi
Pia, kulikuwepo minong'ono kutoka kwa baadhi ya waumini wakisema wanasubiri kumwona Sheikh Walid kwenye mimbari akitoa neno lolote baada ya hatua zilizochukuliwa dhidi yake.
Hata hivyo, Swala ya Ijumaa ilianza saa 6:30 mchana na Sheikh Walid hakuwa miongoni mwa walioongoza swala wala kuhutubia na hakuwepo.
Chanzo: Mwananchi
Katika mitandao ya kijamii kulisambazwa taarifa za waumini kujikusanya katika msikiti huo kwenda kufanya ibada na kumwona kiongozi huyo wa kidini aliyesimamishwa siku nne zilizopita.
Sheikh Kawambwa, alisimamishwa uongozi na Baraza la Ulamaa la Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), pamoja na masheikh wengine wawili wa Mkoa wa Singida na Kigoma, kwa tuhuma za ukiukaji wa maadili.
Tofauti na ljumaa nyingine zisizo ndani ya Mwezi wa Ramadhan, Ibada ya leo ilikuwa na idadi kubwa ya waumini kiasi cha wengine kukosa nafasi ndani na wakaswali nje ya jengo.
Soma: Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Walid Omar Kawambwa atenguliwa kwa kukiuka 'misingi' ya Uongozi
Pia, kulikuwepo minong'ono kutoka kwa baadhi ya waumini wakisema wanasubiri kumwona Sheikh Walid kwenye mimbari akitoa neno lolote baada ya hatua zilizochukuliwa dhidi yake.
Hata hivyo, Swala ya Ijumaa ilianza saa 6:30 mchana na Sheikh Walid hakuwa miongoni mwa walioongoza swala wala kuhutubia na hakuwepo.
Chanzo: Mwananchi