UJUMBE WA IDD: NINI KIFANYIKE
Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025: Chaguzi nyingi Tanzania zinakamilika kwa amani na umwagaji mdogo na mkubwa wa damu. Hata hivyo, upo uwezekano wa kufanya uchaguzi wa amani pakee. Tunapendekeza ifuatavyo:
1. Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi, Sheria ya Vyama vya Siasa na sheria ya Jeshi la Polisi ni sheria muhimu sana katika kujenga mfumo wa Demokrasia na utoaji haki. Hapa Tanzania sheria hizo zinalalamikiwa na jamii na taasisi mbalimbali. Serikali kupitia 4R za Rais, ilishughulikia kwa kiwango ambacho
hakijaridhiwa na makundi tulioyataja. Wito wetu, tunamuomba mheshimiwa Rais
Samia Suluhu Hassan kukutana na wadau wanaowakilisha wananchi kujadili
malalamiko yaliyopo kabla ya uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
2. Pawekwe kanuni ya kikao maksusi cha wadau kutathmini amani na mustakbali
wa uchaguzi siku 30, kabla ya uchaguzi na kuheshimiwa makubaliano yake.
3. Tume ya uchaguzi isimamie mchakato kwa haki, watu wasinyimwe haki ya
kuchagua na kuchaguliwa kwa makosa madogo madogo.
4. Tume ilinde haki za mgombe ikiwemo ya mawakala wake kupewa haki ya
kuwepo kwa wakati na kushiriki katika kila hatua inayomhusu mgombea.
5. Tume isimtangaze mgombea ambaye hakupata ridhaa ya wananchi. Isifanye
urasimu kumtangaza aliyeshinda (na hasa wa chama cha upinzani).