Sheikh Mkuu Dsm aibua utata Freemason

Sheikh Mkuu Dsm aibua utata Freemason

Naomba kujuzwa,

Kwa hiyo hata kwenye mazishi ya Wakristo, mnapoalikwa hamtakiwi kuhudhuria? Achana kusoma dua, je muislamu haruhusiwi kuhudhuria?

Je, kula vyakula pamoja na vinywaji vilivyoandaliwa pia ni kosa?
Inapaswa kuhudhuria na kula na kunywa vilivyoruhusiwa kisheria
Ila hairuhusiwi kushiriki ktk ibada na hata kumuombea dua
 
Mimi niliwahi kuambiwa na Shehe mmoja kuwa.

Mtume alipoona watu wanapita na maiti akasimama, mmoja akamuuliza "Mbona unasimama na aliyefariki ni kafiri?

Akamjibu maiti haina kosa na inatakiwa kuheshimiwa bila kujali kipindi cha uhai mhusika alikua na imani gani.

Sasa kama aliyekupa uelewa wa Mungu wa kweli hakua na shida kusimama 'kafiri' anapitishwa, kwanini umtenge 'kafiri' huyu?

NB. Sina uelewa mpana wa dini ya kiislamu, Maneno siyo exactly kama niliyoambiwa siku hiyo ila maudhui ni hayo.
Kuheshimu maiti hata kwenda kuzika (kwa wanaume) haijakatazwa ila kumuombea duaa HAPANA, halafu ujue yule ni kiongozi kuna kundi la watu wanafata vile afanyavyo, kama anaingia hadi kanisani huyu anawekwa kwenye kundi la WANAFIKI,
WANAFIKI hawataingia peponi mpaka watubu.
 
Ni muda sasa waislam wa Tanzania kuamka na kutafuta ilmu sehemu mbali mbali kuliko kuwafata hawa mashekh ubwabwa a.k.a wachumia tumbo, a.k.a wanafki.
kila siku wanakuja na vioja vipya.
 
Mpaka sasa hatujui nani yupo sahihi,Ila Binadamu hawezi kuwa hakimu wa Binadamu mwenzako mpaka kwenye mambo ya Imani mpaka utaingia kaburini hakimu mkuu wa yote ni Muumba mwenyewe! Tusihukumiane.....Kumwona binadamu mwenzio ana makosa mengi kuliko wewe sijui Hiyo hesabu kakupa nani?
Una maanisha hata wezi wakiiba tuwaache?
 
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salumu mwishoni mwa wiki iliyopita alizua utata katika kona mbalimbali za kijamii kufuatia kufanya dua maalumu ya kumwombea aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Freemason Afrika Mashariki, marehemu Sir Jayantilal Keshavji ‘Andy Chande’ (pichani).

Tukio hilo lilifanyika Aprili 21, mwaka huu katika Shule ya Sekondari ya Shabani Robert na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi, akiwemo Rais Msaatafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa sanjari na wanafunzi wengine waliowahi kusoma katika shule hiyo.



Sir Andy Chande alifariki dunia, Aprili 7, mwaka huu nchini Kenya kwa maradhi ya presha na kuzikwa katika Makaburi ya Baniani, Makumbusho jijini hapa kwa kuchomwa moto.

Katika enzi za uhai wake, Sir Andy Chande aliwahi kuweka wazi kuwa yeye ni mfuasi na kuhani mkuu wa Jumuiya ya Freemason, jumuiya ambayo inaaminika na baadhi ya watu kwamba iko kinyume na mafundisho ya dini za Kiislamu na Kikristo. Katika tukio hilo la kuwakumbuka waasisi wa shule hiyo, Shehe Alhadi aliongoza dua maalumu kwa upande wa dini ya Kiislamu kwa ajili ya kumwombea marehemu Chande jambo lililoibua mjadala mkubwa.

MSIKIE HUYU

Baadhi ya watu walihoji kuwepo kwa shehe mkuu wa Dar kwenye dua hiyo wakati marehemu alijulikana kuwa ni Freemason ambayo wengi hawaiamini kama ina sera za Mungu. Msikie huyu:

“Mimi binafsi sidhani kama ni sahihi kumfanyia dua mtu ambaye aliwahi kuweka wazi kwamba yeye yupo upande wa kushoto, tena akiwa mwenyekiti na kuhani mkuu wa jumuiya ambayo inaaminika inakwenda kinyume na maadili ya Kimungu,” alisema Kimashi John katika ukurasa wake wa Facebook.

Mbali na mtu huyo, mijadala mingi siku hiyo ilikuwa kuhudhuria kwa shehe mkuu kwenye shughuli hiyo.

Gazeti la Uwazi, baada ya kuyasikia hayo, liliamua kumtafuta Shehe Alhadi mwenyewe ili kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo.
Akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Shehe Alhadi alikuwa na haya ya kusema:

“Katika dua niliyoiomba siku ile hakuna neno nililosema kwamba Mungu aiweke roho ya marehemu Chande mahali pema peponi. Unaweza kusikiliza tena rekodi za ile dua, nilichokifanya ni kumwombea kwa Mwenyezi Mungu amlipe kwa mambo yote aliyoyafanya duniani maana yeye ndiye hakimu wa mwisho.”

Aidha, katika hatua nyingine Uwazi lilipotaka kujua kama alishawahi kumpa elimu ya dini ya Kiislamu, marehemu Sir Chande ikiwa ni pamoja na kumtaka asilimu, Shehe Alhadi hakuwa tayari kulizungumzia hilo zaidi ya kukiri kwamba amekuwa akifahamiana na marehemu kwa muda
mrefu.


Hakuna kosa alilofanya Al Hadi, kamuomba Mwenyezi Mungu amuweke Chandi atakapo kwa aliyoyatenda duniani.

Hata kama angeuombea pepo basi hilo ni ommbi tu na halina aana kuwa atapewa hiyo pepo au la. Hakimu wa mwisho ni Allah.

Mbona wapo "Waislam" wengi sana ma Free MMasons na tunawazika na kuwasalia na kuwaombea pepo, lakini mwisho wa siku? Ni Allah pekee.

Hata mimi nnamuombea kwa Allah Sir Andy Chande awekwe popote anapostahiki.
 
Alikua mtu ila alipinga uwepo wa MUNGU tunayemuabudu.


Hata Ammi yake, ndugu ya baba'ke Mtume wetu, kipenzi chetu, Muhammad Salla Allahu Alayhi Wasalaam, Abu Lahab, alimpinga Mtume na aliupinga Uislam kwa nguvu zake zote, lakini Mtume alikuwa akimuombea atoke kwenye udhalim huo, licha ya kuwa ilikuwa imeshashuka aya kuwa huyo makazi yake ni motoni, surat Al-Masad (Tabatiyada).

Alichofanya Hadi hakina makosa, kamuomba Allah amuweke popote anapostahili, hata mimi nnamuomba Allah amuweke Chande popote anapostahili.
 
Hii mada ni fitna tu ya kuwatenganisha Waislam.

Waislam tuwe makini katika mada kama hizi. Zinatutengenisha.

Tuungane wote na kuona kuwa Sheikh Hadi hana kosa alilolifanya.
 
Hakuna kosa alilofanya Al Hadi, kamuomba Mwenyezi Mungu amuweke Chandi atakapo kwa aliyoyatenda duniani.

Hata kama angeuombea pepo basi hilo ni ommbi tu na halina aana kuwa atapewa hiyo pepo au la. Hakimu wa mwisho ni Allah.

Mbona wapo "Waislam" wengi sana ma Free MMasons na tunawazika na kuwasalia na kuwaombea pepo, lakini mwisho wa siku? Ni Allah pekee.

Hata mimi nnamuombea kwa Allah Sir Andy Chande awekwe popote anapostahiki.
Sikujua kua na wewe ni mnafki kiasi hiki, unajinasibu kuitetea dini humu kumbe hakuna kitu. Hivi hujui nini kua hairuhusuwi kabisa kunyanyua mikono yako kumwombea dua MTU aliyekana uwepo wa Mungu tunayemwabudu? Inategemea anaomba katika mazingira ya kukemia au kutoa support kwa washiriki wa msiba.

Yeye alipewa mwaliko kama kiongozi wa waislam wa mkoa wa Dar, alifika kwa mwaliko huo. Basi angetumia nafasi hiyo kukemea dini kama aliyokua Chande, usiwe mnafki sema alipewa nafasi kama Mani na kwa minajili ipi?
 
Hii mada ni fitna tu ya kuwatenganisha Waislam.

Waislam tuwe makini katika mada kama hizi. Zinatutengenisha.

Tuungane wote na kuona kuwa Sheikh Hadi hana kosa alilolifanya.
Bado na narudia kua unaleta unafki, moto mweusu tii unakuhusu mbele ya Allhah S.W.
 
Wabongo wengi hatuishi katika imani zetu dini uliyozaliwa nayo ndio hiyo hiyo unaing'ang'ania na kutoana macho sijui uelewa mdogo sijui tunakosea wapi, binafsi sir chande alisimamia alisimamia alichokiamini
 
Hata Ammi yake, ndugu ya baba'ke Mtume wetu, kipenzi chetu, Muhammad Salla Allahu Alayhi Wasalaam, Abu Lahab, alimpinga Mtume na aliupinga Uislam kwa nguvu zake zote, lakini Mtume alikuwa akimuombea atoke kwenye udhalim huo, licha ya kuwa ilikuwa imeshashuka aya kuwa huyo makazi yake ni motoni, surat Al-Masad (Tabatiyada).

Alichofanya Hadi hakina makosa, kamuomba Allah amuweke popote anapostahili, hata mimi nnamuomba Allah amuweke Chande popote anapostahili.
Kumuombea mtu akiwa hai ni sawa kabisa huenda ipi siku Mola akamfumbua macho na kuelekea njia inayostahili, ila kumuombea akiwa amekufa hakuna kitu kama hicho,

Kumuomba Mungu amuweke mahala anapostahili sawa je kulikua na ulazima kwa Shekh mkubwa kama yeye kusema chochote kwenye yale mazishi??? analeta taswira gani kwa wanafunzi wake wanaomfuata.

Ni huyo huyo aliashaingia mpaka kanisani kwa kisingizio kua anahubiri amani,

Hatuwezi kufumbia macho jambo hili na kumpongeza, kuna siku atakuja kusema waislam twende kanisan tushiriki dua ya pamoja kuliombea taifa kwa kigezo cha uzalendo.
 
Kumuombea mtu akiwa hai ni sawa kabisa huenda ipi siku Mola akamfumbua macho na kuelekea njia inayostahili, ila kumuombea akiwa amekufa hakuna kitu kama hicho,

Kumuomba Mungu amuweke mahala anapostahili sawa je kulikua na ulazima kwa Shekh mkubwa kama yeye kusema chochote kwenye yale mazishi??? analeta taswira gani kwa wanafunzi wake wanaomfuata.

Ni huyo huyo aliashaingia mpaka kanisani kwa kisingizio kua anahubiri amani,

Hatuwezi kufumbia macho jambo hili na kumpongeza, kuna siku atakuja kusema waislam twende kanisan tushiriki dua ya pamoja kuliombea taifa kwa kigezo cha uzalendo.


Ameombewa awekwe popote anapostahiki, kuna tatizo lipi hapo?
 
Bado na narudia kua unaleta unafki, moto mweusu tii unakuhusu mbele ya Allhah S.W.


Hahahaha, umekuwa na ujuzi wa "ghaib" ambao hata Mtume wetu, kipenzi chetu, Muhammad Salla Allahu Alayhi Wasalaam hakuwa nayo?

Jifunze kuandika vizuri.
 
Sikujua kua na wewe ni mnafki kiasi hiki, unajinasibu kuitetea dini humu kumbe hakuna kitu. Hivi hujui nini kua hairuhusuwi kabisa kunyanyua mikono yako kumwombea dua MTU aliyekana uwepo wa Mungu tunayemwabudu? Inategemea anaomba katika mazingira ya kukemia au kutoa support kwa washiriki wa msiba.

Yeye alipewa mwaliko kama kiongozi wa waislam wa mkoa wa Dar, alifika kwa mwaliko huo. Basi angetumia nafasi hiyo kukemea dini kama aliyokua Chande, usiwe mnafki sema alipewa nafasi kama Mani na kwa minajili ipi?

Wacha porojo wewe, kamuombea awekwe popote anapostahiki kuna kosa lipi?
 
Hahahaha, umekuwa na ujuzi wa "ghaib" ambao hata Mtume wetu, kipenzi chetu, Muhammad Salla Allahu Alayhi Wasalaam hakuwa nayo?

Jifunze kuandika vizuri.
Unaelewa makosa uliyoyafanya kwa makusudi, rudi katubu. Unafki ulioonesha leo nimekusamehe bure tu.
 
Ameombewa awekwe popote anapostahiki, kuna tatizo lipi hapo?
Kwahiyo unataka kusema ndivyo vitabu visemavyo? Mbona huelewi kitu wewe? Huenda nawe ni muumini wa jamii hiyo unayejifichia koti la uislam nisikulazimishe.
 
Kuna mtu anawasema freemanson wakati kiunoni kwake ana hirizi na chale hadi makalioni
 
Back
Top Bottom