Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,827
- 3,569
Sheikh wangu,Ralph...
Kama nilovyokueleza hapo mwanzo ikiwa huamini kuwa EAMWS ilivunjwa kwa kuwa ilikuwa na mipango imara ya kuwanyanyua Waislam mimi siwezi kukulazimisha uamini.
Lakini wahusika wakuu wanajua fika ukweli huu.
Utabakia hivyo hivyo huamini kuwa wapo wanaofaidika na hali hii lakini jua kuwa hutoacha kutusikia sisi tukiwakumbusha viongozi wetu kuhusu dhulma hii na wala si nia yetu kuleta farka katika jamii.
Allah katufunza Waislam kwa onyo kali akitueleza: "Msidhulumu wala msikubali kudhulumiwa."
Historia ya wazee wetu katika kupigania uhuru wa nchi yetu na kuleta haki na kujenga umoja mimi ndiyo niliyoiandika kwa huu mkono wangu unaoandika hapa tena nikiwa kijana wa miaka 30.
Historia hii kwa hofu tu ilifutwa lakini nimeirejesha na kitabu kinakwenda toleo la tano katika miaka 20.
Hakuna yeyote aliyesimama kusema mimi nimesema uongo.
Mimi kwa mkono huu ndiye niliyeweza ku-document historia nzima ya Baba wa Taifa toka siku ya kwanza anatia mguu wake anavuka kizingiti cha nyumba ya marehemu Abdulwahid Sykes nikaeleza yote na vipi alijulishwa kwa Sheikh Hassan bin Ameir na mipango yote iliyopita kote akitembezwa nchi nzima akifikia nyumba za Waislam hadi uhuru ukapatikana mwaka 1961.
Haiyumkiniki mimi kizazi cha wazalendo hawa niwe na haja ya kufarikisha.
Mkono huu ndiyo ulioandika pia kwa masikitiko makubwa yote yaliyotokea baada ya uhuru ya kuandikwa kwa historia ya TANU mwaka 1981 na kwa hofu na khiyana historia hii ikafutwa.
Vipi nikulazimishe uamini haya yote?
Lakini mimi hawa waliounda TANU na kupigania uhuru wa nvhi yetu ni wazee wangu na wengi nimewaona kwa macho yangu na wengine wameniona nikiwa mtoto na kuwajua wazazi wangu.
Hakika mimi na wewe hatuwezi kuwa sawa katika uelewa wa historia hii.
Sina uhakika kama nimefanikiwa kukuonesha tunachotofautiana katika huu mjadala. Ngoja nijitahidi kueleza kwa kifupi.
Nakubaliana na wewe kiasi kikubwa kwa mambo makuu mawili:
- Historical facts unazotoa. Nyingi hazina ubishi, na hakika tunaelimika kusoma kuhusu hayo matukio mbalimbali uliyoeleza katika kitabu chako (nimekisoma chote) yaliyotokea wakati wa harakati za uhuru, na za wahusika wake. Kama mtu alishiriki harakati fulani, hiyo ni fact, haiwezi kubadilishwa ikasemwa hakushiriki. Kama mtu alitoa mchango fulani, haiwezekani kukanusha na kudai hakutoa, hata kama ikikanushwa ukweli haubadiliki ukawa uwongo kwa kuwa kuna watu wamekanusha.
- Vyanzo unavyotumia na kuhakiki taarifa zako vipo, na ni traceable, hata mwingine akifuatilia atahakiki.
Nikupe mfano kwa kunukuu sehemu ya sentensi yako ya kwanza hapo juu. Umesema "..........EAMWS ilivunjwa kwa kuwa ilikuwa na mipango imara ya kuwanyanyua Waislam......." Sentensi hii ina tunachokubaliana na tunachotofautiana.
EAMWS ilivunjwa (hii ni fact, tunakubaliana) kwa kuwa ilikuwa na mipango imara ya kuwanyanyua waislam (hapa tunatofautiana. Ushahidi wa hili uko wapi?) Hao waliovunja hiyo taasisi walitoa sababu gani, na je hizo sababu zina ukweli au uongo gani? (kwa ushahidi). Je taasisi nyingine zilizokuwa zinawanyanyua waislamu nazo zilivunjwa, au hazikuwepo? Waislamu walikatazwa au kuzuiwa kuunda taasisi nyingine yenye malengo yaleyale ya kuwanyanyua waislamu?
Hiyo conclusion ya kuhusu sababu ya kuvunjwa kwa taasisi hiyo huna data za kuithibitisha.
Kwa hakika nakusifu kwa uandishi mzuri wa kiswahili na kiingereza, na nimekusikia ukizungumza lugha zote mbili kwa umahiri kabisa. Simulizi zako kuhusu yaliyotokea na yalivyotokea hazipingwi kwa kuwa kwa kiasi kikubwa ni za kweli. Kwenye zile za "What happened, when, where, by who and how" uko vizuri. Tatizo liko kwenye "why", hapo ndipo unapotuingiza chaka mzee wangu.