Hapo kwenye red wana agenda gani Kenya??
Kuhusu swala la serikali na dola kutumia tishio la Al Shaabab kama sababu ya kutisha na kuogopesha watanzania binafsi siliafiki na nina muunga mkono Sheikh Ponda kuhusiana na hilo, Ila;
Je, ni sahihi Sheikh Ponda kuhusishanisha uislamu na Al shabaab??
Je, anayepinga mashambulio ya Al shabaab anaupinga uislam???
Je, waislamu wanaowakilishwa na Sheikh Ponda wanaridhia kuwa fedheha dhidi ya Al Shaabab ni fedheha dhidi ya waislamu???
25 NOVEMBER 2011
Na David John
KAMATI ya Kutetea Haki za Waislamu nchini, imeihadharisha Serikali kutojihusisha na mambo ya kidini hasa yanayohusu kundi la Al-shaabab kwa shinikizo la mataifa makubwa.
Katibu wa kamati hiyo, Shekhe Ponda Issa Ponda, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema kamati hiyo imemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Shamsi Vuai Nahodha, kupinga kauli yake aliyowataka Watanzania kuwa makini na wahamiaji haramu ili kudhibiti kundi hilo lisiingie nchini.
Shekhe Ponda alisema ni vyema Serikali ikawa makini na sera za mataifa makubwa ambayo yameingia katika migogoro na baadhi ya nchi za Afrika kwa maslahi binafsi.
Serikali iache kujiingiza katika migogoro na kundi hili, jambo la msingi ni kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu si vinginevyo, alisema Shekhe Ponda na kuongeza kuwa, si kweli kwamba kundi hilo ni la kigaidi kama alivyosema Bw. Nahodha bali kinachofanywa na kundi hilo ni kulinda mipaka ya nchi yao.
Alisema Bw. Nahodha hapaswi kuwaweka Watanzania katika hofu ya kuvamiwa na kushindwa kusafiri kwa shughuli mbalimbali ambazo ndioz huwapatia kipato na kukuza uchumi wao kutokana na taarifa za upotoshwaji dhidi ya kundi hilo.
Waziri anapozungumzia kundi hili ni sawa na kudhalilisha Uislamu, mbona hivi karibuni wameingia Wakongo wakiwa na silaha nzito lakini Serikali haikufanya kitu, kwanini Al-Shaabab, alihoji Shekhe Ponda.
Bw. Ponda alisema kauli iliyotoa Bw. Nahodha, imelenga kuwagawa Watanzania ili waichukie nchi ya Somalia kitu ambacho si sahihi.
Hivi karibuni, Bw. Nahodha alisema kutokana na nchi jirani ya Kenya kukumbwa na vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na kundi hilo, umefika wakati wa Watanzania kuwa makini na watu ambao wanaingia nchini kinyemela bila kufuata utaratibu
Ata wewe unaropoka unavyoweza ndo serikali imeachia watu wapige domo wee uhuru wa maoni na ni subjective we ukiona la mwenzio pumba the contrary is true to him to your opinions acheni watu wafunguke tu..Wakuu ina maana huyu shekh hajaingizwa kwenye daftari la mgao wa ccm? mbona anamponda vuai na anatetea magaidi wa alshabab? Shekh angefunguka zaidi kwa kuiponda Alshabab wa Tz ambao ni ccm na polisi wanao walipua wananchii kwa dhiki, dhihaka na karaa wanazopata shekh angewaeleza hawa ccm kwanza..na nijuavyo mimi alshabab ni kikundi cha kigaidi ina maana gaidi akiwa mwislam ni halali kidini ya kiislam..? au alindwe na kutetewa tu sababu ni mwislam? enzi za mwalimu mashekhe na ma padre walikuwa wanapima kauli zao kabla ya kuingiza public lakini siku hizi kila mtu anaropoka anavoweza..
Hivi ugaidi ni nini? Maana kwa definition yake vikundi vya waasi wote duniani ni vikundi vya kigaidi....narudia hivi vikundi havitaisha kama sera za nchi za magharibi hawataacha invasion kwenye ardhi zingine...hivi hao USA,NATO mnaowatetea kila siku wameua watu wangapi? Mbona wao hawaitwi killerz? Na anesema eti uislamu unaruhusu MAUAJI athibitishe maneno yake kutoka katika vitabu vyao nadhani ndo mjadala utakuwa wa kisomi zaidi
Pole sana ndugu,ukipewa mahali pa kupata ushahidi huendi kutazama unaendelea kulalama tu!