Shehe Mohammed Issa acha kumkashfu Shehe Hamza!

Shehe Mohammed Issa acha kumkashfu Shehe Hamza!

Lakini pia wewe ulimsikia huyo Padri Hamza alivyokiri kuwa alikuwa anaenda katika njia sahihi. Hata hivyo sheikh Muhammad Issa alikuwa akitoa na reference za Qur an na haditihi za mtume katika kumuweka sawa huyu murtad.

Aliyeenda kanisani kusema kuwa sasa ni zama za gospel na sio zama kujua sheria.
Hakuna cha Murtadi wala nini, mi niliona ile clip, sioni mahala alipokosea Sheikh Hamza, kwani Yesu hajapewa utukufu ndani ya Qur'an? Na je si tumeambiwa lazima arudi ndio iwe kiama? Na si ni nabii wa Mungu!
 
Kwani nani kasema utatoka??hivi kwa nini ninyi mnakuwa na mawazo NEGATIVE???
Kiswahili hikijui kwa hiyo unadhani uko Sawa Pole sana.
Fuatilia wachangiaji utaelewa siyo kukurupuka.
 
Mohamed Issa ni mmoja wa viongozi wa madhehebu ya sunni!

Kamtukana Shehe Hamza kwa sababu alikwenda kuhubiri kanisani na kusifia utukufu wa Yesu Kristo!
Waislamu, wakristo watu watu gani sote tumeumbwa na Mungu. Tusifanye maisha yawe magumu. Mwisho wa siku kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake na wala si kwa dini yake.
 
Hatuna kidubwasha kinachoitwa kuran bali kuna Quran katika uislam,
Hakuna mungu katika uislam bali kuna Allah subhaana wata'ala.
Umenipata mkuu,mwambie huyo mnafki muanzisha mada.
Lol...kumbe ktk uislamu hamna Mungu kuna Allah tuu.....mi eti najuaga Allah ndio Mungu .
 
Shetani hawezi kukubali Yesu kuwa mwana wa Mungu. hilo ndilo shetani analopingana nalo sana. sababu anajua hicho cheo ni kikubwa sana na kinazidi kumuondoa na kumuweka mbali zaidi zaidi na nia yake ya kujifanya ni mungu. lakini kwa mimi mtu akinambia Yesu si mwana wa mungu. haindhuru kitu kabisa. maana kwa yeye kuamini hivyo ni sawa kabisa na si ajabu. ingekuwa ajabu anapokubali jambo hilo. so hata ukimtukana Yesu na ukaikanyaga biblia n. wala haina athari kwangu kwa sababu Mungu wangu yupo ndani yangu na ukuu wake umeonekana kwa namna nyingi. na lakini yeye alikataa kupigana vita vya damu na nyama kupigania ukristo. alisema vita vyenu si vya damu na nyama bali ni dhidi ya mfalme wa anga hili,mfalme wa giza.

una uhuru kabisa wa kuamini Yesu si lolote si chochote. unaweza mfananisha na watu wengine wengi upendavyo lakini kwa mimi " kwa maana neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu"1wakorintho1-18" na Mungu alichagua mambo dhaifu ya dunia ili awaaibishe walio na nguvu.


(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome😉"
2 wakorintho 10:4
Ni kweli kabisa....kinachojalisha is what inside you. Sio mtoto wa Kiislamu kakojolea Biblia ...Wakristo wachome Msikiti!!! Haiwezekani.
 
Hakuna cha Murtadi wala nini, mi niliona ile clip, sioni mahala alipokosea Sheikh Hamza, kwani Yesu hajapewa utukufu ndani ya Qur'an? Na je si tumeambiwa lazima arudi ndio iwe kiama? Na si ni nabii wa Mungu!
Yesu amepewa utukufu ila kuna mambo Hamza ameteleza kwa kusema kuwa hizi ni zama za Gospel wakti kwa imani yake ni kuwa qur an ndiyo kitabu cha mwisho .

Ndio maana wakatokea wajuzi kumkumbusha alipoteleza ndio maana hata yeye mwenyewe amekili kuwa aliteleza na amerudi katika imani yake.

NOTE :hakuna nabii asiyepewa utukufu katika qur an wote wamepewa utkufu kwa mitihani waliyopitia kwenye kusmabaza dini.
 
Hiyo redio imani si ya waislamu....kwahiyo mnaitumia kutukanana ninyi kwa ninyi!?!! Ngoja niishie hapa
Cha ajabu wengine wanadai alikwenda kutubu kwa shehe wa mkoa! Kama ni kweli kwa nini waendelee kumkashfu?!
 
sasa kama anakosea asiambiwee tena kama ikathibitika kuwa ni kweli anapotosha inapaswa atahadharishwe uislam ni dini ya haqi na tukitofautiana turudi ktk kitab na sunna tutapata jibu tu.....lengo la kuja kupost hii habar yako ni nini?
 
Kwa jazba kubwa umesikika ukimkashfu Shehe Hamza kwamba anawapotosha waislam!

Wewe shehe Issa usijifanye ndiye unaifahamu Koran kuwapita waislam wote! Unapaswa kufahamu kuwa Shehe Hamza ni msomi aliyetukuka katika Koran! Kama una hoja ya kupinga mahubiri yake, pinga kwa hoja na vielelezo na siyo kutoa kashfa!

Kumbuka wote tunajifunza kutokana na maandiko! Wewe Issa hukuwepo wakati wa Mtume Mohammed hivyo kama wengine wote na wewe unasoma maandiko tuliyoyakuta! Usilazimishe wote tuwe na uelewa sawa na wewe!
Uyo hamza mwenye amekiri amekosea kwenye hayo mahubiri na ameomba rardhi kwa waislam wote baadaya ya kutubu kwa Allah
 
Back
Top Bottom