SHARO MILIONEA-Kwanini?

Kijana ameondoka mapema sana, japo kifo hakina umri lakini inauma sana kwa kijana wa umri ule, maisha ndio yanaanza, wazazi wanapumua wakijua sasa kijana anawasaidia katika hii ziki ya TZ, wasanii nao wanajua mtu fulani ameongezeka katika fani huku wengine wakifikiria jinsi ya kupata maujanja toka kwa Sharo, ghafla kijana anazimika kama mshumaa anatuacha tunaulizana, tuna majonzi tunatafuta mchawi lakini ndio hivyo MUNGU amempenda zaidi..........tuliobaki tumuombee na kukumbuka kuwa hapa duniani tu wapitaji........R.I.P SHARO......Binti yangu wa miaka 2 anapenda sana msemo wako wa kule hakukaliki men ananifanya nacheka kila wakati.
 
Hii dunia mmmmh its sad mtu amejitahidi hadi kufika hapo alipo na kupoteza ndoto zke zote kwa muda mchache. Bwana awe na ndugu,jamaa,marafiki kwenye huu wakati mgumu
 
Mshkaji ameniuma sana aisee,nakumbuka filamu ya kwanza kumuon ilikuwa ni komedi moja hivi inaitwa CHABO ame-akti na muhogo mchungu miaka ya 2009 au 2010 hivi kuanzia hapo nilitokea kumkubali sana,sasa hivi mambo yake yapo kwenye pic anapiga deal za maana na makampuni makubwa kama Airtel ndiyo haya yanamkuta duh!Kwakweli tujiandae ndugu zangu kifo hakipigi hodi wala haki-beep. R.I.P Jembe langu la ukweli.
 
What happened?

Huna Taarifa! ... Fredrick Sanga

Msanii/Muigizaji/Mchekeshaji Hussein Ramadhani Mtioeti (27) maarufu SHARO MILIONEA amefariki dunia katika ajali ya gari jijini Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Prudence Masawe, amethibitisha kutokea kwa ajali na kusema kuwa marehemu amefikwa na umauti baada ya gari lake aina ya Toyota Haria lenye namba za usajili T478DVR kuacha njia na kupinduka.


sharo-milionea.jpg




gari.jpg


Hili ndilo gari aina ya Toyota Harrier lenye namba T278 BVR ilipinduka na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha msanii Sharo milionea USIKU WA JANA MIDA YA SAA MBILI USIKU

127.jpg


212.jpg
 
Mwigizaji Bora katika matangazo ya AIRTEL hasa kwenye matangazo ya Kuhamia Airtel
Ameaacha umahili wake kwetu
Mungu na aiweke roho yake mahali pema
 
Back
Top Bottom