Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,289
- 8,510
Dunia inajua, Tanzania inajua kwamba mwanaharakati na mwanasheria mbobezi aliyeamua kuingia kwenye siasa ndugu Tundu alipigwa risasi nyingi tu hadi zikamfikisha ubeligiji kutibu. Shahidi namba moja na aweza pia kuwa mshukiwa namba moja ni Dereva wa TUNDU.
DEREVA amefichwa, haijulikani alipo kwa hofu kuwa akipatikana maisha yake yapo hatarini. Je ni hatari gani? Mimi na walio wengi hatujui, wanaojua ni wale walioficha dereva. Pengine, tunaweza kudhani, Dereva akiwa shahidi namba moja wahusika wa tukio waweza kumdhuru, na akiwa mtuhumiwa namba moja washirika wake waweza kumdhuru.
Toka awali tukio kutokea jitihada kubwa kuficha dereva zimefanyika na zinaendelea. Dereva hana ushirikiano wowote na dola Tanzania, pengine hata vyombo vya habari ndani au nje kama vile TBC, AZAM, BBC, DW, NTV. Basi japo kujitokeza tukasikia upande wake na akaulizwa maswali chokonozi kama ilivyo kwa BOSS wake Tundu.
TUNDU kapigwa risasi mguu wa kulia upande wa dereva, iweje dereva akakosa kajeraha japo kimoja kidogodogo hivi? Siri anajua Tundu na dereva wake!!!! Ni swali gumu lakini jepesi.
Je risasi zilichagua wa kumpata?
Je kwanini Tundu na dereva wake hawakurudi ofisi za bunge baada ya kugundua kuna nia ovu inawafuata kwenye Nissan nyeupe
Je, mbona hawakunyoosha kwenda polisi baada ya kugundua hatari
Swali kubwa zaidi.
Kwanini Dereva kafichwa hadi uchaguzi umefika? Amefichwa asiongee na polisi wala vyombo vya habari ndani na nje. Uchaguzi ukiisha atajitokeza sasa maana lengo lilikuwa kuongeza hamasa ya uchaguzi kwa mhusika
DEREVA amefichwa, haijulikani alipo kwa hofu kuwa akipatikana maisha yake yapo hatarini. Je ni hatari gani? Mimi na walio wengi hatujui, wanaojua ni wale walioficha dereva. Pengine, tunaweza kudhani, Dereva akiwa shahidi namba moja wahusika wa tukio waweza kumdhuru, na akiwa mtuhumiwa namba moja washirika wake waweza kumdhuru.
Toka awali tukio kutokea jitihada kubwa kuficha dereva zimefanyika na zinaendelea. Dereva hana ushirikiano wowote na dola Tanzania, pengine hata vyombo vya habari ndani au nje kama vile TBC, AZAM, BBC, DW, NTV. Basi japo kujitokeza tukasikia upande wake na akaulizwa maswali chokonozi kama ilivyo kwa BOSS wake Tundu.
TUNDU kapigwa risasi mguu wa kulia upande wa dereva, iweje dereva akakosa kajeraha japo kimoja kidogodogo hivi? Siri anajua Tundu na dereva wake!!!! Ni swali gumu lakini jepesi.
Je risasi zilichagua wa kumpata?
Je kwanini Tundu na dereva wake hawakurudi ofisi za bunge baada ya kugundua kuna nia ovu inawafuata kwenye Nissan nyeupe
Je, mbona hawakunyoosha kwenda polisi baada ya kugundua hatari
Swali kubwa zaidi.
Kwanini Dereva kafichwa hadi uchaguzi umefika? Amefichwa asiongee na polisi wala vyombo vya habari ndani na nje. Uchaguzi ukiisha atajitokeza sasa maana lengo lilikuwa kuongeza hamasa ya uchaguzi kwa mhusika