Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,277
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.
Sehemu ya kwanza.
Dunia nzima ilikuwa kimya kwa muda, hakukuwa na mtu aliyeamini kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa mbali na televisheni, wakazisogelea, waliokuwa na simu zilizokuwa na uwezo wa kuingia kwenye huduma za internet, walifanya hivyo na kuangalia taarifa iliyoonekana kuingia muda huo.
Taarifa iliyokuwa ikionekana ndiyo ambayo iliwavuta watu wengi na kutamani kujua ni kitu gani hasa kilichokuwa kikiendelea. Kulikuwa na taarifa kubwa juu ya upotevu wa ndege kubwa ya Shirika la Ndege la Orange Airlines, Airbus A350-900 walibaki wakiuliza ni kitu gani kilitokea.
Watu hawakuamini, taarifa zilianzia mbali kwamba ndege hiyo ya sita kwa ukubwa duniani iliyokuwa ikifanya safari yake kutokea nchini Marekani kuelekea Uholanzi na Dubai kwa kupitia viwanja kadhaa vya ndege barani Ulaya ilikuwa imepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Kila mtu alichanganyikiwa, tukio la kupotea kwa ndege hiyo likawarudisha watu nyuma na kuikumbuka ndege ya Shirika la Ndege ya Malaysia, Airlines Flight 370 ilivyokuwa imepotea mwaka 2014.
Kila mtu aliogopa, waandishi wa habari walipopata taarifa kuhusu ndege hiyo hawakutaka kupoteza muda, haraka sana wakawasiliana na mamlaka husika ili kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Hakukuwa na mtu aliyelizungumzia tukio hilo kwa undani kwani mpaka muda huo watu wengi walihisi ilikuwa ni tetesi kwa lengo la kuwatisha watu fulani. Watu wa mamlaka husika walichokisema kilikuwa ni kimoja tu kwamba wangehakikisha wanawasiliana na marubani wa ndege hiyo na kuzungumza nao ili kuona kama kulikuwa na ukweli wowote ule.
Tetesi hizo ziliendelea kuvuma, kila mtu aliyesikia alihitaji kujua ukweli kwa kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa na ndugu zao humo hawakutulia, tetesi zile ziliwaumiza na kuhisi kwamba zilikuwa kweli kabisa.
Ndege hiyo ambayo iliondoka nchini Marekani ndani ya Jiji la New York katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK ilitarajiwa kuingia nchini Uingereza baada ya saa tano ambapo ingetumia saa mbili juu ya Bahari ya Atlantiki lakini kitu cha ajabu kuanzia muda ambayo iliachia ardhi ya Marekani, hawakuweza kuwasiliana nao kitu kilichomfanya kila mmoja kuogopa.
Watu wakajazana katika uwanja wa ndege wa JFK, walihitaji kujua kilichokuwa kikiendelea, walichokisema ni kwamba mara ya mwisho waliwasiliana na wenzao walipokuwa angani lakini baada ya dakika chache hawakuweza kuwapata kitu kilichoonyesha kwamba kulikuwa na tatizo mahali fulani.
Hiyo haikuishia nchini Marekani tu, bali hata nchini Uingereza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow uliokuwa jijini London kulikuwa na watu wengi waliotaka kufahamu kuhusu ndege hiyo, kwa kifupi, hakukuwa na mtu aliyekubali kama ndege hiyo ilipotea.
Viongozi wa Kampuni ya Orange Inc ambayo ilikuwa ikisimamia ndege hiyo wakakutana katika kikao cha dharura kwa ajili ya kuzungumza kile kilichotokea.
Kwenye kikao hicho kila mmoja alitoa maoni yake, hapo kabla waliwasiliana na watu wa rada na kuzungumza nao na kuwaomba kuwapa taarifa juu ya ndege hiyo lakini kitu cha ajabu kabisa hakukuwa na taarifa nzuri waliyopewa kwani hata watu wa rada hiyo nao walishangaa kuona mawasiliano yanakatika pasipo kujua sababu iliyofanya kitu hicho.
Baada ya saa moja na nusu, taarifa hizo hazikuwa tetesi tena, zilithibitishwa kwamba ndege hiyo ilipotea hivyo watu walitakiwa kuripoti na kuwaambia watu wengine.
Kila mtu alizungumza lake, wapo waliosema kwamba Marekani alihusika kupotea kwa ndege hiyo, wapo waliosema Kundi la Kigaidi la Mujahdeen liliilipua ndege hiyo kama ishara ya kuitisha dunia kwamba walikuwa na nguvu ya kufanya kitu chochote kile.
Kila mmoja alichanganyikiwa, waliongea mambo mengi lakini hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na taarifa kamili kuhusu ndege hiyo iliyopotea.
Kwa kutumia jeshi la anga, Marekani ikatuma ndege zake na kwenda kuitafuta, walizunguka sehemu kubwa kwa ndege hizo za kasi, walitumia mpaka satalaiti zao lakini kitu cha ajabu kabisa, hawakuweza kufanikiwa kuipata.
“Labda itakuwa imekwama kwenye milima mirefu!” alisema mwanaume mmoja.
“Kwa hiyo?”
“Tuzitume ndege zikaangalie huko,” alisema mwanaume mwingine.
Hilo ndilo lililofanyika, haraka sana ndege zikatumwa na kuelekea katika milima mikubwa kama Evarest, Himalaya na mingine kwenda kuangalia ili kuona kama ndege hiyo ilikuwa imekwama huko.
Baada ya saa kadhaa tangu watu hao waondoke, simu ikapigwa na kuambiwa kwamba ndege hiyo haikuonekana huko, haikuwepo kitu kilichomaanisha kwamba walitakiwa kwenda kuangalia sehemu nyingine.
Hiyo iilikuwa ni siku ya kwanza kupotea kwa ndege hiyo, dakika zilikatika, saa zilikimbia, siku ya pili ikaingia lakini hakukuwa na taarifa zilizosema mahali ambapo ndege hiyo ilipokuwa.
“Hebu wasilianeni na CIA tuone watatuambiaje,” alisema mwanaume mmoja na hivyo simu kupigwa huko.
Wao ndiyo waliokuwa na nguvu ya kupiga simu katika kampuni ya Kimarekani ya CPS Engeneering iliyokuwa jijini Washington DC ambao walikuwa watu pekee waliokuwa na jukumu la kutengeneza injini za ndege kubwa za Boeing na kuwauliza kuhusu ndege hiyo.
Bosi wa kampuni hiyo, haraka sana akawasiliana na vijana wake wa IT na kuzungumza nao. Kwa kawaida, kwenye kila injini ya ndege kubwa waliyokuwa wakiitengeneza, kwa ndani waliweka GPS kwa ajili ya kuifuatilia kila mahali ilipokuwa ikienda.
Hilo lilikuwa suala la siri sana ambalo halikuwa likijulikana zaidi ya vijana hao wa IT, bosi wa kampuni hiyo na baadhi ya viongozi wa Kijasusi kutoka hapo CIA.
Vijana hao walipoambiwa kuhusu kupotea kwa ndege hiyo, wakaingia kwenye kompyuta zao na kuanza kuitafuta huku wakiliandika jina la ndege hiyo, namba ya injini yake, ikaja na kuanza kuzunguka kila kona wakiitafuta.
Kazi ilikuwa kubwa, kabla ya saa moja asubuhi, ilikuwa ikionekana, GPS ilisema kwamba ilikuwa usawa wa Bahari ya Atlantiki ikielekea katika Bara la Ulaya lakini baada ya muda fulani, hata GPS yenyewe haikuweza kusoma kitu kilichowashangaza hata wao wenyewe.
“Hii ndege itakuwa imeanguka kwenye maji,” alisema kijana mmoja.
“Kipi kinachokufanya kufikiria hivyo?”
“Ni kwa sababu kifaa cha GPS kimeacha kusoma ndege ikiwa usawa wa bahari, inawezekana kabisa iliangukia baharini na hivyo kifaa kuingia maji na kuzima,” alisema kijana huyo.
Taarifa hiyo ikapelekwa mpaka makao makuu ya CIA, hakukuwa na sababu ya kubaki ofisini tu bila kufanya juhudi za kuwatuma watu kwenda huko. Simu ikapigwa na wanajeshi wa majini wakaanza kuelekea huko wakiitafuta ndege hiyo.
Ilikuwa kazi kubwa ambayo hawakuwahi kukutana nayo kabla, walizunguka kila kona, walitumia vifaa vikubwa kuingia ndani ya bahari, huko walikutana na meli zilizozama, ndege nyingine ambazo ziliwahi kuanguka lakini hawakuweza kukutana na ndege hiyo kubwa.
Wakati wao wakiendelea na utafutaji, dunia nzima ilikuwa ni kilio tu, watu walihuzunika, zaidi ya abiria 550 hawakujulikana walipokuwa.
Lilikuwa jambo baya na gumu kuvumilika, wengi waliendelea kuilaumu serikali ya Marekani kwani waliamini kabisa kwamba walikuwa watu ambao waliipoteza ndege hiyo kwa malengo yao binafsi na ndiyo maana hawakutaka kulizungumzia sana suala hilo.
Rais wa Marekani kipindi hicho, Bwana Powell Ludovick akaingiwa doa, kwake, kitendo cha kupotea kwa ndege hiyo na wakati alikuwa na nguvu katika taifa kubwa kama Marekani ilionekana ni kama dharau, hakutaka kuona kila mtu akiizungumzia Marekani kwa ubaya hivyo kuwaagiza watu wake wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha ndege hiyo inapatikana haraka sana.
“Tunajitahidi mkuu!” alisema Mkurugenzi wa CIA, Bwana Matt.
“Fanya kila liwezekanalo, tuna muda mfupi,” alisema Powell.
Siku ya tatu ikaingia, ya nne nayo ikaja, mpaka wiki inakatika bado hapakuwa na taarifa rasmi ya kuzungumzia mahali ndege hiyo ilipokuwa.
Hilo lilikuwa jambo lililoshangaza, ndege nyingi zilizokuwa zimepotea zilionekana isipokuwa ndege hiyo tu ambayo watu wengi walihisi inawezekana ilitoka nje ya dunia na kwenda katika sayari nyingine.
Wakati mwingine hata jambo hilo lilionekana kuwa gumu kukubalika kwani kwa jinsi habari hiyo ilivyokuwa gumzo duniani, jinsi ilivyokuwa ikisumbua vichwa vya watu wengi basi NASA (National Aeronautics and Space Administration) ambayo ilihusika na masuala ya anga isingebaki kimya, ni lazima wangesema mahali ndege hiyo ilipokuwa kama tu ingekuwa imetokea nje ya dunia hii.
Watu waliokuwa na ndugu zao ambao walikuwa ndani ya ndege hiyo wakaanza kuzika nguo za watu hao kwa kuamini hapakuwa na dalili zozote za kuwapata watu hao na inawezekana kabisa huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.
Ilikuwa ni huruma, makaburi ya pamoja yalijengwa haraka na watu kuzika nguo na vifaa vingine vya ndugu zao waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Kama kulalamika, walifanya hivyo sana, walilia mno lakini hakukuwa na kilichobadilika, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa ndugu zao, yaani ndege ile iliwezekana ilikuwa mahali fulani, huko, ililipuliwa na volkano au ilianguka katika Bara la Antaktika ambako hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akiishi huko kutokana na baridi kali.
Japokuwa watu walikuwa wakilia na kuomboleza, hapakuwa na mtu ambaye alijua kilichokuwa nyuma ya ndege hiyo kubwa.
Kati ya watu 550 waliokuwa ndani ya ndege hiyo, pia ndani yake iliwabeba watu watano, wasiojuana ambapo kila mmoja nyuma yake alikuwa na stori nzito ya maisha yake.
Ili kwa baadhi ya watu sehemu nyingine wawe na amani, furaha ilikuwa ni lazima watu hao wafe, wapotee katika mazingira ya kutatanisha ambayo kusingekuwa na mtu yeyote atakayejua kama walikuwa wameuawa.
Humo ndani ya ndege watu hao watano hawakujuana lakini walikuwa na mambo makubwa maishani mwao. Kama watu hao wangefika salama huko walipokuwa wakienda ilikuwa ni lazima dunia ichafuke, ili dunia iendelee kuwa sehemu salama, ilikuwa ni lazima kifanyike kile kilichofanyika.
Ni stori za watu watano tu ambao leo hii walisababisha zaidi ya abiria 550 kutokujulikana mahali walipokuwa. Ni hao watu watano ndiyo waliosababisha kipindi hicho dunia nzima ilie na kuomboleza kwa kuamini kwamba kweli ndege hiyo ilipotea na kwenda kulipuka sehemu fulani.
Kwa sababu simulizi ya Biashara ya Kifo inakaribia mwishoni, nimeanza na hii simulizi mpya huku tukiendelea kusubiri ile iishe.
Je, nini kitaendelea?
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.
Sehemu ya kwanza.
Dunia nzima ilikuwa kimya kwa muda, hakukuwa na mtu aliyeamini kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa mbali na televisheni, wakazisogelea, waliokuwa na simu zilizokuwa na uwezo wa kuingia kwenye huduma za internet, walifanya hivyo na kuangalia taarifa iliyoonekana kuingia muda huo.
Taarifa iliyokuwa ikionekana ndiyo ambayo iliwavuta watu wengi na kutamani kujua ni kitu gani hasa kilichokuwa kikiendelea. Kulikuwa na taarifa kubwa juu ya upotevu wa ndege kubwa ya Shirika la Ndege la Orange Airlines, Airbus A350-900 walibaki wakiuliza ni kitu gani kilitokea.
Watu hawakuamini, taarifa zilianzia mbali kwamba ndege hiyo ya sita kwa ukubwa duniani iliyokuwa ikifanya safari yake kutokea nchini Marekani kuelekea Uholanzi na Dubai kwa kupitia viwanja kadhaa vya ndege barani Ulaya ilikuwa imepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Kila mtu alichanganyikiwa, tukio la kupotea kwa ndege hiyo likawarudisha watu nyuma na kuikumbuka ndege ya Shirika la Ndege ya Malaysia, Airlines Flight 370 ilivyokuwa imepotea mwaka 2014.
Kila mtu aliogopa, waandishi wa habari walipopata taarifa kuhusu ndege hiyo hawakutaka kupoteza muda, haraka sana wakawasiliana na mamlaka husika ili kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Hakukuwa na mtu aliyelizungumzia tukio hilo kwa undani kwani mpaka muda huo watu wengi walihisi ilikuwa ni tetesi kwa lengo la kuwatisha watu fulani. Watu wa mamlaka husika walichokisema kilikuwa ni kimoja tu kwamba wangehakikisha wanawasiliana na marubani wa ndege hiyo na kuzungumza nao ili kuona kama kulikuwa na ukweli wowote ule.
Tetesi hizo ziliendelea kuvuma, kila mtu aliyesikia alihitaji kujua ukweli kwa kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa na ndugu zao humo hawakutulia, tetesi zile ziliwaumiza na kuhisi kwamba zilikuwa kweli kabisa.
Ndege hiyo ambayo iliondoka nchini Marekani ndani ya Jiji la New York katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK ilitarajiwa kuingia nchini Uingereza baada ya saa tano ambapo ingetumia saa mbili juu ya Bahari ya Atlantiki lakini kitu cha ajabu kuanzia muda ambayo iliachia ardhi ya Marekani, hawakuweza kuwasiliana nao kitu kilichomfanya kila mmoja kuogopa.
Watu wakajazana katika uwanja wa ndege wa JFK, walihitaji kujua kilichokuwa kikiendelea, walichokisema ni kwamba mara ya mwisho waliwasiliana na wenzao walipokuwa angani lakini baada ya dakika chache hawakuweza kuwapata kitu kilichoonyesha kwamba kulikuwa na tatizo mahali fulani.
Hiyo haikuishia nchini Marekani tu, bali hata nchini Uingereza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow uliokuwa jijini London kulikuwa na watu wengi waliotaka kufahamu kuhusu ndege hiyo, kwa kifupi, hakukuwa na mtu aliyekubali kama ndege hiyo ilipotea.
Viongozi wa Kampuni ya Orange Inc ambayo ilikuwa ikisimamia ndege hiyo wakakutana katika kikao cha dharura kwa ajili ya kuzungumza kile kilichotokea.
Kwenye kikao hicho kila mmoja alitoa maoni yake, hapo kabla waliwasiliana na watu wa rada na kuzungumza nao na kuwaomba kuwapa taarifa juu ya ndege hiyo lakini kitu cha ajabu kabisa hakukuwa na taarifa nzuri waliyopewa kwani hata watu wa rada hiyo nao walishangaa kuona mawasiliano yanakatika pasipo kujua sababu iliyofanya kitu hicho.
Baada ya saa moja na nusu, taarifa hizo hazikuwa tetesi tena, zilithibitishwa kwamba ndege hiyo ilipotea hivyo watu walitakiwa kuripoti na kuwaambia watu wengine.
Kila mtu alizungumza lake, wapo waliosema kwamba Marekani alihusika kupotea kwa ndege hiyo, wapo waliosema Kundi la Kigaidi la Mujahdeen liliilipua ndege hiyo kama ishara ya kuitisha dunia kwamba walikuwa na nguvu ya kufanya kitu chochote kile.
Kila mmoja alichanganyikiwa, waliongea mambo mengi lakini hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na taarifa kamili kuhusu ndege hiyo iliyopotea.
Kwa kutumia jeshi la anga, Marekani ikatuma ndege zake na kwenda kuitafuta, walizunguka sehemu kubwa kwa ndege hizo za kasi, walitumia mpaka satalaiti zao lakini kitu cha ajabu kabisa, hawakuweza kufanikiwa kuipata.
“Labda itakuwa imekwama kwenye milima mirefu!” alisema mwanaume mmoja.
“Kwa hiyo?”
“Tuzitume ndege zikaangalie huko,” alisema mwanaume mwingine.
Hilo ndilo lililofanyika, haraka sana ndege zikatumwa na kuelekea katika milima mikubwa kama Evarest, Himalaya na mingine kwenda kuangalia ili kuona kama ndege hiyo ilikuwa imekwama huko.
Baada ya saa kadhaa tangu watu hao waondoke, simu ikapigwa na kuambiwa kwamba ndege hiyo haikuonekana huko, haikuwepo kitu kilichomaanisha kwamba walitakiwa kwenda kuangalia sehemu nyingine.
Hiyo iilikuwa ni siku ya kwanza kupotea kwa ndege hiyo, dakika zilikatika, saa zilikimbia, siku ya pili ikaingia lakini hakukuwa na taarifa zilizosema mahali ambapo ndege hiyo ilipokuwa.
“Hebu wasilianeni na CIA tuone watatuambiaje,” alisema mwanaume mmoja na hivyo simu kupigwa huko.
Wao ndiyo waliokuwa na nguvu ya kupiga simu katika kampuni ya Kimarekani ya CPS Engeneering iliyokuwa jijini Washington DC ambao walikuwa watu pekee waliokuwa na jukumu la kutengeneza injini za ndege kubwa za Boeing na kuwauliza kuhusu ndege hiyo.
Bosi wa kampuni hiyo, haraka sana akawasiliana na vijana wake wa IT na kuzungumza nao. Kwa kawaida, kwenye kila injini ya ndege kubwa waliyokuwa wakiitengeneza, kwa ndani waliweka GPS kwa ajili ya kuifuatilia kila mahali ilipokuwa ikienda.
Hilo lilikuwa suala la siri sana ambalo halikuwa likijulikana zaidi ya vijana hao wa IT, bosi wa kampuni hiyo na baadhi ya viongozi wa Kijasusi kutoka hapo CIA.
Vijana hao walipoambiwa kuhusu kupotea kwa ndege hiyo, wakaingia kwenye kompyuta zao na kuanza kuitafuta huku wakiliandika jina la ndege hiyo, namba ya injini yake, ikaja na kuanza kuzunguka kila kona wakiitafuta.
Kazi ilikuwa kubwa, kabla ya saa moja asubuhi, ilikuwa ikionekana, GPS ilisema kwamba ilikuwa usawa wa Bahari ya Atlantiki ikielekea katika Bara la Ulaya lakini baada ya muda fulani, hata GPS yenyewe haikuweza kusoma kitu kilichowashangaza hata wao wenyewe.
“Hii ndege itakuwa imeanguka kwenye maji,” alisema kijana mmoja.
“Kipi kinachokufanya kufikiria hivyo?”
“Ni kwa sababu kifaa cha GPS kimeacha kusoma ndege ikiwa usawa wa bahari, inawezekana kabisa iliangukia baharini na hivyo kifaa kuingia maji na kuzima,” alisema kijana huyo.
Taarifa hiyo ikapelekwa mpaka makao makuu ya CIA, hakukuwa na sababu ya kubaki ofisini tu bila kufanya juhudi za kuwatuma watu kwenda huko. Simu ikapigwa na wanajeshi wa majini wakaanza kuelekea huko wakiitafuta ndege hiyo.
Ilikuwa kazi kubwa ambayo hawakuwahi kukutana nayo kabla, walizunguka kila kona, walitumia vifaa vikubwa kuingia ndani ya bahari, huko walikutana na meli zilizozama, ndege nyingine ambazo ziliwahi kuanguka lakini hawakuweza kukutana na ndege hiyo kubwa.
Wakati wao wakiendelea na utafutaji, dunia nzima ilikuwa ni kilio tu, watu walihuzunika, zaidi ya abiria 550 hawakujulikana walipokuwa.
Lilikuwa jambo baya na gumu kuvumilika, wengi waliendelea kuilaumu serikali ya Marekani kwani waliamini kabisa kwamba walikuwa watu ambao waliipoteza ndege hiyo kwa malengo yao binafsi na ndiyo maana hawakutaka kulizungumzia sana suala hilo.
Rais wa Marekani kipindi hicho, Bwana Powell Ludovick akaingiwa doa, kwake, kitendo cha kupotea kwa ndege hiyo na wakati alikuwa na nguvu katika taifa kubwa kama Marekani ilionekana ni kama dharau, hakutaka kuona kila mtu akiizungumzia Marekani kwa ubaya hivyo kuwaagiza watu wake wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha ndege hiyo inapatikana haraka sana.
“Tunajitahidi mkuu!” alisema Mkurugenzi wa CIA, Bwana Matt.
“Fanya kila liwezekanalo, tuna muda mfupi,” alisema Powell.
Siku ya tatu ikaingia, ya nne nayo ikaja, mpaka wiki inakatika bado hapakuwa na taarifa rasmi ya kuzungumzia mahali ndege hiyo ilipokuwa.
Hilo lilikuwa jambo lililoshangaza, ndege nyingi zilizokuwa zimepotea zilionekana isipokuwa ndege hiyo tu ambayo watu wengi walihisi inawezekana ilitoka nje ya dunia na kwenda katika sayari nyingine.
Wakati mwingine hata jambo hilo lilionekana kuwa gumu kukubalika kwani kwa jinsi habari hiyo ilivyokuwa gumzo duniani, jinsi ilivyokuwa ikisumbua vichwa vya watu wengi basi NASA (National Aeronautics and Space Administration) ambayo ilihusika na masuala ya anga isingebaki kimya, ni lazima wangesema mahali ndege hiyo ilipokuwa kama tu ingekuwa imetokea nje ya dunia hii.
Watu waliokuwa na ndugu zao ambao walikuwa ndani ya ndege hiyo wakaanza kuzika nguo za watu hao kwa kuamini hapakuwa na dalili zozote za kuwapata watu hao na inawezekana kabisa huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.
Ilikuwa ni huruma, makaburi ya pamoja yalijengwa haraka na watu kuzika nguo na vifaa vingine vya ndugu zao waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Kama kulalamika, walifanya hivyo sana, walilia mno lakini hakukuwa na kilichobadilika, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa ndugu zao, yaani ndege ile iliwezekana ilikuwa mahali fulani, huko, ililipuliwa na volkano au ilianguka katika Bara la Antaktika ambako hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akiishi huko kutokana na baridi kali.
Japokuwa watu walikuwa wakilia na kuomboleza, hapakuwa na mtu ambaye alijua kilichokuwa nyuma ya ndege hiyo kubwa.
Kati ya watu 550 waliokuwa ndani ya ndege hiyo, pia ndani yake iliwabeba watu watano, wasiojuana ambapo kila mmoja nyuma yake alikuwa na stori nzito ya maisha yake.
Ili kwa baadhi ya watu sehemu nyingine wawe na amani, furaha ilikuwa ni lazima watu hao wafe, wapotee katika mazingira ya kutatanisha ambayo kusingekuwa na mtu yeyote atakayejua kama walikuwa wameuawa.
Humo ndani ya ndege watu hao watano hawakujuana lakini walikuwa na mambo makubwa maishani mwao. Kama watu hao wangefika salama huko walipokuwa wakienda ilikuwa ni lazima dunia ichafuke, ili dunia iendelee kuwa sehemu salama, ilikuwa ni lazima kifanyike kile kilichofanyika.
Ni stori za watu watano tu ambao leo hii walisababisha zaidi ya abiria 550 kutokujulikana mahali walipokuwa. Ni hao watu watano ndiyo waliosababisha kipindi hicho dunia nzima ilie na kuomboleza kwa kuamini kwamba kweli ndege hiyo ilipotea na kwenda kulipuka sehemu fulani.
Kwa sababu simulizi ya Biashara ya Kifo inakaribia mwishoni, nimeanza na hii simulizi mpya huku tukiendelea kusubiri ile iishe.
Je, nini kitaendelea?