Shambulio la damu

Madame S

JF-Expert Member
Mar 4, 2015
17,172
34,277
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.

Sehemu ya kwanza.

Dunia nzima ilikuwa kimya kwa muda, hakukuwa na mtu aliyeamini kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa mbali na televisheni, wakazisogelea, waliokuwa na simu zilizokuwa na uwezo wa kuingia kwenye huduma za internet, walifanya hivyo na kuangalia taarifa iliyoonekana kuingia muda huo.
Taarifa iliyokuwa ikionekana ndiyo ambayo iliwavuta watu wengi na kutamani kujua ni kitu gani hasa kilichokuwa kikiendelea. Kulikuwa na taarifa kubwa juu ya upotevu wa ndege kubwa ya Shirika la Ndege la Orange Airlines, Airbus A350-900 walibaki wakiuliza ni kitu gani kilitokea.
Watu hawakuamini, taarifa zilianzia mbali kwamba ndege hiyo ya sita kwa ukubwa duniani iliyokuwa ikifanya safari yake kutokea nchini Marekani kuelekea Uholanzi na Dubai kwa kupitia viwanja kadhaa vya ndege barani Ulaya ilikuwa imepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Kila mtu alichanganyikiwa, tukio la kupotea kwa ndege hiyo likawarudisha watu nyuma na kuikumbuka ndege ya Shirika la Ndege ya Malaysia, Airlines Flight 370 ilivyokuwa imepotea mwaka 2014.
Kila mtu aliogopa, waandishi wa habari walipopata taarifa kuhusu ndege hiyo hawakutaka kupoteza muda, haraka sana wakawasiliana na mamlaka husika ili kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Hakukuwa na mtu aliyelizungumzia tukio hilo kwa undani kwani mpaka muda huo watu wengi walihisi ilikuwa ni tetesi kwa lengo la kuwatisha watu fulani. Watu wa mamlaka husika walichokisema kilikuwa ni kimoja tu kwamba wangehakikisha wanawasiliana na marubani wa ndege hiyo na kuzungumza nao ili kuona kama kulikuwa na ukweli wowote ule.
Tetesi hizo ziliendelea kuvuma, kila mtu aliyesikia alihitaji kujua ukweli kwa kile kilichokuwa kimetokea. Waliokuwa na ndugu zao humo hawakutulia, tetesi zile ziliwaumiza na kuhisi kwamba zilikuwa kweli kabisa.
Ndege hiyo ambayo iliondoka nchini Marekani ndani ya Jiji la New York katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK ilitarajiwa kuingia nchini Uingereza baada ya saa tano ambapo ingetumia saa mbili juu ya Bahari ya Atlantiki lakini kitu cha ajabu kuanzia muda ambayo iliachia ardhi ya Marekani, hawakuweza kuwasiliana nao kitu kilichomfanya kila mmoja kuogopa.
Watu wakajazana katika uwanja wa ndege wa JFK, walihitaji kujua kilichokuwa kikiendelea, walichokisema ni kwamba mara ya mwisho waliwasiliana na wenzao walipokuwa angani lakini baada ya dakika chache hawakuweza kuwapata kitu kilichoonyesha kwamba kulikuwa na tatizo mahali fulani.
Hiyo haikuishia nchini Marekani tu, bali hata nchini Uingereza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow uliokuwa jijini London kulikuwa na watu wengi waliotaka kufahamu kuhusu ndege hiyo, kwa kifupi, hakukuwa na mtu aliyekubali kama ndege hiyo ilipotea.
Viongozi wa Kampuni ya Orange Inc ambayo ilikuwa ikisimamia ndege hiyo wakakutana katika kikao cha dharura kwa ajili ya kuzungumza kile kilichotokea.
Kwenye kikao hicho kila mmoja alitoa maoni yake, hapo kabla waliwasiliana na watu wa rada na kuzungumza nao na kuwaomba kuwapa taarifa juu ya ndege hiyo lakini kitu cha ajabu kabisa hakukuwa na taarifa nzuri waliyopewa kwani hata watu wa rada hiyo nao walishangaa kuona mawasiliano yanakatika pasipo kujua sababu iliyofanya kitu hicho.
Baada ya saa moja na nusu, taarifa hizo hazikuwa tetesi tena, zilithibitishwa kwamba ndege hiyo ilipotea hivyo watu walitakiwa kuripoti na kuwaambia watu wengine.
Kila mtu alizungumza lake, wapo waliosema kwamba Marekani alihusika kupotea kwa ndege hiyo, wapo waliosema Kundi la Kigaidi la Mujahdeen liliilipua ndege hiyo kama ishara ya kuitisha dunia kwamba walikuwa na nguvu ya kufanya kitu chochote kile.
Kila mmoja alichanganyikiwa, waliongea mambo mengi lakini hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na taarifa kamili kuhusu ndege hiyo iliyopotea.
Kwa kutumia jeshi la anga, Marekani ikatuma ndege zake na kwenda kuitafuta, walizunguka sehemu kubwa kwa ndege hizo za kasi, walitumia mpaka satalaiti zao lakini kitu cha ajabu kabisa, hawakuweza kufanikiwa kuipata.
“Labda itakuwa imekwama kwenye milima mirefu!” alisema mwanaume mmoja.
“Kwa hiyo?”
“Tuzitume ndege zikaangalie huko,” alisema mwanaume mwingine.
Hilo ndilo lililofanyika, haraka sana ndege zikatumwa na kuelekea katika milima mikubwa kama Evarest, Himalaya na mingine kwenda kuangalia ili kuona kama ndege hiyo ilikuwa imekwama huko.
Baada ya saa kadhaa tangu watu hao waondoke, simu ikapigwa na kuambiwa kwamba ndege hiyo haikuonekana huko, haikuwepo kitu kilichomaanisha kwamba walitakiwa kwenda kuangalia sehemu nyingine.
Hiyo iilikuwa ni siku ya kwanza kupotea kwa ndege hiyo, dakika zilikatika, saa zilikimbia, siku ya pili ikaingia lakini hakukuwa na taarifa zilizosema mahali ambapo ndege hiyo ilipokuwa.
“Hebu wasilianeni na CIA tuone watatuambiaje,” alisema mwanaume mmoja na hivyo simu kupigwa huko.
Wao ndiyo waliokuwa na nguvu ya kupiga simu katika kampuni ya Kimarekani ya CPS Engeneering iliyokuwa jijini Washington DC ambao walikuwa watu pekee waliokuwa na jukumu la kutengeneza injini za ndege kubwa za Boeing na kuwauliza kuhusu ndege hiyo.
Bosi wa kampuni hiyo, haraka sana akawasiliana na vijana wake wa IT na kuzungumza nao. Kwa kawaida, kwenye kila injini ya ndege kubwa waliyokuwa wakiitengeneza, kwa ndani waliweka GPS kwa ajili ya kuifuatilia kila mahali ilipokuwa ikienda.
Hilo lilikuwa suala la siri sana ambalo halikuwa likijulikana zaidi ya vijana hao wa IT, bosi wa kampuni hiyo na baadhi ya viongozi wa Kijasusi kutoka hapo CIA.
Vijana hao walipoambiwa kuhusu kupotea kwa ndege hiyo, wakaingia kwenye kompyuta zao na kuanza kuitafuta huku wakiliandika jina la ndege hiyo, namba ya injini yake, ikaja na kuanza kuzunguka kila kona wakiitafuta.
Kazi ilikuwa kubwa, kabla ya saa moja asubuhi, ilikuwa ikionekana, GPS ilisema kwamba ilikuwa usawa wa Bahari ya Atlantiki ikielekea katika Bara la Ulaya lakini baada ya muda fulani, hata GPS yenyewe haikuweza kusoma kitu kilichowashangaza hata wao wenyewe.
“Hii ndege itakuwa imeanguka kwenye maji,” alisema kijana mmoja.
“Kipi kinachokufanya kufikiria hivyo?”
“Ni kwa sababu kifaa cha GPS kimeacha kusoma ndege ikiwa usawa wa bahari, inawezekana kabisa iliangukia baharini na hivyo kifaa kuingia maji na kuzima,” alisema kijana huyo.
Taarifa hiyo ikapelekwa mpaka makao makuu ya CIA, hakukuwa na sababu ya kubaki ofisini tu bila kufanya juhudi za kuwatuma watu kwenda huko. Simu ikapigwa na wanajeshi wa majini wakaanza kuelekea huko wakiitafuta ndege hiyo.
Ilikuwa kazi kubwa ambayo hawakuwahi kukutana nayo kabla, walizunguka kila kona, walitumia vifaa vikubwa kuingia ndani ya bahari, huko walikutana na meli zilizozama, ndege nyingine ambazo ziliwahi kuanguka lakini hawakuweza kukutana na ndege hiyo kubwa.
Wakati wao wakiendelea na utafutaji, dunia nzima ilikuwa ni kilio tu, watu walihuzunika, zaidi ya abiria 550 hawakujulikana walipokuwa.
Lilikuwa jambo baya na gumu kuvumilika, wengi waliendelea kuilaumu serikali ya Marekani kwani waliamini kabisa kwamba walikuwa watu ambao waliipoteza ndege hiyo kwa malengo yao binafsi na ndiyo maana hawakutaka kulizungumzia sana suala hilo.
Rais wa Marekani kipindi hicho, Bwana Powell Ludovick akaingiwa doa, kwake, kitendo cha kupotea kwa ndege hiyo na wakati alikuwa na nguvu katika taifa kubwa kama Marekani ilionekana ni kama dharau, hakutaka kuona kila mtu akiizungumzia Marekani kwa ubaya hivyo kuwaagiza watu wake wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha ndege hiyo inapatikana haraka sana.
“Tunajitahidi mkuu!” alisema Mkurugenzi wa CIA, Bwana Matt.
“Fanya kila liwezekanalo, tuna muda mfupi,” alisema Powell.
Siku ya tatu ikaingia, ya nne nayo ikaja, mpaka wiki inakatika bado hapakuwa na taarifa rasmi ya kuzungumzia mahali ndege hiyo ilipokuwa.
Hilo lilikuwa jambo lililoshangaza, ndege nyingi zilizokuwa zimepotea zilionekana isipokuwa ndege hiyo tu ambayo watu wengi walihisi inawezekana ilitoka nje ya dunia na kwenda katika sayari nyingine.
Wakati mwingine hata jambo hilo lilionekana kuwa gumu kukubalika kwani kwa jinsi habari hiyo ilivyokuwa gumzo duniani, jinsi ilivyokuwa ikisumbua vichwa vya watu wengi basi NASA (National Aeronautics and Space Administration) ambayo ilihusika na masuala ya anga isingebaki kimya, ni lazima wangesema mahali ndege hiyo ilipokuwa kama tu ingekuwa imetokea nje ya dunia hii.
Watu waliokuwa na ndugu zao ambao walikuwa ndani ya ndege hiyo wakaanza kuzika nguo za watu hao kwa kuamini hapakuwa na dalili zozote za kuwapata watu hao na inawezekana kabisa huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.
Ilikuwa ni huruma, makaburi ya pamoja yalijengwa haraka na watu kuzika nguo na vifaa vingine vya ndugu zao waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Kama kulalamika, walifanya hivyo sana, walilia mno lakini hakukuwa na kilichobadilika, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa ndugu zao, yaani ndege ile iliwezekana ilikuwa mahali fulani, huko, ililipuliwa na volkano au ilianguka katika Bara la Antaktika ambako hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akiishi huko kutokana na baridi kali.
Japokuwa watu walikuwa wakilia na kuomboleza, hapakuwa na mtu ambaye alijua kilichokuwa nyuma ya ndege hiyo kubwa.
Kati ya watu 550 waliokuwa ndani ya ndege hiyo, pia ndani yake iliwabeba watu watano, wasiojuana ambapo kila mmoja nyuma yake alikuwa na stori nzito ya maisha yake.
Ili kwa baadhi ya watu sehemu nyingine wawe na amani, furaha ilikuwa ni lazima watu hao wafe, wapotee katika mazingira ya kutatanisha ambayo kusingekuwa na mtu yeyote atakayejua kama walikuwa wameuawa.
Humo ndani ya ndege watu hao watano hawakujuana lakini walikuwa na mambo makubwa maishani mwao. Kama watu hao wangefika salama huko walipokuwa wakienda ilikuwa ni lazima dunia ichafuke, ili dunia iendelee kuwa sehemu salama, ilikuwa ni lazima kifanyike kile kilichofanyika.
Ni stori za watu watano tu ambao leo hii walisababisha zaidi ya abiria 550 kutokujulikana mahali walipokuwa. Ni hao watu watano ndiyo waliosababisha kipindi hicho dunia nzima ilie na kuomboleza kwa kuamini kwamba kweli ndege hiyo ilipotea na kwenda kulipuka sehemu fulani.

Kwa sababu simulizi ya Biashara ya Kifo inakaribia mwishoni, nimeanza na hii simulizi mpya huku tukiendelea kusubiri ile iishe.

Je, nini kitaendelea?
 
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.

Sehemu ya Pili.

HISTORIA YA MTU WA KWANZA KATI YA WALE WATANO ILIYOMFANYA KUWA NDANI YA NDEGE HIYO.

Mtu wa kwanza ndani ya ndege

“Natalie! Tell me, what the is going on?” (Natalie, niambie, ni kitu gani kinaendelea?) aliuliza mwanaume mmoja aliyevalia suti ambaye alisimama mbele ya msichana mmoja mrembo wa sura, mwenye umbo namba nane ambaye alikuwa na sura ya kitoto, vishimo mashavuni mwake vilivyomfanya kupendeza zaidi.
“Nothing Gabriel,” (hakuna kitu) alijibu Natalia huku akimwangalia mwanaume huyo aliyeitwa Gabriel aliyekuwa akimwangalia katikati ya macho yake.
Bado Gabriel alihisi kabisa kulikuwa na tatizo mahali fulani, alimfahamu Natalia, alikuwa ndugu yake, alimzoea, kila alipokuwa na tatizo alijua kabisa kwamba kulikuwa na kitu kinaendelea.
Kwa jinsi alivyoonekana siku hiyo alijua kabisa kulikuwa na kitu kikubwa kilichokuwa kikimtatiza. Natalie alikuwa dada yake wa damu, walikua pamoja na walifanya mambo mengi wakiwa pamoja. Siku hiyo msichana huyo alionekana kuwa tofauti. Akamsogelea na kuanza kuzungumza naye kwa karibu zaidi.
Natalia alikuwa mtawa ambaye alimaliza masomo yake katika kanisa lililokuwa Stockholm nchini Sweden. Alisoma huko kwa miaka mitatu na hatimaye kumaliza na kuwa mtawa aliyekamilika ambaye katika maisha yake yote alijiahidi kwamba angemtumia Mungu mpaka siku atakapoingia kaburini.
“Kuna nini? Natalia, kuna jambo unanificha,” alisema Gabriel huku akimwangalia ndugu yake huyo.
“Ninaumia moyoni mwangu! Hivi Mungu anaujua huu uchafu unaofanyika humu kwa baadhi ya watu waliokosa hofu yake?” aliuliza Natalie huku akimwangalia Gabriel.
“Uchafu gani?”
“Hapana! Nitakwambia siku nyingine!” alisema Natalia.
Hilo ndilo jambo lililomuumiza kichwa Gabriel, hakutaka kumuona ndugu yake huyo akiwa kwenye hali hiyo, alichanganyikiwa, moyo wake ulimuuma kupita kawaida.
Akakosa amani, furaha, kila alipomwangalia moyo wake ulimwambia kwamba kulikuwa na jambo hatari lililokuwa likiendelea nyuma ya maisha ya msichana huyo mrembo.
Alichokifanya ni kuanza kumfuatilia. Kila siku asubuhi alikuwa mtu wa kwanza kwenda katika mlango wa chumba cha msichana huyo na kuanza kusikiliza kwa siri.
Alifanya hivyo kwa kuwa alihitaji kujua kilichokuwa kikiendelea huko, hakusikia kama Natalie alikuwa akiwasiliana kwa simu kwani muda wote alikuwa mtu wa kusali huku maneno yake yakisikika kama yakimlalamikia Mungu kwa kile kilichokuwa kikiendelea kutokea kila siku.
Haikuwa nyakati za asubuhi tu, hata alipokuwa akienda mlangoni hapo usiku na kusikiliza, sala yake ilikuwa ileile kwamba kulikuwa na jambo kubwa lililokuwa likiendelea, kwa nini Mungu hakuingilia kati?
“Kuna jambo gani hapa?” aliuliza Gabriel huku akionekana kuchanganyikiwa.
Upelelezi wake kwa ndugu yake huyo haukuisha, kila siku alihakikisha anamfuatilia taratibu, kila alipotoka nyumbani na kwenda kanisani, alikuwa nyuma yake, hakupenda kumuona akiwa kwenye hali hiyo, alitamani kumuona akiwa na furaha kila siku katika maisha yake, hivyo ilikuwa ni lazima kuhakikisha anafanya kila liwezekanalo ili msichana huyo anakuwa na tabasamu muda wote.
Hakuwa akimfuatilia kanisani tu, hata alipokuwa akitoka kwenda kwenye mizunguko yake alikuwa akimfuatilia kwa nyuma.
Alimuona Natalie akienda kwenye mgahawa na kukutana na wasichana wengine wawili ambao nao walikuwa watawa kama alivyokuwa na kuanza kuongea nao.
Alikaa kwa mbali na kuwaangalia kwa darubini, kwa jinsi walivyoonekana, mazungumzo yao waliyokuwa wakiongea hayakuwa ya kawaida hata kidogo, nyuso zao zilionyesha kabisa kulikuwa na kitu kikubwa kilichokuwa kikiendelea katika maisha yao, kitu ambacho walikifanya kuwa siri kubwa mno.
Gabriel hakuwa na uwezo wa kuwafuata na kusikiliza mazungumzo yao ila aliona kabisa kwamba alikuwa na uwezo wa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha anayapata mazungumzo yao yote.
Alichokifanya ni kuanza kutafuta kinasa sauti madukani ambacho ndicho angekitumia kunasa mazungumzo hayo. Alihangaika kwenye maduka na hatimaye kukipata kimoja hivyo kujipanga kukiweka katika mkoba wa Natalie ili siku akienda kuonana na wale marafiki zake asikie kile kilichokuwa kikizungumziwa.
Siku zikaendelea kukatika, kila siku ilikuwa ni lazima kwa Natalie kwenda kuonana na marafiki zake hao kwenye mgahawa ule na kuanza kuzungumza.
Kitendo cha kufika mahali hapo mara kwa mara kikawafanya hata wahudumu wa hapo kuwazoea na kuanza kuwaita majina kila walipokuwa wakihudumia.
Gabriel aliacha kufanya mambo yake, alitamani sana kujua kilichokuwa kikiendelea. Alimkumbuka Natalie jinsi alivyokuwa akisumbua kila siku nyumbani kwamba alitamani kuwa mtawa siku moja, ilikuwa ndoto yake ambayo ilikua na kukua na hatimaye kuitimiza na kwenda kusoma huko nchini Sweden.
Japokuwa alisoma na kuhitimu lakini msichana huyo hakukuwa na furaha hata kidogo, alionekana kuwa na maisha fulani ambayo yalikuwa ni ya siri sana yaliyomtisha mno Gabriel.
“Natalie, nakumbuka siku ambayo ulituambia nyumbani kwamba ulitamani sana siku moja uwe mtawa, unakumbuka?” aliuliza Gabriel huku akimwangalia msichana huyo.
“Nakumbuka!”
“Kila mmoja alikuwa akikuombea kwamba ukamilishe ndoto yako, sijui unakumbuka?”
“Nakumbuka sana.”
“Kuna siku baba alituamsha usiku na kusema anahitaji kusali nasi kwani alihisi kabisa hakuwa na siku nyingi za kuishi. Nakumbuka kabisa tulipiga magoti na kutuombea tutimize ndoto zetu, unakumbuka na hilo pia?” aliendelea kuuliza Gabriel.
“Ndiyo!”
“Hatimaye leo hii umetimiza ndoto yako na kuwa mtawa.”
“Namshukuru Mungu kwa hilo.”
“Sasa kwa nini huna furaha sasa?” aliuliza Gabriel.
Natalie akanyamaza, akauinamisha uso wake chini na kuanza kulengwa na machozi na ndani ya sekunde kadhaa yakaanza kudondoka moja kwa moja mpaka sakafuni.
Gabriel alijua kabisa kulikuwa na jambo moja katika kutimiza ndoto hiyo na ndiyo maana kila alipokuwa akimuuliza kuhusu jambo hilo msichana huyo alikuwa akilia.
Gabriel hakutaka kukubali, ilikuwa ni lazima ajue kile kilichokuwa kikiendelea. Alimlazimisha sana Natalie kumwambia kila kitu ambacho kilisababisha machozi yake kutoka kila siku lakini msichana huyo hakutaka kukubali.
“Kwa nini hutaki?”
“Nikikwambia! Kesho tu utauawa!” alijibu Natalie jibu ambalo lilimshtua Gabriel.
“Yaani nitauawa?”
“Ndiyo! Utauawa.”
“Na nani?”
“Kuna siri kubwa sana Gabby! Usione kwamba sitaki kukwambia ukweli, ninaona kabisa utauawa kama tu utajua ukweli,” alisema Natalie.
“Sawa. Tufanye kwamba mimi mwenyewe nataka kufa, kwa nini usiniambie?”
“Nitakwambia siku nyingine.”
“Natalie...”
“Nitakwambia siku nyingine,” alisema Natalie, hapohapo akachukua simu yake na kupiga sehemu, baada ya sekunde kadhaa akawa anazungumza na msichana mmoja ambaye alimwambia kwamba waonane kama ilivyokuwa siku nyingine.
Wakati msichana huyo akiwa bafuni anaoga, haraka sana Gabriel akaenda chumbani kwa Natalie na kukiweka kile kinasa sauti kwenye mkoba wake ili kama ingetokea angetoka nao basi aweze kunasa mazungumzo ambayo yangekwenda kuzungumziwa siku hiyo.
Akarudi sebuleni, alibaki akimuomba Mungu kwamba msichana huyo achukue mkoba wake na kuondoka nao ili ajue ni kitu gani kilikuwa kikikiendelea.
Baada ya dakika kadhaa, Natalie akatoka huku akiwa amevalia vazi lake la kitawa,shingoni akiwa na rozali kubwa na kuondoka nyumbani hapo huku akiwa na mkoba wake kitu kilichomfanya Gabriel kumshukuru Mungu.
Haraka sana akachukua kompyuta yake, akaweka headphone na kutaka kusikiliza kile kilichokuwa kikizungumziwa kila wasichana hao walipokuwa wakikutana katika mgahawa huo.
Natalie alipofika na kukaa tu, Gabriel akaanza kusikiliza mazungumzo yao waliyokuwa wamepanga kuongea siku hiyo. Hakwenda kuwaona, kusikia sauti tu kwake ilitosha kabisa kujua kile kilichokuwa kikiendelea huko.
“Umewasiliana nao?” aliuliza Natalie.
“Ndiyo! Walisema kwamba watakuja niwape ushahidi wa picha ili waupeleke makao makuu lakini hawakuwasiliana nami tena na kuna taarifa nilizipata kwamba wameuawa,” alisikika msichana mmoja.
“Mh! Mbona jambo hili linanitisha sana?” aliuliza Natalie.
“Yaani wewe acha. Kama itatokea na mimi nikauawa, nina picha zote za ushahidi, nimezificha nyumbani kule chini kwenye shimo, humo, kuna kisanduku ambacho kipo nyuma ya picha ya Yesu, ukiitoa hiyo picha, utakutana na hicho kisanduku ambacho kinafunguliwa kwa namba ya siri ambazo ni 2728,” alisema Mary.
“Mary! Hautokufa, hautouawa mpaka tufanikiwe katika hili!” alisema Natalie.
“Nani atatusaidia kama watu tunaotaka watusaidie wanauawa kila siku?” aliuliza msichana mwingine.
“Anna! Nadhani tunatakiwa kulifikiria hili kwanza, ila ni lazima hizi habari zifike makao makuu! Nilitamani sana kuwa mtawa, sikuamini kama walewale maaskofu wangu ndiyo ambao wangenibaka na kuniuza kwa matajiri ili wafanye na mimi mapenzi kwa sababu ya kupata pesa za kuendesha maisha yao! Siwezi kukubali,” alisema Natalie huku akisikika akianza kulia kwa kilio cha kwikwi.
“Ni lazima tufanye kila liwezekanalo kuhakikisha dunia nzima inajua huu unyama. Natalie, picha zako siku ulipokuwa unafanyiwa matukio hayo zipo?” aliuliza Anna.
“Ninazo! Na kama itatokea nikauawa, picha zangu zipo chumbani kwangu, nimeziweka chini ya kapeti, kuna sehemu ina kishimo ambacho humo ndipo picha zilipo,” alisema Natalie.
Huku nyuma ambapo Gabriel alikuwa akisikiliza kwenye kompyuta yake, aliposikia kwamba picha hizo zilikuwa chumbani kwa Natalie, akaenda, akaufungua mlango kwa ufunguo wa akiba na kuingia ndani.
Mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa hasira, hakuamini maneno yale aliyoyasikia, machozi yalimtoka, kitendo alichofanyiwa ndugu yake kiliugusa moyo wake.
Aliamini alikwenda kusomea utawa, alijichunga dhidi ya wanaume mpaka alipokwenda huko kukamilisha ndoto yake lakini kitu kilichotokea ni kwamba alianza kutumikishwa kingono na watu walioitwa maaskofu.
Alipofika chumbani, akaenda mpaka sehemu aliposikia, akafungua kapeti na kuona hiyo sehemu ambayo akaifungua na kukutana na bahasha ambayo akaichukua na kuangalia ndani.
Alikutana na picha, alipoziangalia, uchungu mkubwa, hasira zikaushika moyo wake, akajikuta akikaa chini na kuanza kulia.
Picha zile zilimuonyesha tajiri mmoja akimbaka dada yake, tajiri huyo alionekana kuwa na furaha, alikuwa akijipiga picha ambazo inawezekana Natalie baadaye aliziiba.
Haikuishia hapo tu, pia aliziona picha nyingine zikimuonyesha dada yake na wasichana wengine wakibakwa na watu wengine ambao aliwafahamu kabisa, walikuwa mabilionea ambao kwa maneno waliyokuwa wakizungumza walisema kwamba waliuzwa kwa mabilionea na kwenda kufanya nao mapenzi kisiri, tena walilazimishwa huku bastola zikiwa pembeni.
Haraka sana Gabriel akazichukua zile picha na kwenda kuziprinti kwenye kompyuta chumbani kwake na kubaki na kopi kama ushahidi na kuzirudisha zile orijino palepale alipozichukua, akatoka na kwenda chumbani kwake kuendelea kusikiliza mazungumzo yao.

Je, nini kitaendelea?
Tumeanza kuelezea historia ya mtu wa kwanza kati ya wale watano, tujue sababu ni kwa nini alikuwa ndani ya ndege hiyo, alitoka wapi na alikuwa akienda wapi, na kufanya nini.
Tukutane siku ya Jumamosi kwa muendelezo
 
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.

Sehemu ya Tatu.

Wasichana hao watatu walifanyiwa mambo ya kinyama, hawakuwa na mahali pa kusemea kwa kuwa waliogopa kuuawa kama walivyouawa wengine, ilikuwa ni lazima watafute mtu ambaye angeyapeleka malalamiko yao katika uongozi wa Kanisa la Living Christ lililokuwa maarufu duniani na kuzungumza kile walichokuwa wakifanyiwa huko chuoni.
Hawakujua ni nani ambaye alistahili kuambiwa maneno hayo na kumpa picha hizo kwa sababu kila mtu ambaye walijaribu kufanya mawasiliano naye, aliuawa hata kabla hajawafikia na kuwapa picha zile za kuzipeleka makao makuu yaliyokuwa nchini Ubelgiji kwa ajili ya maaskofu hao kuchukuliwa hatua.
Baada ya kuziangalia picha zile, Gabriel akarudi kwenye kompyuta yake na kuendelea kusikiliza, alijua mahali picha za wasichana wawili zilipokuwa lakini hakujua mahali picha nyingine za Anna alipozificha na ilikuwa ni lazima kujua mahali zilipokuwa ili siku ambayo angezihitaji basi angekwenda kuzichukua.
Wakati akiwa hapo tayari kwa kuwasikiliza, alisikia kelele za treni na kugundua kwamba walimaliza kuzungumza na hivyo kila mtu kutawanyika.
Gabriel alibaki chumbani kwake akilia kwa maumivu makali, hakuamini kama kile kilichokuwa kimetokea, watu ambao walikuwa wakiaminika, waliokuwa wakiendesha ibada kila siku ndiyo ambao waliwafanyia wasichana hao matendo ya ngono kwa kuwachukua na kuwapeleka katika makasri ya matajiri na kuwafanyisha ngono.
Hilo lilimuuma kupita kawaida na kujiapiza kwamba ni lazima dunia ijue kile kilichotokea, ni lazima picha hizo zifikishwe makao makuu ya kanisa hilo na kuwaonyeshea uovu uliokuwa ukifanywa na maaskofu ambao kila Jumapili walikuwa wakisimama mbele ya kanisa na kuwaambia watu kwamba waache uovu.
“Ni lazima nitapeleka ushahidi wa picha zote, hata kama itatokea nitauawa, basi niuawe nikiwa nimekwishafika nchini Ubelgiji,” alisema Gabriel huku akijiapiza kwamba ni lazima afanye jambo kuwaokoa wasichana wengine waliokuwa wakienda kusomea utawa katika vyuo vya kanisa hilo.
***
Kanisa la Living Christ lilikuwa miongoni mwa madhehebu makubwa kabisa duniani ambalo lilikuwa na wafuasi zaidi ya milioni mia mbili na themanini duniani kote.
Mbali na dhehebu la Kiroma ambalo lilikuwa na wafuasi wengi duniani, kanisa hilo lilikuwa likishika nafasi ya pili kwa kuwa na watu wengi duniani nyuma ya Waroma.
Kila nchi makanisa makubwa yalijengwa huku yakiongozwa na watu waliokuwa na vyeo vya maaskofu, tofauti na Waroma ambao waliongozwa na mapadri.
Living Christ nao walikuwa na watawa ambao walitakiwa kusomea masomo maalumu kwa ajili ya kulitumikia kanisa hilo maisha yao yote.
Kila msichana ambaye alitakiwa kujiunga na kozi ya utawa, sharti la kwanza kabisa lilikuwa ni kuchunguzwa kama alikuwa bikira.
Hiyo ilikuwa ni kazi maalumu iliyofanywa na askofu mmoja aliyeitwa kwa jina la David Ishmael ambaye yeye ndiye alikuwa akithibitisha kwamba huyu alitakiwa kwenda au kuachwa.
Askofu huyo alikuwa nchini Ubelgiji yalipokuwa makao makuu ya kanisa hilo. Kila siku alikuwa akipokea wasichana wadogo ambao walikuwa na ndoto za kuwa watawa ili wamtumikie Mungu maisha yao yote.
Kila aliyekuwa akiingia ndani ya ofisi yake na kutaka kujiunga na chuo cha kanisa hilo ilikuwa ni lazima amwangalie kama alikuwa bikira au la, na kama alikuwa na sifa ya kuwa bikira, ilikuwa ni lazima aitoe, msichana ambaye angekataa basi asingeweza kujiunga na chuo hicho.
Msichana Natalie alifika hapo, ndani ya chumba hicho akiwa na furaha tele. Alisafiri kutoka nchini Marekani kwa ajili ya kwenda kuchukua masomo ya utawa na kumtumikia Mungu maisha yake yote.
Alijitunza, hakumruhusu mwanaume yeyote yule auguse mwili wake, alimuwekea ahadi Mungu wake kwamba katika maisha yake yote angekuwa bikira na ndiyo maana aliamua kuwa mtawa huku akiacha kufanya mambo mengine maovu.
“Hii imekuwa ndoto yangu kwa kipindi kirefu, hakika ninakwenda kuitimiza, nitamtumikia Mungu maisha yangu yote,” alisema Natalie huku akiwa katika viti nje ya ofisi ya Askofu David akisubiri kuingia ndani..
Baada ya dakika chache zamu yake ambaye ndiye alikuwa mtu wa mwisho akaingia ndani ya ofisi ya Askofu David na kuanza kufanyiwa usaili.
Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya mwisho, askofu huyo ndiye alikuwa mtu wa mwisho kudhihirisha kwamba msichana fulani alikuwa bikira au la.
Kwenye nafasi hiyo hawakutaka kumuweka mwanamke, kwenye dhehebu lao hawakuwaamini wanawake, walitaka kila kitu kifanywe na mwanaume na ndiyo maana hakukuwa na askofu wa kike kwa kuwa tu hata enzi za Mfalme Daudi hakukuwa na mwanamke yeyote aliyepewa madaraka ndani ya kanisa.
“Unaitwa nani?” aliuliza Askofu David huku akimwangalia Natalie aliyeonekana kuwa na furaha ya ajabu.
“Natalie Andrew.”
“Unahisi una vigezo vya kuwa mtawa katika kanisa letu?” aliuliza Askofu David huku tayari tamaa ya mwili ikiwa imeanza kumkamata.
“Ndiyo baba askofu!” alijibu msichana huyo, Askofu David akaangalia mitihani aliyoifanya, alifaulu vizuri ila alitaka kuhakikisha kitu kimoja tu, kama alikuwa bikira au la.
“Hebu panda hapo juu ya meza, vua nguo zako,” alisema Askofu David maneno yaliyoonekana kumshtua Natalie.
“Unasema?”
“Nataka nione kama wewe ni bikira kweli,” alisema askofu huyo.
Natalia akawa na moyo mzito kufanya kile alichoambiwa, maishani mwake mwote alijiapiza asingefanya mapenzi na mwanaume yeyote yule, na si hivyo tu bali hata kuuona utupu wake.
Kulikuwa na wanaume wengi waliomfuata kwa ahadi mbalimbali lakini aliwakatalia, kitendo cha askofu kumwambia apande juu ya meza na kuvua nguo zake ili ahakikishe kama alikuwa bikira ulikuwa mtihani mzito mno.
Huku akiwa anafikiria ni kitu gani alitakiwa kufanya, akamuona askofu huyo akianza kuvua nguo zake na kubaki mtupu kama alivyozaliwa.
“Panda juu ya meza nikuchunguze,” alisema askofu huyo huku akichezea sehemu zake za siri.
Natalie alibaki akishangaa, hakuamini kile alichokuwa akikiangalia, hakuamini kama ile ndiyo staili ambayo Askofu David alikuwa akiifanya ili kuona kama mtu fulani alikuwa bikira au la.
Alitamani kutimiza ndoto aliyokuwanayo tangu utotoni lakini kile alichotaka kufanyiwa kilionekana kuwa kama unyama fulani.
“Hii ndiyo nafasi yako ya mwisho! Kama ni bikira, basi umepita, ila kama si bikira, utarudi kwenu, na kama utakwenda kumuhadithia mtu yeyote kile kilichotokea humu, kanisa litatumia nguvu zake kukumaliza kama lilivyowamaliza wengine,” alisema askofu huyo maneno yaliyomtisha msichana huyo.
Hakuwa na la kufanya, hakukubali kuona akikosa nafsi ya kuwa mtawa, kitu ambacho alikitamani tangu alipokuwa mdogo.
Yeye mwenyewe akapanda juu ya meza, macho yake yakaanza kuwa mekundu, akawa analia lakini askofu David hakutaka kujali, akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine mpaka kumuacha mtupu kabisa.
Natalie hakuamini kama bikira yake alikuwa akienda kuipoteza ndani ya ofisi hiyo, kila alipomwangalia askofu David ambaye alikuwa mzee sawa na umri wa baba yake alibaki akilia tu.
Mwanaume huyo akamlalia kwa juu na kuanza kumbaka juu ya meza hiyo. Alisikia maumivu makali chini ya kitovu, damu zikaanza kumtoka mfululizo, alilia lakini askofu huyo hakutaka kujali, ndiyo kwanza alikuwa akienda juu na chini kuhakikisha bikira ya Natalie inatoka ndani ya ofisi hiyo.
Hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kuumiza maishani mwake kuliko siku nyingine. Alilia sana lakini askofu huyo hakujali, alifanya naye kwa dakika kumi ndipo akamwambia kwamba amepita, ni kweli alikuwa bikira hivyo angepelekwa nchini Sweden kwenda kusoma.
Hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake aliyokuwa akiifanya miaka yote, hakukuwa na kiongozi wa kanisa aliyejua, ilikuwa ni siri ya wasichana waliokuwa wakifanyiwa usaili mahali hapo, mbaya zaidi hapakuwa na yeyote aliyediriki kusema kilichokuwa kikitokea huko kwa kuogopa kufukuzwa.
Siku hiyo alikaa na kulia sana, hakuwa peke yake, kulikuwa na wasichana wengine wawili, Anna na Mary ambao nao walifanyiwa vilevile kama alivyofanyiwa yeye na wote walikuwa wakilia tu.
Walibembelezana na siku iliyofuata wakaondoka na kuelekea chuoni huko Sweden ambapo huko wakaanza masomo yao katika chuo cha kanisa hilo.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa na furaha tena, si wao tu bali hata wasichana wengine waliokuwa chuoni hapo walionekana kuwa kama wao.
Walijua kabisa kwamba na hao pia walifanyia mambo ya kinyama kama walivyofanyiwa wao. Walisoma huku kila mmoja akiahidi kwamba kitendo cha kufanya mapenzi na Askofu David angekuwa mtu wa mwisho na wasingeweza kufanya tena mpaka siku watakazoingia kaburini.
Wakati wakiendelea na masomo chuoni hapo huku kila siku wakisali na kumuabudu Mungu, wakaanza kuona mambo yasiyokuwa ya kawaida yakiendelea chuoni hapo.
Kila siku ya Jumapili wasichana watatu walikuwa wakichukuliwa na kuondoka kuelekea nje ya chuo hicho na kurudi usiku wa manane. Kila walipouliza, waliambiwa walipelekwa katika ibada maalumu na viongozi wengine kwa ajili ya kuyaombea mataifa yaliyokuwa na vita.
Hilo likawatia hofu, hawakuamini kama kile walichoambiwa ndicho kilikuwa ukweli. Walikaa chuoni hapo kwa hofu kubwa mpaka wakati mwingine wakajutia ndoto zao za kutamani kuwa watawa kama walivyokuwa.
Baada ya miezi mitatu, wakaambiwa nao walihitajika na kiongozi wa chuo hicho kwani kulikuwa na jambo muhimu walilotakiwa kuambiwa.
Kwanza wakashtuka, mara nyingi watu waliokuwa wakiitwa katika ofisi ya mkuu wa chuo ilikuwa ni kwa wale wasichana waliotakiwa kwenda kuhubiri neno la Mungu nje ya chuo hicho kama walivyofanya wale wengine.
“Kuna nini?” aliuliza Natalie huku akionekana kuwa na hofu.
“Mh! Sijui! Ila ninachohisi na sisi tunatakiwa kutoka usiku kwenda kufanya maombi na viongozi,” alisema Anna huku akionekana kuwa na hofu.
“Kutoka nje ya chuo?”
“Ndiyo! Nimesikia hivyo! Mungu wangu, hivi kwa nini nilitaka kuwa mtawa?” alisema Anna huku akianza kulia huku akiilaani siku ambayo alipata ndoto ya kuwa mtawa.
“Hebu twendeni, labda kuna jingine,” alisema Mary.
Wakaanza kwenda huko.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumatatu hapahapa bila kukosa
 
Ni hatari.. Askofu anajivunjia tuu bikra kirahisi rahisi..
.NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.

Sehemu ya nne.

Nathalie, Anna na Mary hawakutaka kwenda kule walipoambiwa watakwenda lakini hawakuwa na jinsi, ni uongozi wa chuo ndiyo uliowaambia kwamba waende kwa sababu kulikuwa na ibada maalumu ambayo huwakutanisha wasichana mbalimbali na maaskofu kutoka nchi nyingine duniani na kufanya maombi ya pamoja.
Walipoambiwa hivyo kidogo wakawa na amani mioyoni mwao na kuhisi kwamba inawezekana kweli kule walipokuwa wakipelekwa kulikuwa na ibada maalumu na kukutana na watu wengine kwa ajili ya kusali pamoja.
Ilipofika majira ya saa tatu usiku, wakaingia ndani ya gari na kuondoka huku wakitangulizana na wazee wawili waliokuwa kwenye uongozi wa juu katika chuo hicho cha utawa.
Walikuwa kimya garini, hawakutakiwa kuzungumza kitu chochote kile. Safari iliendelea kwa zaidi ya saa mbili, gari likatoka ndani ya mji na kuelekea huko mbali kabisa. Ilikuwa ni safari ndefu ambayo hata wao wenyewe walishangaa.
Walitamani kuongea na kuulizana kuhusu safari hiyo lakini hawakuruhusiwa, walinyamaza mpaka gari lile lilipoanza kuingia ndani ya jumba moja kubwa na la kifahari.
Walishangaa, walichokitegemea ni kwamba wangeingia ndani ya kanisa kubwa ambalo ndilo waliambiwa kulikuwa na ibada iliyokuwa ikiendelea na maaskofu wengine.
Kwa jinsi walivyoliangalia jumba lile, walijua kabisa sehemu hiyo haikuwa salama hata kidogo, hivyo wakasubiri kuona ni kitu gani ambacho kingetokea.
Wanaume watatu waliokuwa na bunduki wakalisogelea gari lile na kuufungua mlango kisha kuwataka kuteremka.
Walishtuka, kitendo cha kuona watu hao wakiwa na bunduki kikawapa uhakika kabisa kwamba sehemu hiyo haikuwa salama kwani kama ni kanisani, kulikuwa na ibada kusingekuwa na watu waliokuwa na bunduki kama walivyokuwa.
Wakaingizwa ndani ya jumba hilo, lilikuwa la kifahari, walikaa kwenye masofa makubwa huku wakionekana kuwa na hofu kupita kawaida.
Kwenye kuta za jumba hilo hapo sebuleni kulikuwa na picha kadhaa za wanawake waliokuwa uchi wa mnyama, wengine walikuwa wakifanya mapenzi na wanaume mbalimbali, kwa jinsi ilivyoonekana tu, hawakuwa na maswali zaidi, walijua kile ambacho kilikuwa kikienda kutokea ndani ya jumba hiyo.
Wakati wakiwa wametulia, wanaume watatu wakafika sebuleni hapo, walikuwa ni wazee wa umri kuanzia miaka hamsini, walivalia mataulo huku wakiwa na vitambi vya saizi ya kati.
Wakawaangalia wasichana hao, nyuso zao zikaonyesha tabasamu pana na kufurahia uwepo wao ndani ya nyumba hiyo.
“I want that one,” (namtaka huyo) alisema mzee mmoja huku akimuonyeshea kidole Nathalie.
Wanaume hao walijichagulia wasichana hao kama walikuwa sokoni, Nathalie na wenzake walibaki wakishangaa, hawakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, ilikuwaje wapelekwe sehemu hiyo na wakati waliambiwa walikuwa wakienda kuungana na maaskofu kwa ajili ya kufanya ibada?
Wale viongozi waliowapeleka wakaanza kuwaambia maneno ya vitisho kwamba kila kitu ambacho kingetokea mahali hapo kilitakiwa kuwa siri kubwa na kama kungekuwa na mtu yeyote angethubutu kuitoa siri hiyo basi ilikuwa ni lazima auawe kama wengine.
Hawakuishia hapo, waliendelea kuwaambia hiyo ndiyo ilikuwa siri ya kanisa hilo kubwa kujiendeleza. Lilikuwa na pesa nyingi kwa sababu walikuwa na wafadhili wengi ambao wengine walikuwa wazee hao, mabilionea waliokuwa wakilipa kiasi kikubwa cha pesa.
“Kumbukeni, kwa yeyote atakayetoa siri hii, kichwa chake kitakutwa sokoni, lakini pia kila mtakapokuwa mkifanya mapenzi mtakuwa mkipigwa picha na kurekodiwa. Siku ukitoa siri, picha zinawekwa kwenye mitandao ya ngono kabla ya kuuawa,” alisema kiongozi wao ambaye alionekana kutokuwa na hofu kwa kile kilichokuwa kikienda kutokea.
Hilo ndilo lilikuwa kanisa la Living Christ ambalo lilijiendelea kwa kuwauza wasichana waliokuwa wakisomea utawa katika vyuo mbalimbali.
Biashara hiyo ilikuwa ni ya siri kabisa, watu walipata pesa kwa njia za hatari na hawakutaka dunia ijue wala viongozi wao wa juu kabisa wajue kilichokuwa kikiendelea.
Siku hiyo ilikuwa ni nyingine iliyokuwa na maumivu makali mioyoni mwao, ilikuwa ni siku ambayo iliibadilisha mioyo yao na kuichukia dini ya Kikristo kwa kuamini kwamba madhehebu yote yalikuwa yakifanya kama hivyo.
Walifanya mapenzi huku wakipigwa video, iliwauma, walilia lakini wazee hao hawakutaka kuwaacha, ilikuwa ni kama walikuwa wakiigiza mkanda wa ngono na waigizaji maarufu kama Mandingo, Johnny Sin na wengineo.
Baada ya saa tatu, wakamaliza na hivyo kupandishwa ndani ya gari na safari ya kurudi chuo kuanza. Njiani walikuwa wakilia, hawakuamini kile kilichotokea, waliliamini dhehebu lao, waliwaamini viongozi wao lakini kumbe mwisho wa siku walikuwa wakifanyishwa matendo ya kikatili kama yale.
Bado waliendelea kupigwa mikwara mingi kwamba hawakutakiwa kumwambia mtu yeyote yule kwani vinginevyo wangeuawa kikatili na maiti zao kufichwa sehemu au kwenda kuchomwa moto. Hilo likawaogopesha na hivyo kunyamaza kimya.
***
Mabilionea waliendelea kufanya mapenzi na wasichana wabichi kwa malipo ya dola laki tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya shilingi bilioni moja kwa kila baada ya miaka mitatu.
Hawakuwa na muda wa kwenda mitaani na kununua machangudoa, kitu walichokifanya kilikuwa ni kuwasiliana na viongozi wa vyuo vya watawa na kuamua kuwalipa malipo makubwa lakini kwa makubaliano ya kupelekewa wasichana warembo kila Jumapili.
Ilikuwa ni biashara kubwa na ya siri sana ambayo hakukuwa na watu wengine waliokuwa wakifahamu kama mabilionea hao walikuwa na tabia hiyo ya kuwachukua wasichana wadogo na kwenda kufanya nao ngono kila Jumapili.
Kule chuoni, kila mmoja alikuwa kimya, kile kilichotokea kilitakiwa kuwa siri kubwa, hawakutakiwa kuzungumza kwa mtu yeyote yule, waliambiwa wanyamaze mpaka siku ambayo wangeingia kaburini.
Huo ndiyo ukawa mchezo, kila siku za Jumapili wasichana walikuwa wakichukuliwa na kupelekwa kwa mabilionea hao na kutumikishwa kingono huku pesa wakipewa viongozi wa chuo hicho.
Siku ziliendelea kukatika, siri ikawa mioyoni mwao, si kwamba wao pekee ndiyo waliokuwa wakifanyiwa michezo hiyo bali nusu ya wanachuo chuoni hapo walikuwa wakifanyiwa michezo hiyo hatari.
Baada ya miezi miwili ya kutumikishwa kingono, Nathalie akafahamiana na msichana mwingine aliyekuwa hapo chuoni, msichana huyo aliitwa Magdalena Khan.
Alikuwa mzuri wa sura, alitokea nchini Ujerumani. Kama alivyokuwa yeye hata msichana huyo naye alikuwa na ndoto za kuwa mtawa siku moja.
Alijitunza kwa miaka mingi huku akimuahidi Mungu kwamba angekufa akiwa bikira lakini baada ya kukutana na Askofu David kwenye usaili, ndoto zake zikafia hapo na kuendelea kutumikishwa kingono hata alipokuwa chuoni.
Magdalena alikuwa na hasira kali, hakutaka kuendelea kuona akinyanyaswa kingono katika miaka mitatu yote ambayo angekuwa chuoni hapo, ilikuwa ni lazima apambane, ni lazima atoroke ndani ya chuo hicho na kwenda nje ambapo huko angesimulia kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Alilia sana, alihuzunika, hakuwa na siri moyoni mwake, baada ya kuzoeana kidogo na Nathalie, akaanza kumuhadithia kile kilichokuwa kikiendelea kila alipokuwa akitolewa chuoni na wenzake kupelekwa sehemu.
Alijua hiyo ilikuwa kwao tu kumbe nusu ya wanachuo walikuwa wakitumikishwa kingono kama wengine. Kwa jinsi alivyokuwa akimuhadithia Nathalie, mpaka msichana huyo akaanza kulia, japokuwa yeye aliumizwa lakini kila alipomwangalia Magdalena, Magdalena alionekana kuumizwa zaidi yake.
“Nathalie! Nina mimba,” alisema Magdalena maneno yaliyomfanya Nathalie kushtuka.
“Una mimba?”
“Ndiyo! Ni siri, ninakwambia wewe tu. Nilipopelekwa kule kutumikishwa kingono, niliambiwa na yule mzee tusitumie kinga,” alisema Magdalena huku akilia.
“Umeuambia uongozi?”
“Ndiyo nafikiria kufanya hivyo!” alisema.
Magdalena hakutaka kuwa kimya, alichokifanya ni kumfuata kiongozi ambaye alikuwa akiratibu biashara hiyo na kumwambia kwamba alikuwa na mimba.
Kiongozi huyo aliyeitwa Fonce Thomas akashtuka, hakutegemea kuambiwa kitu kama hicho kwa kuwa aliamini wasichana wenyewe walikuwa wakijitunza kwa kujua siku zao za hatari.
Akamwangalia sana Magdalena, akajua kabisa kwamba kama wangeruhusu msichana huyo aendelee kuwa na mimba hiyo basi ingekuwa hatari kwao na inawezekana kabisa kila kitu kingejulikana.
Akawashirikisha wenzake na kuwaambia kilichotokea, kama alivyoshtuka yeye, hata nao wakashtuka na hivyo kutakiwa kufanya jambo kuficha hilo.
“Mimba itolewe,” alisema Fonce.
“Hapana! Bado ni tatizo! Nimefikiria kitu kimoja,” alisema mwanaume aliyeitwa kwa jina la Michael.
“Kipi?”
“Huyu msichana auawe! Tunatakiwa tutengeneze ugonjwa ambao utamuua ndani ya mwezi mmoja tu, ufanane na kansa, nitazungumza na daktari mmoja na ninaamini atanipa sumu ya kumuua ndani ya mwezi mmoja,” alisema Michael.
Haraka sana Michael akawasiliana na daktari mmoja na kumwambia kilichotokea kwamba kuna msichana mmoja alitakiwa kuchomwa sindano iliyokuwa na virusi vya Vabyrosis ambavyo vilikuwa na nguvu ya kuufanya moyo wa binadamu kuanza kuchakaa na mwisho wa siku kufa huku akionekana kuwa na kansa ya ndani katika moyo wake na mapafu.
Hilo halikuwa tatizo, daktari huyo akakubaliana naye na hivyo uongozi kumchukua Magdalena na kuondoka naye kuelekea huko hospitalini.
Alichoambiwa ni kwamba uongozi haukuwa ukiamini kama kweli alikuwa na mimba hivyo walikuwa na jukumu na kumchukua na kwenda kumpiga ili kujua ukweli.
Walipofika, hawakuuchukua mkojo wake, wakachukua sindano iliyokuwa na virusi vile na kumchoma, baadaye ndipo wakajifanya kuchukua mkojo wake.
“Ni kweli ana mimba,” alisema daktari.
“Basi sawa!”
Akapewa majibu, alilia sana, hakutarajia katika maisha yake kupata ujauzito kwa kuwa alijiahidi angekufa akiwa bikira.
Wakaondoka hospitalini hapo huku akilia. Hakunyamaza, mpaka anaingia bwenini bado alikuwa akilia sana lakini hakumwambia mtu mwingine kilichotokea zaidi ya Nathalie, aliogopa sana kwa kuwa alipewa vitisho kwamba kama angediriki kumwambia mtu yeyote yule basi wangemchinja.
“Imekuwaje?” aliuliza Nathalie, aliamua kumfuata kisiri usiku.
“Nimekutwa nayo! Moyo umeniuma sana,” alijibu Magdalena.
“Kwa hiyo walikupima tu?”
“Ndiyo! Walinichoma na sindano!”
“Ya nini?”
“Sijajua! Daktari alisema anichome sindano tu!”
“Ila mimba si wanapima kwa mkojo! Sasa kwa nini uchomwe sindano?”
“Sijajua! Ila walinichoma sindano! Unahisi kwamba wanataka kuniua?” aliuliza Magdalena huku akilia, alionekana kuogopa kupita kiasi.
“Hawawezi kukuua!”
“Sasa ile sindano ya nini?”
“Sijajua! Ila hawawezi kuua,” alisema Nathalie huku akimtia moyo.
Kitendo cha kuambiwa alichomwa sindano kikaanza kumtia hofu Nathalie, hakujua hasa dhumuni la msichana huyo kuchomwa sindano hiyo.
Akahisi kulikuwa na kitu nyuma ya pazia, hakutaka kumwambia mtu yeyote yule mpaka aone kile ambacho kingeendelea baada ya hapo.
Lilikuwa jambo lisilowezekana kwa msichana kama huyo kupata mimba halafu uongozi usifanye kitu chochote kile, yaani apate mimba, wamuulize tu, akubali, apimwe, ionekane halafu wakae tu, kwake halikuwezekana.
Akawa na hofu, alitamani kuwashirikisha wenzake lakini akasita, alitaka kuona mwisho wa jambo hilo lingekuwa nini, alihitaji kuona kama Magdalena angekufa au la kwani moyo wake ulimwambia hivi; kama kweli msichana huyo alichomwa sindano ambayo hakuijua, basi kuna jambo lingeweza kutokea, hasa mimba kutoka.
Japokuwa Nathalie alitamani sana jambo hilo likae moyoni mwake na asimwambie mtu yeyote, akashindwa hivyo akawashirikisha wenzake kila kitu kilichotokea kwa msichana huyo kwamba aligundulika ana mimba na alipowaambia viongozi walimpeleka hospitalini ambapo huko akachomwa sindano.
Hiyo sindano ndiyo walishindwa kujua ilikuwa na nini, wakaanza kufuatilia huku wakionekana kuogopa kupita kiasi kwani walikwishagundua kabisa mahali hapo hakukuwa salama tena na kama ingetokea kwa mtu yeyote kupata mimba basi kilichokuwa kikifuata ni kuchomwa sindano ile.
Siku ziliendelea kukatika, baada ya mwezi mmoja hali ya Magdalena ikaanza kubadilika, akaanza kuhisi baridi kali huku mwili wake ukianza kuwasha sana, hakujua kilichokuwa kikiendelea, alikuwa mtu wa kukesha usiku akilia kwani hakujua kitu kilichokuwa kikimsibu mpaka kuwa kwenye hali hiyo.
Viongozi walewale wakamchukua na kumpeleka hospitali ambapo huko iligundulika moyo wake haukuwa ukifanya kazi vizuri na alikuwa na muda mfupi wa kuishi hivyo alitakiwa kujiandaa kufa.
Hilo lilimuumiza sana, alichogundua ni kwamba mimba haikuwa ikimpenda, hakukumbuka kuhusu ile sindano aliyochomwa, alichokikumbuka ni kuhusu mimba tu.
Akarudishwa chuoni huku akilia, wanafunzi wakatangaziwa tatizo alilokuwanalo msichana huyo na kwa sababu alikuwa na ugonjwa huo basi walitakiwa kuungana naye kwenye maombi na kuanza kumuombea.
Nathalie na wenzake walilia sana, waligundua kwamba sindano ile ndiyo iliyokuwa imebadilisha kila kitu na wala haikuwa ile mimba. Walikusanyika kanisani na kumuombea Magdalena lakini walijua kabisa kwamba walikuwa wakifanya kitu ambacho kilikuwa ni bure kabisa.
Hali ya afya yake ilizidi kuwa mbaya. Akaanza kukohoa madonge ya damu, ngozi ikaanza kusinyaa huku rangi yake nyeupe ikibadilika na kuanza kufifia na kwa mbali kuanza kupata unjano fulani.
Haikuishia hapo, alianza kukonda na kuwashwa mwili mzima. Magdalena alikuwa kwenye mateso makali, aliteseka, alilia peke yake chumbani kwake na baada ya siku kadhaa, akafariki dunia huku akiwa kitandani hapo.
Ilikuwa ni huzuni kwa kila mtu, wanafunzi wengi walilia, waliyaona yale aliyokuwa ameyapitia, ilikuwa ni picha yenye kuumiza kwamba msichana yule mrembo ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa mtawa mwisho wa siku alikufa kwenye kifo kibaya na kilichokuwa na maumivu kama kile.
Moyo wa Nathalie ukawa na hasira kali, aliumia, alimuomba Mungu, alimlaumu kwa kuruhusu jambo lile. Yeye na wenzake wakaanza kukaa kwa hofu huku wakimuomba Mungu katika miaka yote mitatu ambayo walitakiwa kukaa mahali hapo na kusoma basi awasaidie wasipate mimba na kuwatokea yale yaliyomtokea Magdalena.
Kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma ndivyo ilivyokuwa ikiendelea, bado waliendelea kutumikishwa kingono kila wikiendi huku wakipigwa video za picha zilizokuwa zikionyesha kila kitu kilichokuwa kikifanyika.
“Ni lazima nifanye kitu nipate hizi picha,” alisema Nathalie.
Hicho ndicho alichokuwa akikihitaji, alijua kabisa kwamba picha zile walizokuwa wakipigwa zilihifadhiwa, hawakujua lengo lakini ilikuwa ni lazima afanye kila liwezekanalo kuhakikisha anazipata picha hizo.
Kwa kuwa alikuwa msichana mjanja na mrembo, kwa yule mwanaume aliyekuwa akifanya naye mara kwa mara akajifanya kumzoea huku akimuonyesha mapenzi matamu kana kwamba alikuwa mume wake wa ndoa.
Alimfanya kujisikia raha, huru na muda mwingi alimwambia kwamba kwa kuwa walizoeana basi ingekuwa vizuri zaidi kama wangekuwa wanafanya kwa uhuru kama mke na mume.
Hilo likamfanya bilionea huyo kumwamini Nathalie na kila alipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumuuliza msichana huyo, alimchukua na kuelekea naye chumbani.
Wanaume walikuwa wakibadilishana lakini kwa mzee Kurtson ilikuwa ni tofauti kabisa, yeye alimuhitaji mtu wake ambaye aliamini kwamba aliletwa katika dunia hii kwa ajili ya kuwa naye tu.
Kipindi cha kwanza hakuwa mzoefu sana lakini kwa kuwa mara nyingi alikuwa akifanya mchezo huo, akapata uzoefu, akajua kuzilegeza nyonga zake, akajua kuutumia mdomo yake kikamilifu kitu kilichomchanganya mzee huyo.
Alichowaambia watu wake ni kwamba walitakiwa kuwa wapole kwa Nathalie kwani ndiye alikuwa msichana aliyebadilisha maisha yake na kumuonyeshea ni kwa jinsi gani mapenzi yalitakiwa kufanywa.
“Hii nyumba yangu ni nyumba yako pia,” alisema mzee Kurtson huku akimwangalia Nathalie aliyekuwa pembeni yake akimchezea kifua chake.
“Kweli bebi?”
“Ndiyo! Yaani wewe jisikie huru kabisa,” alisema.
“Na hao wanaume wengine kwenye vyumba vingine?” aliuliza.
“Hao huwa wanakuja kulala na kuondoka, ila mwenye nyumba ni mimi,” alitamba mzee huyo.
“Nashukuru kulifahamu hilo bebi!” alisema Nathalie, hapohapo akamnyonya mdomo na kuanza kubadilishana mate.
Hayo yote alikuwa akiyafanya kwa kulazimishwa, alihitaji kuzipata picha zilizokuwa zikipigwa, hakujua ni kwa jinsi gani angezipata lakini aliamini kwa sababu alianza kuzoeana na mwanaume huyo basi ingekuwa rahisi kwake kuzipata picha zote.
“Ila nataka ufanye kitu kimoja!” alisema Nathalie kwa sauti nyembamba.
“Chochote utakacho!”
“Nikiwaga chuo huwa ninakukumbuka sana, hivi huwezi kuniruhusu hata siku za masomo niletwe peke yangu bebi nije kulala na wewe mpaka asubuhi?” aliuliza.
“Hilo si tatizo! Ngoja nizungumze na viongozi wako,” alisema.
“Au wewe hutaki?”
“Nataka sana bebi! Yaani nilitamani mno kitu hicho kitokee,” alisema mzee huyo.
Siku hiyo hiyo akazungumza na viongozi wa chuo hicho cha watawa na kuwaambia kuhusu kile alichoambiwa na Nathalie, hilo halikuwa tatizo kwa sababu aliahidi kutoa malipo makubwa zaidi.
Wakakubaliana naye hivyo Nathalie kuchukuliwa siku za kawaida peke yake na kupelekwa huko. Hakukuwa na mtu aliyejua kilichokuwa kikiendelea, kwenye hilo, hakutaka kuwaambia hata marafiki zake, alihitaji kulifanya hilo yeye peke yake.
Kila alipokuwa akiingia katika nyumba hiyo, ndani alikuwa yeye na mzee huyo, wafanyakazi wawili na walinzi ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kulinda nyumba hiyo.
Kila kona kulikuwa na kamera, alihitaji kuzipata picha zilizokuwa zikipigwa kwa kamera hizo na ndiyo maana aliona ili kuzipata kwa urahisi ilikuwa ni lazima aende huko na kujifanya kama alikuwa akihitaji kuwekwa ndani kabisa.
Kila alipofika kitu cha kwanza kilikuwa ni kwenda jikoni na kupika chakula, alikuwa akifanya kila kitu kana kwamba alikuwa ameolewa.
Mzee Kurtson ambaye alikuwa kazini, kila aliporudi alikuta kila kitu kikiwa tayari na hivyo kufikia kula na baada ya hapo ilikuwa ni kwenda kuzikonga nyoyo zao kitandani.
Hilo liliendelea kwa mwezi mzima, kazi yake ilikuwa kila Jumamosi, Jumanne na Alhamisi ni kwenda kwa mzee huyo kumbe kazi kubwa ilikuwa ni kuhangaika kuzipata picha zile.
Huko, akazoeana na kijana aliyeitwa Armando ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kushughulika na mambo yote ya zile kamera na kuzihifadhi picha zilizokuwa zikipigwa kila siku.
Alipogundua hilo, hakutaka kuchelewa, akaanza kuweka urafiki naye kwa karibu. Kijana huyo aliogopa, alijua kabisa kwamba mzee Kurtson alikuwa mtu hatari kama tu angegundua kwamba alikuwa karibu na msichana huyo.
Alijaribu kumkwepa lakini Nathalie hakukwepeka, kila alipofanya hili na lile, msichana huyo alikuwa karibu naye.
“Armando...” alimuita Nathalie kwa sauti ndogo.
“Nini?”
“Ninakupenda sana mpenzi!” alimwambia.
“Unanipenda mimi? Naogopa, bosi atajua!” alisema.
“Kwani utamwambia?”
“Hapana!”
“Sasa atajuaje?” aliuliza Nathalie.
Hakujibu swali hilo kwani alishtukia kinywa cha Nathalie kilikwenda kinywani mwake na kuanza kubadilishana mate huku akianza kuchezewa sehemu ya zipu.
Kijana huyo akachanganyikiwa, Nathalie alijua jinsi ya kumdatisha mwanaume, alimfanyia matendo ya hatari ambayo yalimfanya kijana huyo kulalamika kimahaba kupita kawaida.
Siku ya kwanza walifanya kwa siri, walipomaliza, akavaa nguo zake na kuelekea kitandani kwa mzee Kurtson na kulala hapo mpaka mzee huyo aliporudi na kupokelewa kwa mahaba tele.
Huo ndiyo ulikuwa mchezo wao, muda wote Nathalie alikuwa makini kutaka kugundua mahali memori kadi zilipokuwa zikikaa, alipogundua tu, kazi ikawa kwake kumpagawisha mwanaume huyo mpaka apate nafasi ya kuichukua.
Hilo halikuwa jambo gumu kama alivyofikiria kwani ilimchukua wiki moja tu, akafanikiwa kuichukua na kuiweka kwenye kitambaa cha nywele zake na kuifunga vilivyo kisha kurudi chumbani huku akiziacha kamera zile zikiwa hazina memori kadi ambayo ilikuwa ikitumika kurekodi kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Aliporudi chuo siku hiyo akawaita marafiki zake na kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimeendelea kwamba alifanya kila liwezekanalo kuhakikisha akipata memori kadi na alifanikiwa hivyo baada ya kuondoka hapo Sweden, kazi ilikuwa ni kwenda kuziprinti na kumtafuta mwanaume ambaye angewasaidia kuzipeleka picha hizo makao makuu.
***
“Memori kadi ipo wapi?”
“Nimeihifadhi ndani, ina picha na video zote.”
“Kweli?”
“Ndiyo!” alijibu Nathalie kitu kilichomfanya kila mtu kuwa na furaha.
Japokuwa alipata alichokuwa akikihitaji lakini hakutaka kuacha kwenda nyumbani kwa mzee Kurtson, ilikuwa ni lazima afanye hivyo kwa sababu alihisi kwamba kama angekatisha kwenda basi inawezekana angegunduliwa kila alichokuwa amekifanya.
Aliendelea kwenda huko huku akimuomba Mungu asipate mimba kwani alijua kabisa kwamba kama kitu hicho kingetokea basi ilikuwa ni lazima na yeye auawe kama alivyokuwa kwa Magdalena.
“Mungu nisaidie katika hili,” alisema huku akiwa ameishika rozali yake.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumatano hapahapa
 
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU
0718069269.

Sehemu ya Tatu.

Wasichana hao watatu walifanyiwa mambo ya kinyama, hawakuwa na mahali pa kusemea kwa kuwa waliogopa kuuawa kama walivyouawa wengine, ilikuwa ni lazima watafute mtu ambaye angeyapeleka malalamiko yao katika uongozi wa Kanisa la Living Christ lililokuwa maarufu duniani na kuzungumza kile walichokuwa wakifanyiwa huko chuoni.
Hawakujua ni nani ambaye alistahili kuambiwa maneno hayo na kumpa picha hizo kwa sababu kila mtu ambaye walijaribu kufanya mawasiliano naye, aliuawa hata kabla hajawafikia na kuwapa picha zile za kuzipeleka makao makuu yaliyokuwa nchini Ubelgiji kwa ajili ya maaskofu hao kuchukuliwa hatua.
Baada ya kuziangalia picha zile, Gabriel akarudi kwenye kompyuta yake na kuendelea kusikiliza, alijua mahali picha za wasichana wawili zilipokuwa lakini hakujua mahali picha nyingine za Anna alipozificha na ilikuwa ni lazima kujua mahali zilipokuwa ili siku ambayo angezihitaji basi angekwenda kuzichukua.
Wakati akiwa hapo tayari kwa kuwasikiliza, alisikia kelele za treni na kugundua kwamba walimaliza kuzungumza na hivyo kila mtu kutawanyika.
Gabriel alibaki chumbani kwake akilia kwa maumivu makali, hakuamini kama kile kilichokuwa kimetokea, watu ambao walikuwa wakiaminika, waliokuwa wakiendesha ibada kila siku ndiyo ambao waliwafanyia wasichana hao matendo ya ngono kwa kuwachukua na kuwapeleka katika makasri ya matajiri na kuwafanyisha ngono.
Hilo lilimuuma kupita kawaida na kujiapiza kwamba ni lazima dunia ijue kile kilichotokea, ni lazima picha hizo zifikishwe makao makuu ya kanisa hilo na kuwaonyeshea uovu uliokuwa ukifanywa na maaskofu ambao kila Jumapili walikuwa wakisimama mbele ya kanisa na kuwaambia watu kwamba waache uovu.
“Ni lazima nitapeleka ushahidi wa picha zote, hata kama itatokea nitauawa, basi niuawe nikiwa nimekwishafika nchini Ubelgiji,” alisema Gabriel huku akijiapiza kwamba ni lazima afanye jambo kuwaokoa wasichana wengine waliokuwa wakienda kusomea utawa katika vyuo vya kanisa hilo.
***
Kanisa la Living Christ lilikuwa miongoni mwa madhehebu makubwa kabisa duniani ambalo lilikuwa na wafuasi zaidi ya milioni mia mbili na themanini duniani kote.
Mbali na dhehebu la Kiroma ambalo lilikuwa na wafuasi wengi duniani, kanisa hilo lilikuwa likishika nafasi ya pili kwa kuwa na watu wengi duniani nyuma ya Waroma.
Kila nchi makanisa makubwa yalijengwa huku yakiongozwa na watu waliokuwa na vyeo vya maaskofu, tofauti na Waroma ambao waliongozwa na mapadri.
Living Christ nao walikuwa na watawa ambao walitakiwa kusomea masomo maalumu kwa ajili ya kulitumikia kanisa hilo maisha yao yote.
Kila msichana ambaye alitakiwa kujiunga na kozi ya utawa, sharti la kwanza kabisa lilikuwa ni kuchunguzwa kama alikuwa bikira.
Hiyo ilikuwa ni kazi maalumu iliyofanywa na askofu mmoja aliyeitwa kwa jina la David Ishmael ambaye yeye ndiye alikuwa akithibitisha kwamba huyu alitakiwa kwenda au kuachwa.
Askofu huyo alikuwa nchini Ubelgiji yalipokuwa makao makuu ya kanisa hilo. Kila siku alikuwa akipokea wasichana wadogo ambao walikuwa na ndoto za kuwa watawa ili wamtumikie Mungu maisha yao yote.
Kila aliyekuwa akiingia ndani ya ofisi yake na kutaka kujiunga na chuo cha kanisa hilo ilikuwa ni lazima amwangalie kama alikuwa bikira au la, na kama alikuwa na sifa ya kuwa bikira, ilikuwa ni lazima aitoe, msichana ambaye angekataa basi asingeweza kujiunga na chuo hicho.
Msichana Natalie alifika hapo, ndani ya chumba hicho akiwa na furaha tele. Alisafiri kutoka nchini Marekani kwa ajili ya kwenda kuchukua masomo ya utawa na kumtumikia Mungu maisha yake yote.
Alijitunza, hakumruhusu mwanaume yeyote yule auguse mwili wake, alimuwekea ahadi Mungu wake kwamba katika maisha yake yote angekuwa bikira na ndiyo maana aliamua kuwa mtawa huku akiacha kufanya mambo mengine maovu.
“Hii imekuwa ndoto yangu kwa kipindi kirefu, hakika ninakwenda kuitimiza, nitamtumikia Mungu maisha yangu yote,” alisema Natalie huku akiwa katika viti nje ya ofisi ya Askofu David akisubiri kuingia ndani..
Baada ya dakika chache zamu yake ambaye ndiye alikuwa mtu wa mwisho akaingia ndani ya ofisi ya Askofu David na kuanza kufanyiwa usaili.
Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya mwisho, askofu huyo ndiye alikuwa mtu wa mwisho kudhihirisha kwamba msichana fulani alikuwa bikira au la.
Kwenye nafasi hiyo hawakutaka kumuweka mwanamke, kwenye dhehebu lao hawakuwaamini wanawake, walitaka kila kitu kifanywe na mwanaume na ndiyo maana hakukuwa na askofu wa kike kwa kuwa tu hata enzi za Mfalme Daudi hakukuwa na mwanamke yeyote aliyepewa madaraka ndani ya kanisa.
“Unaitwa nani?” aliuliza Askofu David huku akimwangalia Natalie aliyeonekana kuwa na furaha ya ajabu.
“Natalie Andrew.”
“Unahisi una vigezo vya kuwa mtawa katika kanisa letu?” aliuliza Askofu David huku tayari tamaa ya mwili ikiwa imeanza kumkamata.
“Ndiyo baba askofu!” alijibu msichana huyo, Askofu David akaangalia mitihani aliyoifanya, alifaulu vizuri ila alitaka kuhakikisha kitu kimoja tu, kama alikuwa bikira au la.
“Hebu panda hapo juu ya meza, vua nguo zako,” alisema Askofu David maneno yaliyoonekana kumshtua Natalie.
“Unasema?”
“Nataka nione kama wewe ni bikira kweli,” alisema askofu huyo.
Natalia akawa na moyo mzito kufanya kile alichoambiwa, maishani mwake mwote alijiapiza asingefanya mapenzi na mwanaume yeyote yule, na si hivyo tu bali hata kuuona utupu wake.
Kulikuwa na wanaume wengi waliomfuata kwa ahadi mbalimbali lakini aliwakatalia, kitendo cha askofu kumwambia apande juu ya meza na kuvua nguo zake ili ahakikishe kama alikuwa bikira ulikuwa mtihani mzito mno.
Huku akiwa anafikiria ni kitu gani alitakiwa kufanya, akamuona askofu huyo akianza kuvua nguo zake na kubaki mtupu kama alivyozaliwa.
“Panda juu ya meza nikuchunguze,” alisema askofu huyo huku akichezea sehemu zake za siri.
Natalie alibaki akishangaa, hakuamini kile alichokuwa akikiangalia, hakuamini kama ile ndiyo staili ambayo Askofu David alikuwa akiifanya ili kuona kama mtu fulani alikuwa bikira au la.
Alitamani kutimiza ndoto aliyokuwanayo tangu utotoni lakini kile alichotaka kufanyiwa kilionekana kuwa kama unyama fulani.
“Hii ndiyo nafasi yako ya mwisho! Kama ni bikira, basi umepita, ila kama si bikira, utarudi kwenu, na kama utakwenda kumuhadithia mtu yeyote kile kilichotokea humu, kanisa litatumia nguvu zake kukumaliza kama lilivyowamaliza wengine,” alisema askofu huyo maneno yaliyomtisha msichana huyo.
Hakuwa na la kufanya, hakukubali kuona akikosa nafsi ya kuwa mtawa, kitu ambacho alikitamani tangu alipokuwa mdogo.
Yeye mwenyewe akapanda juu ya meza, macho yake yakaanza kuwa mekundu, akawa analia lakini askofu David hakutaka kujali, akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine mpaka kumuacha mtupu kabisa.
Natalie hakuamini kama bikira yake alikuwa akienda kuipoteza ndani ya ofisi hiyo, kila alipomwangalia askofu David ambaye alikuwa mzee sawa na umri wa baba yake alibaki akilia tu.
Mwanaume huyo akamlalia kwa juu na kuanza kumbaka juu ya meza hiyo. Alisikia maumivu makali chini ya kitovu, damu zikaanza kumtoka mfululizo, alilia lakini askofu huyo hakutaka kujali, ndiyo kwanza alikuwa akienda juu na chini kuhakikisha bikira ya Natalie inatoka ndani ya ofisi hiyo.
Hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kuumiza maishani mwake kuliko siku nyingine. Alilia sana lakini askofu huyo hakujali, alifanya naye kwa dakika kumi ndipo akamwambia kwamba amepita, ni kweli alikuwa bikira hivyo angepelekwa nchini Sweden kwenda kusoma.
Hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake aliyokuwa akiifanya miaka yote, hakukuwa na kiongozi wa kanisa aliyejua, ilikuwa ni siri ya wasichana waliokuwa wakifanyiwa usaili mahali hapo, mbaya zaidi hapakuwa na yeyote aliyediriki kusema kilichokuwa kikitokea huko kwa kuogopa kufukuzwa.
Siku hiyo alikaa na kulia sana, hakuwa peke yake, kulikuwa na wasichana wengine wawili, Anna na Mary ambao nao walifanyiwa vilevile kama alivyofanyiwa yeye na wote walikuwa wakilia tu.
Walibembelezana na siku iliyofuata wakaondoka na kuelekea chuoni huko Sweden ambapo huko wakaanza masomo yao katika chuo cha kanisa hilo.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa na furaha tena, si wao tu bali hata wasichana wengine waliokuwa chuoni hapo walionekana kuwa kama wao.
Walijua kabisa kwamba na hao pia walifanyia mambo ya kinyama kama walivyofanyiwa wao. Walisoma huku kila mmoja akiahidi kwamba kitendo cha kufanya mapenzi na Askofu David angekuwa mtu wa mwisho na wasingeweza kufanya tena mpaka siku watakazoingia kaburini.
Wakati wakiendelea na masomo chuoni hapo huku kila siku wakisali na kumuabudu Mungu, wakaanza kuona mambo yasiyokuwa ya kawaida yakiendelea chuoni hapo.
Kila siku ya Jumapili wasichana watatu walikuwa wakichukuliwa na kuondoka kuelekea nje ya chuo hicho na kurudi usiku wa manane. Kila walipouliza, waliambiwa walipelekwa katika ibada maalumu na viongozi wengine kwa ajili ya kuyaombea mataifa yaliyokuwa na vita.
Hilo likawatia hofu, hawakuamini kama kile walichoambiwa ndicho kilikuwa ukweli. Walikaa chuoni hapo kwa hofu kubwa mpaka wakati mwingine wakajutia ndoto zao za kutamani kuwa watawa kama walivyokuwa.
Baada ya miezi mitatu, wakaambiwa nao walihitajika na kiongozi wa chuo hicho kwani kulikuwa na jambo muhimu walilotakiwa kuambiwa.
Kwanza wakashtuka, mara nyingi watu waliokuwa wakiitwa katika ofisi ya mkuu wa chuo ilikuwa ni kwa wale wasichana waliotakiwa kwenda kuhubiri neno la Mungu nje ya chuo hicho kama walivyofanya wale wengine.
“Kuna nini?” aliuliza Natalie huku akionekana kuwa na hofu.
“Mh! Sijui! Ila ninachohisi na sisi tunatakiwa kutoka usiku kwenda kufanya maombi na viongozi,” alisema Anna huku akionekana kuwa na hofu.
“Kutoka nje ya chuo?”
“Ndiyo! Nimesikia hivyo! Mungu wangu, hivi kwa nini nilitaka kuwa mtawa?” alisema Anna huku akianza kulia huku akiilaani siku ambayo alipata ndoto ya kuwa mtawa.
“Hebu twendeni, labda kuna jingine,” alisema Mary.
Wakaanza kwenda huko.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumatatu hapahapa bila kukosa
Hii kama umeirudia madame
 
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU.
0718069269

Sehemu ya Tano.

Miezi ilizidi kusonga mbele, miaka ikakatika na baada ya miaka mitatu, watatu hao na wanafunzi wengine wakamaliza chuo na hivyo kutakiwa kuondoka kurudi nchini mwao ambapo waliunganishwa na makanisa ya huko kwa ajili ya kwenda kumtumikia Mungu.
Tiketi za ndege zikakatwa lakini kabla ya kuondoka, wanafunzi wote wakaitwa kwenye chumba maalumu na kuanza kupewa maneno ya mwisho juu ya kila kitu kilichotokea.
Kubwa zaidi ilikuwa ni kutunza siri, hayo yalikuwa ni maagizo ya kanisa hilo na kila mtu ambaye alionekana kuwa mtawa kwenye kanisa hilo, alipita kulekule walipokuwa wamepita hivyo hakukutakiwa kwa mtu yeyote kwenda kusema siri hiyo sehemu yoyote ile kwa usalama wa kanisa.
“Kama tutakugundua, tutakuua kama tulivyowaua wengine ambao walifanya kinyume na kile tulichowaambia,” alisema mkuu wa chuo hicho aliyeitwa Askofu Andrew Markov.
Baada ya kuambiwa maneno mengi ya vitisho, wakaletewa simu na kuambiwa wazichukue kwa ajili ya mawasiliano mara baada ya kuondoka katika chuo hicho.
Waliambiwa kwa kawaida chuo hicho kiliingia ubia na kampuni ya kutengeneza simu za Mercury ya nchini Ujerumani kwa ajili ya kuwawezesha watu wao kuwasiliana na hata kutumia internet kwa kasi kubwa.
Wakapewa simu hizo, zilikuwa nzuri, walizipenda na siku iliyofuata wakaingia ndani ya ndege na kuondoka.
Nathalie alikuwa akielekea nchini Marekani huku Mary na Anna wakielekea nchini Canada. Katika kipindi cha nyuma walichokuwa wakienda nchini Sweden kwa ajili ya kukamilisha ndoto zao za kuwa watawa, walikuwa na furaha tele, waliona kabisa maisha yao yalikuwa yakienda kubadilika lakini kile walichokutana nacho huko kiliwafanya kulia mno kiasi kwamba hata safari hiyo ilionekana kuwa mbaya kwa maisha yao.
Ndege ilichukua saa kadhaa, ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Toronto Pearson uliokuwa katika Jiji la Toronto ambapo wawili hao wakateremka na kumuacha Nathalie akielekea nyumbani kwao nchini Marekani.
Ndege ilichukua saa kadhaa ikafika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JKF ambapo akateremka na kukutana na kaka yake, Gabriel aliyeonekana kushtushwa na hali aliyokuwanayo kwani hakuwa na furaha kama alivyoondoka, pamoja na kukamilisha ndoto yake ya kuwa mtawa lakini alionekana kuwa na maumivu makali mno.
Gabriel hakumuuliza kitu, wakaingia, wakaondoka mahali hapo. Njiani walikuwa kimya, Nathalie alikuwa na mawazo tele, kile kilichokuwa kimetokea nchini Sweden kilimuumiza kupita kawaida.
Baada ya dakika kadhaa wakafika nyumbani ambapo Gabriel akateremka, akafungua buti la gari na kutoa begi na mizigo mingine ya ndugu yake na kisha kuelekea ndani.
Siku nzima hiyo ilikuwa ni ya mateso kwa Nathalie, alibaki akilia, kumbukumbu ya kile kilichokuwa kimetokea nchini Sweden kilimuumiza mno. Alilia sana lakini hakuweza kubadilisha kitu chochote kile.
Alikuwa na memori kadi yake, baada ya siku mbili akawapigia simu wenzake na kuwaambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane nchini Marekani kwa ajili ya kuzungumza ili wajue ni kitu gani kilitakiwa kufanyika na nani ambaye walitakiwa kumwamini kipindi hicho.
“Kuna mtu anaitwa Zion, anaishi nchini Ujerumani, nimezoeana naye, nadhani huyo ni mtu sahihi sana kama tutakutana naye na kuzungumza,” alisema Anna.
“Unahisi ataweza kuzifikisha hizi picha makao makuu ili kuwaokoa wasichana wengine ambao watakwenda kusomea utawa?”
“Nadhani! Nina uhakika ataweza kusaidia,” alisema Anna, wakati huo walikuwa wameunganisha simu kwa watu watatu na hivyo kulijadili suala hilo.
Nathalie akawaambia kwamba ilikuwa ni lazima kuhakikisha kila mmoja anakuwa na picha hizo kama ushahidi ambao ungetumika katika kanisa hilo na hata mahakamani ili watu wote watiwe nguvuni na kuhukumiwa kwa kile walichokuwa wamewafanyia.
“Haina shida.”
“Ila kwanza tuonane,” alisema Nathalie.
Wakaonana nchini Marekani na kuanza kulizungumzia suala hilo, ilikuwa ni lazima wajadili kwa pamoja na kujua ni kitu gani ambacho walitakiwa kufanya ili kuhakikisha watu wote waliokuwa wamehusika katika mchezo huo wanafungwa gerezani na hata washirika wengine wa kanisa hilo waachane nalo kwani halikuwa kanisa la kumtumikia Mungu kama walivyokuwa wakiaminishwa.
“Basi wasiliana naye!”
“Haina shida! Hilo ondoeni shaka. Natumaini tutarekebisha, atakuja hapa na tutampa hizi picha,” alisema Anna. Picha zile zikaprintiwa na kila mtu kukabidhiwa zake na kuondoka.
***
Viongozi wa kanisa la Living Christ walikuwa makini kwa kila kitu, hawakutaka kumwamini mtu yeyote yule, waliwajua wanawake, walikuwa watu wenye mioyo mepesi ambao hawakuwa na uwezo wa kutunza siri kwa kipindi kirefu na ndiyo maana hata walipokuwa wakiondoka mahali hapo ilikuwa ni lazima kuwafuatilia.
Ufuatiliaji wao ulikuwa ni wa kisasa kabisa, hawakutaka kutuma mtu bali kwa zile simu ambazo waliwakabidhi siku ya mwisho kabla ya kuondoka chuoni hapo ndizo ambazo zilikuwa zikitumika kunasa mawasiliano yao.
Ilikuwa ni kazi nyepesi kujua walikuwa wakiwasiliana na nani, hakukuwa na ugumu wa kufahamu ni mahali gani watu hao walipokuwa.
Walifuatilia kila kitu na hata wasichana hao watatu walipokuwa wakiongea na kupanga mipango yao, waliwafuatilia kwa karibu kabisa.
Waligundua kwamba walifanya mpango wa kuonana nchini Marekani, mbali na kifaa cha GPS walichokuwa wameweka ndani ya kila simu pia kulikuwa na kimaiki kidogo ambacho kilinasa mazungumzo, kiliyarekodi na kuyatuma kule chuoni ambapo viongozi walikuwa wakiyasikia.
Waliposikia kwamba wasichana hao walikuwa na picha juu ya kilichokuwa kimetokea huko Sweden, walichanganyikiwa, hawakulitegemea hilo kwani waliamini kwamba kila kitu kilikuwa siri kubwa na hakukuwa na mtu yeyote ambaye aliruhusiwa kwenda na simu, sasa ilikuwaje mpaka watu hao wapate picha hizo?
Wakajua kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea, haraka sana wakafuatilia maisha ya wasichana hao chuoni hapo, wakagundua Nathalie ndiye aliyekuwa na nafasi ya kwenda nje ya chuo hicho kuonana na bilionea Kurtson na inawezekana kabisa mtu huyo ndiye aliyeruhusu picha za kila kitu kilichokuwa kimetokea kuibwa.
Haraka sana wakampigia simu na kuanza kuzungumza naye, waliongea kwa hasira, kwao waliona kama walikuwa wakigeukiwa kwani hawakutegemea kama kungetokea kitu kama hicho.
Mzee huyo alipoambiwa kuhusu picha hizo, akashtuka, hakutegemea kuambiwa kitu kama hicho na hivyo kuuliza zaidi huku akitaka kupewa ufafanuzi kwamba ni kwa namna gani msichana Nathalie alichukua picha hizo na wakati zilikuwa zikirekodiwa na kamera za CCTV.
“Hatujui! Kwanza kuna memori kadi?” aliuliza kiongozi mmoja.
“Ndiyo!”
“Ndiyo umekwenda kuangalia au?”
“Subiri!”
Mzee huyo akaondoka na kwenda kwenye chumba cha kuhifadhia video na picha ambapo akamkuta kijana wake Armando akiendelea kufanya kazi yake.
Kitu cha kwanza kabisa ni kumuuliza kuhusu memori kadi. Kijana huyo hakuwa na hofu, alichojua ni kwamba memori kadi ilikuwepo na ilikuwa ikirekodi kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Akakifuata kifaa ambacho kilikuwa kikihusika na kutunza kumbukumbu kutoka kwenye memori kadi, alipokifungua na kuangalia ndani, memori kadi haikuwepo.
Alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, alichokijua ni kwamba kila siku memori kadi hiyo ilikuwa humo, sasa iweje isionekane? Iweje leo ionekane kwamba hakukuwa na kitu chochote kilichokuwa kikirekodiwa?
“Vipi?” aliuliza mzee Kurtson.
“Memori kadi haipo,” alijibu Armando.
Mzee huyo alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kuwaambia wanaume hao ambao nao walionekana kama kuchanganyikiwa kama yeye. Kabla ya kuwapigia simu kwanza akakaa chumbani kwake, hakujua ni kitu gani alitakiwa kuwaambia.
Kama kweli aliruhusu mpaka memori kadi ile kuchukuliwa, inamaana huo ndiyo ungekuwa mwisho wa yeye kupelekewa wasichana kwa kuwa tu iligundulika hakuwa makini na kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Alikaa kwenye hali hiyo kwa dakika kadhaa, akachukua simu yake na kuwapigia kisha kuwaambia kilichotokea. Kwanza akakaripiwa kama mtoto mdogo lakini uamuzi wa mwisho uliotolewa ni kwamba hakutakiwa kupelekewa wasichana kama ilivyokuwa.
“Nahitaji mnisamehe! Nitaishi vipi bila kuwapata wasichana hao?” aliuliza mzee huyo, alikuwa akilia kama mtoto, kufanya mapenzi na wasichana wadogo ndiyo ilikuwa tabia yake, alizoea tangu alipokuwa na miaka ishirini, mpaka miaka hiyo ya hamsini na tano, starehe yake ilikuwa ni kufanya mapenzi na wasichana wabichi.
Viongozi hao walikuwa wakijadili ni kitu gani kilitakiwa kufanywa ilimradi wawanyamazishe wasichana hao kwa nguvu kubwa.
Hawakujali kuhusu pesa, kitu pekee walichokihitaji ni kuona ile siri waliyokuwanayo inaendelea kufichwa kwa nguvu kubwa.
Wakati wakiendelea kuwafuatilia ndipo wakagundua kwamba walitaka kuonana na mwanaume aliyeitwa kwa jina la Zion aliyekuwa nchini Ujerumani ambaye ndiye angepewa picha hizo na kuzipeleka makao makuu.
Hawakutaka kukubali, haraka sana wakaanza kumfuatilia mwanaume huyo kupitia namba yake ya simu. Waliweza kumpata na ilionyesha kwamba alikuwa katika Jiji la Berlin, ilikuwa ni lazima kutafutwa hukohuko.
Kwa kupitia namba ileile, wakaangalia usajili wake, nyumba aliyokuwa akiishi, na kipindi hicho Zion alikuwa akisoma katika Chuo Kikuu cha Berlin masomo ya Utabibu.
“Ni lazima auawe haraka sana!” alisema mwanaume mmoja kwenye chumba hicho.
Mawasiliano yakafanyika harakaharaka baina yao na vijana wao waliokuwa nchini Ujerumani na kuwapa kazi moja ya kumuua mwanaume huyo.
Kwa kupitia simu yake wakafanikiwa kupata mpaka picha yake na kuwatumia ambapo baada ya kuipata tu, wakafanikiwa kwenda chuoni, walipomkosa wakaelekea nyumbani kwake.
Huko wakamkuta, wakajitambulisha kwamba walikuwa ni polisi kutoka makao makuu ya polisi hapo Berlin na walifika mahali hapo kwa kuwa walitakiwa kumchukua na kwenda naye kituoni.
“Kuna nini?” aliuliza Zion.
Walimwambia walifuatilia mawasiliano yake kwa njia ya simu na kugundua aliwasiliana na magaidi kutoka katika kundi la kigaidi la Al Qaida lililokuwa na makazi yake huko Mashariki ya Kati.
Zion akashtuka, katika maisha yake hakuwahi kuwasiliana na watu kutoka huko Uarabuni lakini hata kabla hajakubaliana kufuatana na watu hao, akahitaji vitambulisho vyao, wakamuonyeshea, akaridhika na kukubali kuondoka nao.
Njiani, hakuelewa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, alijaribu kuvuta kumbukumbu zake, hakuwahi kufanya mawasiliano na Waarabu, sasa iweje watu hao wamwambie aliwahi kufanya mawasiliano hayo?
Hakujua nyuma ya pazia mpango uliokuwa umefanywa, hakujua kama alitakiwa kuuawa haraka iwezekanavyo.
Alikuwa kimya ndani ya gari, huku wakiwa wamefika katika makutano ya Barabara iliyokuwa ikielekea mjini Koln, akashtukiwa akiguswa na kitu cha baridi ubavuni, alipoangalia, macho yake yakatua kwenye bastola ndogo aina ya Revolver 90.
“Hutakiwi kutingishika, la sivyo utumbo wako utamwagika humuhumu,” alisema mwanaume aliyekaa upande wake wa kushoto, kijasho chembamba kikamtoka, akajua kabisa siku hiyo ndiyo ilikuwa ya mwisho kuvuta pumzi ya dunia hii.

Je nini kitatokea?
Tukutane jumamosi hii.
 
NYEMO CHILONGANI.
SHAMBULIO LA DAMU.
0718069269.

Sehemu ya Sita.

Nathalie na wenzake walikuwa na uhakika kwamba Zion angefika nchini Marekani kuchukua hizo picha na kuzipeleka nchini Ubelgiji katika makao makuu ya Kanisa la Living Christ.
Kwa muda huo hawakutaka kumwamini mtu yeyote zaidi ya mwanaume huyo, si kwa njia ya barua pepe na wala DHL, kwa zile picha walizokuwanazo zilibeba siri kubwa mno ambayo haikutakiwa kugundulika na mtu yeyote zaidi ya viongozi wa juu wa kanisa hilo.
Walichokifanya ni kumsubiri, Zion aliwaambia ndani ya siku mbili angekuwa nchini Marekani lakini kitu cha ajabu kabisa, baada ya siku ya pili kuingia tu hakuwa akipatikana kwenye simu, na mbaya zaidi hakuwa amekwenda nchini Marekani.
Hilo liliwashangaza mno, hawakujua ni kitu gani kilitokea, walichokitegemea ni kwamba mwanaume huyo angefika huko lakini cha ajabu kabisa hakutokea jambo ambalo wakati mwingine liliwafanya kuhisi alitaka kuwauza.
Waliumia mioyoni mwao, Zion akawaonyeshea kwamba hawakutakiwa kumwamini mtu mwingine yeyote hivyo kama kweli walihitaji kuzipeleka picha hizo huko makao makuu, walitakiwa kwenda wao na si kumwambia mtu mwingine.
“Nani aende?” aliuliza Nathalie.
“Nitakwenda mimi!” alijibu Anna huku akiwaangalia wenzake.
“Una uhakika utafika salama?”
“Kwa hilo msijali!” alisema msichana huyo huku akionekana kujiamini kupita kawaida.
Haukuwa uamuzi mbaya, waliona kabisa kwamba kama kweli Anna alitaka kuzipeleka picha hakukuwa na tatizo lolote lile hivyo wakakubaliana naye kuelekea huko.
Siku iliyofuata, Anna akajiandaa tayari kwa kuanza safari hiyo. Saa mbili kabla ya kuanza safari hiyo, waliwasiliana na mkuu wa kanisa hilo, Askofu Richard Poff aliyekuwa nchini Ubelgiji na kuzungumza naye kwa dakika kadhaa huku wakimwambia kulikuwa na kitu cha siri sana na kama wasingechukua hatua kama kanisa basi wangeweza kuliona likianguka kutokana na aibu ambayo ingelikumbuka.
Askofu Poff alishtuka, hakuamini kusikia maneno kama hayo, hakujua ni kitu gani kilizungumziwa, hakujua kulikuwa na nini ambacho wasichana hao walikuwanacho hivyo kukubaliana nao kwamba mmoja aende nchini Ubelgiji na kumpa kitu hicho.
Baada ya muda wa safari kufika huku akiwa na tiketi yake ya Shirika la Ndege la American Airlines, Anna akaagana na wenzake na kuingia kwenye ndege huku akiwa na begi lake ambalo kwa ndani kulikuwa na picha hizo.
Ndani ya ndege hakuzungumza na mtu yeyote yule, alikuwa kimya kabisa, aliogopa, alihisi kabisa kwamba kama kungekuwa na mtu ambaye alifahamu kile kilichokuwa kikiendelea ilikuwa ni lazima kumchezea mchezo hivyo kupoteza kila kitu alichokuwanacho.
Kwenye kiti cha watu wawili alichokuwepo alikaa na mwanaume mmoja wa Kizungu kama yeye ambaye kwa kumwangalia tu alionekana kuwa mchangamfu ambaye muda mwingi alitamani kuzungumza na Anna ambaye alivalia vazi la kitawa huku akionekana kuitilia umakini mkubwa safari yake.
Mwanaume huyo hakutulia, pale alipokaa alikuwa akibabaika huku muda mwingi akijaribu kuweka ukaribu na Anna lakini msichana huyo hakumpa nafasi hiyo.
“Where to sister?” (unakwenda wapi mtawa?) alimuuliza huku akimwangalia kwa uso uliokuwa na tabasamu pana.
“Belgium!” (Ubelgiji) alijibu kwa kifupi.
“Ooh! To preach the Word of Living God?” (Ooh! Kulihubiri Neno la Mungu aliye hai?) aliuliza.
“Yes!” (ndiyo)
Majibu yake yalikuwa ni kwa kifupi sana, hakuhitaji kuzoeana na mtu yeyote yule, alihitaji kuwa mkimya huku akiwa peke yake, kwenye safari hiyo ambapo alibeba siri kubwa alitakiwa kuwa makini, hakukutakiwa kuzoeana na mtu yeyote yule kwa kuogopa kufanyiwa mchezo mbaya.
Baada ya ndege kukaa angani kwa saa ishirini na sita ndipo ikaanza kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa Brussels uliokuwa jijini humo nchiniUbelgiji, akateremka na abiria wenzake na kuanza kuelekea kwenye jengo la uwanja huo kwa ajili ya upekuzi kisha kuondoka.
Hakuwa na mizigo mingi zaidi ya hilo begi alilolibeba, moja kwa moja alipoonekana hakuwa na tatizo lolote lile, akaanza kuelekea nje ya uwanja huo mahali kulipokuwa na idadi kubwa ya watu waliokuwa wakiwasubiria wageni wao, hapo akamuona msichana mmoja akiwa ameshika bango lililoandikwa jina lake huku akiwa amevalia vazi la kitawa.
Alipoyakutanisha macho yake na msichana huyo, akaachia tabasamu pana na kuanza kumsogelea. Alipomkaribia, wakasalimiana Kikristo na kisha kumchukua na kuelekea naye ndani ya gari.
“Huyu ni Askofu Martin ambaye tumetumwa kuja kukupokea mtumishi wa Mungu,” alisema msichana huyo aliyejitambilisha kwa jina la Lucy ambaye kwa kumwangalia tu ilikuwa ni rahisi kugundua alikuwa mtumishi wa Mungu mzuri tu.
“Nimefurahi kukufahamu,” alisema Anna huku akimpa mkono Martin.
Watatu hao wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea makao makuu kuanza. Lucy ndiye aliyekuwa akiendesha gari huku pembeni yake akiwemo Martin, walikuwa wakipiga stori za kidini tu, muda wote walizungumza matendo makuu ambayo Mungu aliendelea kuwatendea katika maisha yao kiasi kwamba hata Anna aliamini kwamba watu hao walikuwa upande wake.
Baada ya dakika kadhaa, huku stori zikiwa zimenoga, gari likasimama kwenye mataa, hata kabla hawajafanya kitu chochote kile, wanaume wawili waliokuwa na miili mikubwa wakaingia ndani ya gari hilo kwa nyuma, mmoja aliingilia mlango wa kushoto na mwingine mlango wa kulia.
Anna akashtuka, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea. Huku hata kabla hajauliza swali lolote lile, wanaume hao wakatoa bastola zao na kuzishika huku wakimtaka msichana huyo atulie kwani kama angefanya kitu chochote kile au hata kupiga kelele basi wangeweza kumuua humohumo na kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angejua.
“Tulia hivyohivyo kama unataka kupigwa picha. Ukitingishika tu au hata kupiga kelele, kitakachotokea ni roho yako kuacha mwili,” alisema jamaa aliyekuwa upande wa kulia.
Anna alibaki akitetemeka, kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakujua kilichokuwa kikiendelea. Martin na Lucy ni kama hawakuona vile, bado walikuwa wakiendelea na stori zao za kumsifu Mungu kama kawaida yake kana kwamba walikuwa gari tofauti.
Baada ya dakika moja, mataa yakaruhusu na kuondoka mahali hapo. Anna alibaki akitetemeka, mapigo ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi, hakuwajua watu hao walikuwa akina nani, hakujua walitaka nini mpaka kuingia ndani ya gari hilo.
***
Simu zilipigwa katika vyuo mbalimbali vya utawa vilivyokuwa vikihusika na michezo hiyo ya ajabu. Kila mtu aliyesikia kile kilichokuwa kikiendelea, aliogopa na kuona kama wasingefanya kitu fulani basi ingekuwa hatari zaidi kwao.
Walichokipanga ni kufuatilia mawasiliano ya wasichana hao na hata zile stori walizokuwa wakipiga kuhusu kile kilichoendelea.
Walichokigundua ni kwamba mtu aliyewasiliana naye alikuwa Zion, watu wakatumwa na kwenda kumuua kisha mwili wake kuuchoma moto katika jumba moja la Bilionea Mitchel ambaye naye alikuwa akihusika kununua watawa waliokuwa katika chuo kimoja kilichokuwa huko Berlin.
Kwenye mazungumzo ya wasichana hao ndipo wakagundua mmojawao aliamua kusafiri yeye mwenyewe kwenda nchini Ubelgiji kukabidhi picha zile kwa Askofu Poff kitu.
Msichana huyo alitakiwa kunyamazishwa haraka sana hivyo baada ya kujua ni muda gani alikuwa akisafiri, wakajipanga kumpokea huku wakijifanya kutoka kwa askofu huyo ambaye bado aliendelea kujiuliza maswali mengi kuhusu kile walichokuwanacho wasichana hao ambao walisema ilikuwa ni hatari tupu na kanisa lingekwenda kuchafuka.
Hawakutaka kuona msichana huyo akifika kwa Askofu Poff, ilikuwa ni lazima kumnyamazisha hata kabla ya kusimama mbele ya mwanaume huyo.
Ili kumpata kwa urahisi, aamini kwamba walitumwa na askofu huyo, wakaamua kumtafuta msichana ambaye alitakiwa kuvalia kitawa na kwenda huko ilimradi asimtilie shaka kwa lolote lile.
Walipompata msichana huyo wakamjaza maneno na kumlipa kiasi kizuri cha pesa na kumwambia aende uwanja wa ndege akitangulizana na mwanaume mmoja.
Walipofika, walimpokea Anna na kuondoka naye kuelekea mahali walipoambiwa wampeleke.Waliambiwa kila kitu kwamba mara baada ya kufika katika makutano ya barabara nne, kungekuwa na foleni hivyo hapo dereva alitakiwa kutoa loki za milango na wanaume wawili wangeingia ndani.
Hilo likafanyika na wanaume hao kuingia ndani ya gari hilo na kuanza kuondoka. Safari hiyo iliishia ndani ya jumba moja, Anna akateremshwa na kupelekwa ndani huku akitetemeka kupita kawaida.
Kitu cha kwanza akapokonywa picha alizokuwanazo na kufungiwa ndani ya chumba kimoja na kuanza kupewa adhabu kwa kile alichotaka kukifanya.
Aliteswa sana, alichapwa mijeredi, alipigwa shoti ya umeme na kupewa mateso mengine makali. Aliumia, mwili ulikosa nguvu mpaka kufikia hatua ya kuomba Mungu aichukue roho yake lakini si kuona akiendelea kuteseka kama ilivyokuwa.
“Kill me! I don’t deserve to live, just kill me now,” (niueni! Sistahili kuishi, niueni tu) alisema Anna kwa sauti ya chini ambayo ilikuwa ni rahisi kugundua ni kwa kiasi gani alikuwa akisikia maumivu makali mwilini mwake.
Haraka sana simu ikapigwa mpaka kwa viongozi hao na kuwapa taarifa kwamba msichana huyo alikuwa amepatikana na walikuwa naye.
Viongozi hao walitoa amri moja tu kwamba kama Anna alikuwa mikononi mwao ilikuwa ni lazima wamuue na kuzipeleka picha hizo kwa mmoja wa viongozi wa chuo cha watawa kilichokuwa hapo Ubelgiji kwani naye pia alikuwa akihusika kwa kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Muueni tu! Nyama yake mtawapa mbwa wale, si vizuri wanyama kuwanyima chakula,” alisema kiongozi aliyekuwa upande wa pili.
Hawakutaka kusubiri au kusikia amri nyingine. Mwanaume mmoja akaelekea katika chumba alichokuwa Anna, alipofika humo akachukua bastola yake na kumuwekea kichwani.
“Unakufa! Utamwambia Mungu kwamba umbeya wako ndiyo uliokumaliza,” alisema mwanaume huyo na mlio wa risasi kusikika.
“Paaaaa...”
Risasi hiyo ikatoka na kumpata Anna kichwani mwake, damu zikaruka, ubongo ukafumuka na kuanguka chini huku damu nyingi zikimtoka kichwani. Ulikuwa ni unyama wa aina yake, viogozi hao walikuwa wakifanya kila liwezekanalo kuwazima watu wote ambao walitaka kwenda kupeleka taarifa juu ya kile kilichokuwa kikiendelea katika vyuo mbalimbali vya watawa.
Walipoona Anna amekufa, wakambeba, wakamvua nguo zote na kumpeleka kwenye banda lililokuwa na mbwa zaidi ya watano waliokuwa na njaa kisha kumtupa humo ambapo mbwa hao wakaanza kumgombea na kumla mpaka walipobakiza mifupa tu.

Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom