Hamduni
Senior Member
- Apr 25, 2020
- 155
- 108
NUKUU: BAADHI YA NUKUU ZA KATIBU WA NEC ITIKADI NA UENEZI WA CCM, SHAKA HAMDU SHAKA ALIPOKUA ANAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO 12 OCTOBA 2021 DODOMA
"Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kusimamia na kuimarisha haki za binadamu, usawa, demokrasia, kupinga aina zote za ubaguzi pamoja na kupiga vita ubadhirifu"
"Chama cha Mapinduzi kinakipongeza ACT Wazalendo kwa kushinda katika jimbo la Konde, Wilaya ya Micheweni mkoani Kaskazini Pemba na hiyo ndio siasa safi"
"Kumalizika kwa chaguzi hizi ndogo za udiwani na ubunge majimbo ya Konde na Ushetu kwetu kumetupa funzo kwa wenzetu katika uso wa demokrasia"
"Katika kujenga na kukuza uchumi serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji"
"Chama cha Mapinduzi kinaendelea kuwaomba na kuwahamasisha wananchi wote kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, Rais ambaye ana dhamira njema ya kutaka kutufikisha kule tunakotaka na kudumisha huduma za msingi za jamii ikiwemo afya, maji, elimu"
"Chama cha Mapinduzi kinatoa wito kwa wanachama na kamati za siasa za ngazi zote kuhakikisha kwamba wanafuatilia kwa karibu sana utekelezaji wa mradi wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19 kuhakikisha hakuna fedha zinaliwa"
"Fedha za mradi wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19 sadaka bali zimekuja kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania. Fedha zimekuja kwa ajili ya kuwaletea maendeleo ya Watanzania na kuhakikisha uchumi wa mtu mmoja mmoja unainuka"
"Chama cha Mapinduzi ni chama kikubwa katika mambo ambayo CCM iko nayo makini ni mambo ambayo yanayobeba maslahi mapana ya CCM na ndio sababu inaendelea kusalia madarakani. Kwa yeyote ambaye aliyekwenda kinyume na taratibu, taratibu zake zipo na zitafuatwa"
"Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kusimamia na kuimarisha haki za binadamu, usawa, demokrasia, kupinga aina zote za ubaguzi pamoja na kupiga vita ubadhirifu"
"Chama cha Mapinduzi kinakipongeza ACT Wazalendo kwa kushinda katika jimbo la Konde, Wilaya ya Micheweni mkoani Kaskazini Pemba na hiyo ndio siasa safi"
"Kumalizika kwa chaguzi hizi ndogo za udiwani na ubunge majimbo ya Konde na Ushetu kwetu kumetupa funzo kwa wenzetu katika uso wa demokrasia"
"Katika kujenga na kukuza uchumi serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji"
"Chama cha Mapinduzi kinaendelea kuwaomba na kuwahamasisha wananchi wote kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, Rais ambaye ana dhamira njema ya kutaka kutufikisha kule tunakotaka na kudumisha huduma za msingi za jamii ikiwemo afya, maji, elimu"
"Chama cha Mapinduzi kinatoa wito kwa wanachama na kamati za siasa za ngazi zote kuhakikisha kwamba wanafuatilia kwa karibu sana utekelezaji wa mradi wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19 kuhakikisha hakuna fedha zinaliwa"
"Fedha za mradi wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19 sadaka bali zimekuja kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania. Fedha zimekuja kwa ajili ya kuwaletea maendeleo ya Watanzania na kuhakikisha uchumi wa mtu mmoja mmoja unainuka"
"Chama cha Mapinduzi ni chama kikubwa katika mambo ambayo CCM iko nayo makini ni mambo ambayo yanayobeba maslahi mapana ya CCM na ndio sababu inaendelea kusalia madarakani. Kwa yeyote ambaye aliyekwenda kinyume na taratibu, taratibu zake zipo na zitafuatwa"
"CCM ndio inaunda dola na kupewa dhamana ya uongozi, tumekuwa tukipita na kuangalia miradi na kusema hapa tumeridhika na hapa hatujaridhika na kutaka hatua zichukuliwe, tunafanya hivyo kwa kuwa sisi ndio tumebeba dhamana na maslahi ya serikali"