Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,545
- 2,175
===
Tofauti kabisa na minongo'no na matarajio ya wengi kuwa huenda Mhe Shaka Hamdu Shaka hakufurahishwa kwa kuondolewa kwake kwenye Chama na kuteuliwa kuwa Mkuu Mpya wa Wilaya ya Kilosa akiondolewa kwenye nafasi hiyo ndani ya Chama aliyeihudumu kwa karibu Miaka miwili,
Hatimaye Leo Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bi Fatma Maswa Shaka Hamdu Shaka akiwa ni mwenye bashasha na furaha sana huku akishangiliwa wakati wote amekula kiapo cha Uaminifu na Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt Samia Suluhu Hassan na kwa Viongozi Wengine,
Mtakumbuka Shaka Hamdu Shaka alikuwa ndie Katibu wa Itikadi & Uenezi wa CCM kabla ya aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ndg Sophia Edward Mjema kuchukua mikoba yake,