Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

116621.jpeg
 
Waziri anasema wameanza kufufua hangar kwa kukarabati taa! gereji la ndege huna unasema unalifufua kwa kutengeneza taaaa???? then whats next spana? Tunanunua nini kwanza, bisibisi au namba kumi boxi?

hela ya service hawana, wameomba Ikulu!

wamemuongezea faili lingine kitandani la tool box la gereji ya ndege, masikini ya Mungu watamuua na stress,

ATCL ni dhaifu!
 
Mkataba wa kukodisha ndege za serikali kwa ATCL unasemaje kuhusu matengenezo ya ndege hizo? Kwa nini Serikali igharimie matengenezo hayo kwa fedha zake pasipo kupitishwa na Bunge na badala yake zinaombwa toka kwa Mukulu ambaye tayari kesharidhia hili? Maswali ni mengi kuliko majibu.
 
Ndege zina services schedule zake kila baada ya miaka kadhaa (ni vitu ambavyo avikwepeki) ndio maana unawasikia wakipiga kelele kufufua hangar la Arusha kupunguza hizo gharama za kupeleka ndege Canada.
Kwa ndege mpya sio mwaka 1 bana tunaelewa kila kitu
 
Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.
Mama weee!!!!!!!! Njoo huku usikie hii, eti serikali imeanza kukarabati hanga (banda) la kutengenezea ndege kwa kuweka taa! Siyo jeki na supana.
Hapa habari ilitakiwa iwe ununuzi wa vifaa vya kufanyia matengenezo siyo taa na maji.
 
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la *NIPASHE* la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_

Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano *Mhandidi Isack Kamwele* , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege

Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini

Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani

Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili

Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu

Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service

Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,

Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo

Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_
 
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la *NIPASHE* la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_

Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano *Mhandidi Isack Kamwele* , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege

Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini

Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani

Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili

Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu

Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service

Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,

Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo

Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_

Mkuu acha kutupiga fix,600 flying hours ni sawa sawa na 25 Flying days,kama kwa wastani kwa siku moja inasafiri masaa mawili means itakuwa imesafiri /fanya safari zake kwa siku 50,almost two Months,Hii story yako peleka kwa watoto wa Form two

Sent from my TECNO CX Air using Tapatalk
 
kikubwa ninachowaza mimi ni hizo ndege kwa kipindi chote zimeingiza shilingi ngapi? maana hapo ndo tunaweza anzia kwa leo, naamini watu wa mavyuma watakuwa washanielewa nacholenga
 
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la *NIPASHE* la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_

Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano *Mhandidi Isack Kamwele* , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege

Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini

Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani

Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili

Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu

Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service

Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,

Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo

Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_
kilamtu na taaluma yake hilo gazeti lipo sawa kwa 100% na limefuata taratibu zote za uandishi pia kanunu ni kipi kilichokosewaaa? huo ndio uandishi wa magazeti lazima mwandishi mashuhuri ajue kuliremba kwa kichwa maridhawa ka hicho ulichokisoma
 
Je, tunao 'Aircraft Engineers & Techicians' wa kutosha na wenye weledi kufanya "service & repair' ya hizo ndege pamoja na workshops?

Tunakarabati karakana kwanza hayo mengine yatajipa mbele ya safari. Kwani si tulianza kununua ndege kwanza ndio tukagundua kuna haja ya kuwa na karakana? Hivyo hivyo mdogo mdogo.
 
Zimeshaingiza kiasi gani Kama faida hadi sasa?
Bro cha ajabu hapa nini? Unadhani ndege ni Vitz? Hiyo ni service ya kawaida na wala hakuna cha ajabu. Kama unapanda basi kwenda Moshi unalipa sh 30 elfu mwingine anakwenda Moshi huko huko analipa laki 3 hujawahi kujiuliza why? Nipashe wameandika kwa maana nyingine ya kawaida tu, lakini wewe unataka kuonyesha kama ni kitu cha ajabu saana. Acheni umbeya kwa mbo msiyoyaelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mv Dar Es Salaam tuliambiwa nikivuko kipya baadae ikagundulika ni mkweche, Binafsi siwezi kushanga ccm kikokotoo kutuingiza MKENGE wa midege mibovu ndio maana watumishi wa umma wakikatiwa tiketi ATCL wanapanda mabasi wanaogopa MIDEGE USED mala buti limefunguka lenye angani, ccm mpya ni wapigaji zaidi ya ccm ya zamani usafiri wa ndege sio kama mwendokasi migari ya kichina ya mwendoka likibuma mnashuka na kutembea kwa mguu #2020 Lissu #
 
Wacha urongo!

hela za matumizi ya serikali hazipitishwi na Rais!

Tunataka kujua hii ni service ya kawaida ama ni ukarabati wa ubovu?

Kama ndege ni mbovu hizi ni terrible teens zimeanza ku rear their ugly face on him?

Kama ni ukarabati wa kawaida kwa nini hela inaenda kuombwa nje ya ATCL, haikuwa kwenye business plan?

Na ni kwa nini Waziri Kamwele ndio ana run ATCL badala ya a professionally qualified, full time dedicated, paid and accountable CEO of the company?

TUNATAKA MAJIBU!
hujui kitu, kaa kimya!
 
“Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Hivi sasa kuna ushindani mkubwa kati ya Kampuni ya GE ya Marekani na Kampuni ya Rolls Royce Uingereza kuhusu nani apate biashara ya injini hiyo.
Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei. Bahati mbaya Sana mazungumzo hayo yalimhusisha Rais John Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao. Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya.

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.

Zitto Kabwe
3/5/2017
 
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la *NIPASHE* la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_

Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano *Mhandidi Isack Kamwele* , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege

Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini

Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani

Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili

Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu

Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service

Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,

Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo

Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_
Acha uzembe. Kwanini hawakukarabati hilo hanger kabla ya kukimbilia kuleta hiyo mindege? Ungekuwa mzalendo kweli ungetambua kuwa hizo hela ambazo Waziri kaomba kwa Rais ni zako wewe mlipakodi hohehahe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom