Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.
Swali fikirishi je kununua ndege aina hizo mpya ni bei gani kwa wale wenye kujua watujuze ''A Country is Not a Company''
 
Mkuu barafu tunaomba maoni yako kutokana na uzoefu wako katika masuala ya usafiri wa anga, Je ni kweli hiko kiasi ndio halisi kwa service? Na hiyo service inatakiwa kila baada ya muda gani tangu zianze kazi?
 
Kwa hiyo waache kufanya biashara sababu kuna wajanja wengi? Najua rais amejithid kupunguza hao watu japo bado wapo baadhi sema wamejificha. Maybe wanajarib lakin kidogo kidogo watafika.

Akina ethiopia walianza mbali sana by then. Hawakuanza na ndege 100
Ni ndoto kwa ATC kukua na kuendelea kibiashara hata kama wangemiliki ndege kibao kama Ethiopia airline kwani kuna wajanja wengi ambao bado wanapanga njama za kupiga pesa kisayansi zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndege zina services schedule zake kila baada ya miaka kadhaa (ni vitu ambavyo avikwepeki) ndio maana unawasikia wakipiga kelele kufufua hangar la Arusha kupunguza hizo gharama za kupeleka ndege Canada.
Hasa ndivyo ilivyo. Hata gari ukinunua jipya kabisa unaambiwa ulipeleke service kila mwaka au hata kabla ya mwaka kuisha kama litakuwa limetembea kilomita kadhaa.
 
Kukarabati ndege ni jambo la kawaida. Ila hapa ndipo tutapojifunza kuwa biashara ya ndege ni zaidi ya kununua tu ndege lukuki.

Na ndiyo maana mashirika mengi huwa hata ndege zao ni za kukodisha, eg south africa airways. Kazi ya kampuni ya ndege inatakiwa iwe ku-manage routes zenye faida na kuhakikisha ndege zinakuwa angani zikiwa zimejaa abiria kila wakati. Najua wengi hamtaelewa mpaka muone.
kwa misukule ya Lumumba na yule spika dhaifu hili ni vigumu sana walielewe!
 
Hizo Bombardier tangu zimeanza rasmi kufanya safari, ni muda gani umepita? Na hiyo scheduled service huwa ni kila baada ya muda gani? Dreamliner je itagharimu kiasi gani?

Cc barafu
Pengine ni borazaidi unejibidisha kuelewa manufacturer's technical recommendation kuhusiana na model Q400 Next G badala ya kutanguliza hitimisho la hisia zako binafsi.
 
Yatakiwa CAG atembee hapo juu ya usalama wa kodi zetu,tuliambiwa kitu kipya ndani ya Miaka 2 service tena,imeingiza faida bei gani.Ni sahihi kumiliki kitu ambacho ni mzigo lengo kumfurahisha mwanasiasa Kwa gharama za kodi zetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka kadhaa iliyopita wakati najiunga na jf niliona ni jukwaa la wasomi kweli kweli
Lakini kadiri siku zinavyokwenda naona kabisa jukwaa limevamiwa na facebook
(Vilaza)
Ndege sio basi la kwenda Tarime
Ndio maana fast jet wamepigwa pin
Ukiendesha biashara ya ndege unatakiwa uwe mchalo kweli kweli
Ndege inakwenda na kilomita zikifika kilomita kadhaa utake ,usitake hata kama magurudumu yake bado yako bomba kama ya basi la abood la kwenda moro to dar unatakiwa utowe na uweke mengine alikadharika na vifaa vingine ni mtindo wa kutoa na kuweka vipya kabisa
Service ya ndege hakuna kuweka kifaa used kama bus ni mtindo ule ule wa bandika bandua hata kama ni kizima kinachotazamwa ni kilomita zake za service kutimia ..

Sent using Jamii Forums mobile app

Hata sijui umeandika nini [emoji1438]‍♂️... Watu wanahoji hizo gharama za service na faida inayotengeneza je vinaendana?
 
Back
Top Bottom