SGR wajenzi wa Ureno wamepotelea wapi?

SGR wajenzi wa Ureno wamepotelea wapi?

Wareno waliuacha mradi muda mrefu sana. Ila ipo chini ya mkeka. Kwa sasa wanaopiga mzigo ni waturuki peke yao. Inasemekana wareno hawakulipwa stahiki zao kama walivyokubaliana - wakafungasha kila kitu na kuondoka nchini.

Yapi Merkezi wanaweza kuwa wamepata guarantee kutoka kwa serikali yao (Uturuki) kwamba wasipolipwa na serikali yetu basi serikali yao itawalipa na kutudai sisi. Sidhani kama wareno walipata uhakika huo.
Kumbe pamoja na majigambo yote, mradi unarndeshwa kisanii hivyo?
 
Mkuu Kalamu1, Asante kwa hii. hapa umesema jambo moja la maana sana kuhusu ujio wa SGR na hatma ya malori.

Kenya walipoanza, ili deni la SGR lilipike, Kenya waliyapakia kwenye SGR kwa lazima all containers bound to Nairobi, makosa yakawa mengi kujikuta kuna containers za Mombasa zinapelekwa Nairobi, na bado SGR haishibi.

Kwa Tanzania, SGR ni Central Corridor tuu, wakati the busiest route ni Southern Corridor, hivyo hata SGR ikianza, bado wenye malori watabeba mizigo ya Tunduma.

Na ili SGR ilipe, inahitaji mzigo wa kushiba haswa, hivyo ikianza ni lazima kulazimisha containers zote za Morogoro Rd, zipelekwe kwa SGR hadi Moro Dry Port na safari sasa zitaanzia Moro. Ikifika Dodoma, vivyo hivyo.

Maadam jirani zetu wametangulia, na SGR yao imeanza kuwa a white elephant, hakuna ubaya kujifunza kwa wenzetu, ili sisi yasitukute yaliyowakuta wenzetu hawa.


Reli ya SGR: Je, Tujifunze kwa wenzetu Kenya kuepusha SGR yetu kuwa ‘A White Elephant’? Wenzetu yameshawakuta... - JamiiForums

P.
Kwa hiyo containers zinazoishia kibaha, Chalinze au bagamoyo huoni kama watakuwa wameongezewa gharama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usidanganywe na mtu. Malori hayaendi popote; na yataendelea tu kupiga mzigo kama kawa.

Naomba tusibishane juu ya hili. Natoa ushahidi wa SGR ya jirani zetu Kaskazini na SGR yao ya mChina. Malori yapo na yanaendelea, licha ya kuwekewa mizengwe wanyimwe mizigo!

Sasa hivi unaambiwa kusafirisha kontena toka bandarini hadi Nairobi la futi 20 ni Ksh 142,,000/; na lile la futi 40 ni Ksh 142000/ , na bado kontena hilo hujalifikisha nyumbani au kiwandani maanake inabidi ukachukue mzigo wako kituoni.

Kusafirisha mizigo hiyo kwa lori gharama zake ni Ksh.65,000/ kwa kontena la futi 20; na Ksh.85000/ kwa lile la futi 40, na tena linafikishwa hadi nyumbani au kiwandani kwako.

Hebu niambie kama wewe ni mfanya biashara, utaachaje kwenda na lori.

Serikali ikiacha pawepo na ushindani wa kibiashara huru bila ya mizengwe ya kulazimisha baadhi ya mizigo isafirishwe kwa reli ili deni la ujenzi liweze kulipwa, reli hiyo ingekuwa ni mzigo kama ile aliyojenga Mwingereza.

Sasa sijui hapa kwetu tofauti yake itakuwaje! Lakini nina hakika malori hayatapotea barabarani; maana hata kule kwa mabeberu, kwa waChina, kwa waJapan hatuoni malori yakipotea barabarani.

Themagufulianz, imenibidi nikujibu kwa kirefu hivi, kwa sababu naona ushabiki wa kushangilia kila kitu umepungua. Tujaribu kupima mambo kwa uhalisi wake, na sio kwa misingi ya kushabikia tu!.

Tuendelee kujenga taifa letu kwa utulivu.
SGR ya Kenya haiwezi kuwa reference maana ufisadi ulitamalaki na usisahau ngawira ya mkopo lazima irejeshwe mapema
 
Kilichofanyika baada ya Yapi kupata mradi waligawana vipande vya kufanya kazi na Motor wale wareno. Motor kwa upande wake akatafuta subcontractor tena na kuwauzia kazi lakini mitambo na mafuta wanachukua kwa Yapi.. Ikaonekana utekelezaji wa kipande cha Motor unayumba na hivyo kupelekea Yapi kuvunja mkataba na Motor mwezi wa kwanza 2019. Sasa hivi mradi unatekelezwa na Yapi
 
Hatuna kawaida hiyo ya kujifunza kwa wenzetu
Mkuu Kalamu1, Asante kwa hii. hapa umesema jambo moja la maana sana kuhusu ujio wa SGR na hatma ya malori.

Kenya walipoanza, ili deni la SGR lilipike, Kenya waliyapakia kwenye SGR kwa lazima all containers bound to Nairobi, makosa yakawa mengi kujikuta kuna containers za Mombasa zinapelekwa Nairobi, na bado SGR haishibi.

Kwa Tanzania, SGR ni Central Corridor tuu, wakati the busiest route ni Southern Corridor, hivyo hata SGR ikianza, bado wenye malori watabeba mizigo ya Tunduma.

Na ili SGR ilipe, inahitaji mzigo wa kushiba haswa, hivyo ikianza ni lazima kulazimisha containers zote za Morogoro Rd, zipelekwe kwa SGR hadi Moro Dry Port na safari sasa zitaanzia Moro. Ikifika Dodoma, vivyo hivyo.

Maadam jirani zetu wametangulia, na SGR yao imeanza kuwa a white elephant, hakuna ubaya kujifunza kwa wenzetu, ili sisi yasitukute yaliyowakuta wenzetu hawa.


Reli ya SGR: Je, Tujifunze kwa wenzetu Kenya kuepusha SGR yetu kuwa ‘A White Elephant’? Wenzetu yameshawakuta... - JamiiForums

P.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichofanyika baada ya Yapi kupata mradi waligawana vipande vya kufanya kazi na Motor wale wareno. Motor kwa upande wake akatafuta subcontractor tena na kuwauzia kazi lakini mitambo na mafuta wanachukua kwa Yapi.. Ikaonekana utekelezaji wa kipande cha Motor unayumba na hivyo kupelekea Yapi kuvunja mkataba na Motor mwezi wa kwanza 2019. Sasa hivi mradi unatekelezwa na Yapi
Okey
 
Hakuna somo la uzalendo mahali popote duniani,acheni kukariri kama kasuku, uzalendo unajijenga wenyewe pale viongozi wanapoamini mamlaka yote yanatoka kwa wananchi na wao ndio wenye haki ya kuchagua mustakbali wao wa maendeleo.
Madhara ya somo la uzalendo kutofundishwa mashuleni ndo naanza kuyaona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna TAZARA na bado mabasi yanajaa! Kuna mwendokasi Dar na dala dala zinajaa! SGR haiwezi ku satisfy demand itapunguza usumbufu kwa kiasi kikubwa. Na kuna wengi watakuwa hawawezi ku afford kupanda pia!
Treni ndio usafiri wa bei cheap kuliko zote so atakayeshindwa kuafford treni labda atembee kwa miguu.
 
Nyie ndio mliyoua reli sasa mtakoma inafufuka.
Nchi kama USA na China wana mtandao wa reli wa uhakika na unaofanya kazi kwa weledi lakini biashara ya malori ipo na inakuwa kila siku.
 
Binafsi mfatiliaji mzuri sana wa huu mradi wa SGR lakini nilisikia tu kuwa Yapi Merkezi na Motor Engine ya Ureno ndiyo wanajenga lakini sijawahi kuwaona Motor Engine tangia mradi uanze wala kuona gari lao au kifaa chochote kile naona Yapi Markezi ya Uturuki tu na nafikiri wao ndiyo wamechukua sehemu kubwa ya ujenzi na hata phase 2 ni Yapi Merkezi pekee watajenga labda tu Motor engine wao wanadili na issue nyingine.
wapo bwana njoo Gerezani Dar utawakuta
 
Treni ndio usafiri wa bei cheap kuliko zote so atakayeshindwa kuafford treni labda atembee kwa miguu.
Sio kweli. Kuna sehemu train inagharama hata mara 10 ya Bus. Mfano train kutoka London hadi Manchester inaweza kufika £100 wakati Bus inakuwa £10-15 hivi
 
siku hizi mnatafuta sababu yoyote ili mpinge tu.
Wewe umeambiwa ujenzi wa SGR unakamilika november habari za wajenzi zinakuhusu nini?
 
Back
Top Bottom