Serikali za CCM na kuwadharau walimu

Serikali za CCM na kuwadharau walimu

MAMBO MENGI YAMEKUA YAKIELEZWA ISIVYO,KAMA JAMBO HULIFAHAMU NI BORA USICHANGIE,WALIMU KAMA WATUMISHI WENGINE WA SERIKALI NI KWELI WANA KIPATO DUNI,LAKINI NAPINGANA NA DHANA KWAMBA NI WALIMU TU NDIO WANAPATA SHIDA YA KIPATO,UKWELI AMBAO WATU WENGI HAWATAKI KUUFAHAMU NI KUWA MISHAHARA YA WATUMISHI WA SERIKALI INAFANANA SANA ,KIKUBWA NI MTUMISHI HUYO ANA KIWANGO KIPI CHA ELIMU NA UZOEFU KAZINI,KINACHOTOFAUTISHA WALIMU NA WATUMISHI WENGINE NI MAISHA YA WIZI,UFISADI NA KULIPANA POSHO KUSIKO NA MSINGI,KWA MFUMO HUU WA JPM KUBANA MATUMIZI WATU WAISHI KWA MISHAHARA YAO NDIO MTAAMINI KWAMBA KAZI ZOTE ZINASTAHILI HESHIMA,WATANZANIA TUBADILIKE TUSIHUSUDU WATU WEZI KWA KUJIDANGANYA ETI WANA MISHAHARA MIKUBWA KUMBE WANAIBA PESA ZETU WENYEWE.FUATILIEN MISHAHARA YA WATUMISHI WOTE MLINGANISHE TENZ MTAGUNDUA MWALIMU ANAPATA MSHAHARA ZAIDI YA WATUMISHI WENGINE KWA KILA LEVEL IWE CERTIFICATE,DIPLOMA AU DEGREE,ANAYEWEZA KUBISHA HILI AJE NA FACTS,SIO POROJO TU
Kaka acha hizo bhana,mshahara wa Mwalimu wa certificate anayeanza kaz Leo ni sawa na posho ya kati kati ya mwezi ya polisi au askari.
Piga picha wewe Mwalimu unalipwa laki 3 kama mshahara toka tarehe 25 hadi tarehe 25 mwezi mpya kati kati ya mwezi hapa ni patupu lakini mwanajeshi au polisi wanalipwa hiyo laki 3 kama mshahara kisha tarehe 15 analipwa tena laki 2 hadi 3 za posho pia wanalipwa na ela ya pango ya nyumba kila mwezi.
Sasa huyu polisi au askari atafanana maisha na Mwalimu ambaye anapata laki 3 tu ndani ya siku 30 ? Bila posho wala chochote?
Hizo ndizo fact za serkali za ccm na dharau kwa walimu.
Usikoment kama uko political motivated
 
Ualimu ni taaluma nyeti sana,ila kila kilichonyeti hujificha lakini wao hujianika.
Ualimu unadharaulika kwa kuwa [HASHTAG]#inasemekana[/HASHTAG] ni kimbilio la waliofeli.
Hatutaweza kupata elimu bora kutoka kwa mwalimu aliyefeli masomo ambayo atakwenda kuyafundisha.
Walimu wameidharaulisha taaluma yao wenyewe kwa KULALAMIKA kila kukicha.
Hata ukimpa mwalimu mil.1 bado ataendelea kuyumba kiuchumi
Waliofaulu vizuri na kusomea ualimu hawalalamiki hata kidogo.
Ualimu ni taaluma ambayo ina asilimia kubwa ya watoto wa maskini ambao wao WANATEGEMEWA kwa kiwango kikubwa.
Ualimu si taaluma ya kuidharau kama UTAWALA ufanyavyo.HAKUNA TAALUMA YENYE WATU WAOGA KAMA UALIMU.
swali....:VIONGOZI WA CHAMA CHA WALIMU WAKO PALE KWA MASLAHI YA NANI?
KWANINI VIONGOZI HAWA WANA MAISHA BORA KULIKO WANAOWALIPA?
ombi langu kama MchovuWaFikra: TAKUKURU NA CAG WAKAFANYE KAZI KATIKA OFISI HIZI ZA CHAMA CHA WALIMU.
Maoni mazuri
 
"Walimu tuna hali ngumu walimu na sisi tu umuhimu walimu tutazua kitimutimu walimu kwenye wizara ya elimu" wagosi wa kaya
Hahahahahaha mkuu umenikumbusha zamani fulani hivi,lakini hadi leo serkali bado haujakumbuka wala Ku consider hali za walimu.
Wao wanakumbuka madawati tu alafu yakivunjwa na wanafunzi Mwalimu atalipa
 
Mimi mbona niko fresh tu, nalima zangu matikiti huku ifakara na chaki nashika bila mawazo.

Nachokumbuka walimu wanapomaliza vyuo wengi huwa wananyong'onyea wakipelekwa vijiji vya mbali, kosa kubwa huwa ni kukimbilia mijini na kamshahara ka laki nne.
 
Mimi mbona niko fresh tu, nalima zangu matikiti huku ifakara na chaki nashika bila mawazo.

Nachokumbuka walimu wanapomaliza vyuo wengi huwa wananyong'onyea wakipelekwa vijiji vya mbali, kosa kubwa huwa ni kukimbilia mijini na kamshahara ka laki nne.
Mkuu kama unalima matikiti lima kwa nguvu,kilimo kitaweza kukuokoa na dhiki laki vijiela vya mshahara wa Mwalimu ni shida unaweza kufa masikini
 
sio walimu tu watumishi wote wa selikali % kubwa wote njaa Kali mikopo ime jaa kila kona si bank si mtaan si magengen na madukani other wise awe na vitega uchumi mbadala au fisadi kama sio rushwa selikali iwa tazame wote si walimu tu Ila naamini walimu ni kada amabayo INA walimu wengi kuliko kada zote sina uhakika kama hata polisi wana weza kua wengi kama walimu sema walimu umoja ni ziro cku mki amua kurekebishiwa kila kitu kwa uwingi wenu mki paza sauti MNA weza
 
Kwamiaka mingi sana walimu wanaofundisha shule za serkali zote za msingi na secondary wamekuwa wakipata masrahi duni sana Tanzania ukilinganisha na watu wa kada nyingine.
Mwalimu wa Tanzania analipwa pesa mdogo sana mbali ya hapo halipwi posho,halipwi ela ya fani aliyosomea wala halipwi overtime. Maisha ya walimu ni magumu sana lakini hapo hapo serkali inatamka kila siku kuwa anataka kuboresha elimu ya Tanzania.
Elimu bora ni pamoja na walimu bora,Mwalimu atakuaje bora kama ana njaa??
Imefika kipindi hata waosha magari wa mitaani wanajiona wana pesa kuliko walimu wa Tanzania.
Hivi serkali za ccm kwani ninyi walimu mnawaonaje au mnawaona hawastahiri kulipwa vizuri?
Pole sana mkuu. Ila nakumbuka enzi za utawala wa jk waziri hawa ghasia aliwahi kutamka kwamba walimu hawawezi kulipwa mishahara mizuri kwa kuwa ni wengi...kwamba kwa sababu ya wingi wao, walilipwa vzr watamakiza fedha za serikali. Hakuishia hapo, ila aliwashauri walimu wasomee fani nyingine zinazolipa mishahara minene. Aidha aljsisitiza kuwa anaueona mshahara wake haumtoshi aache kazi. Hao ndio CCM katika ubora wao.
 
Tatizo ni namna tunavyofikiri na sivyo hali ilivyo kuna waalimu Nina ushahidi wana utajiri wa kutosha huwezi amini wana kila aina ya hali ya kuitwa wakwasi ila wapo waalimu choka mbaya kiasi cha kuidhalilisha hata taaluma yao tujiulize ni mini kinasababisha hali zao ziwe tofauti tena utakuta wengine wameanza kazi pamoja shule moja muundo mmoja na mshahara unaofanana."
The biggest problem is in the mind of the people and not what we see"
Hakuna mshahara Mkubwa wala Mdogo suala la msingi ni aina ya akili inayopokea huo mshahara inawaza nini?Hata kama Serikali ikipandisha kima cha chini cha mshahara kwa waalimu kuwa Milioni tank kama ikiwezekana bila Waalimu wenyewe kubadilika na kubadili namna wanavyofikiri bado mshahara huo hautotosha.
Ieleweke kinachomfanya Mtu aridhike ni mawazo yake na siyo kitu anachopata,mshahara haukuandaliwa kumtajirisha Mtu ila mawazo ya Mtu na maamuzi sahihi juu ya matumizi ya kila fedha inayopita mkononi mwake bila kujali ni nyingi au ni kidogo ndiyo yanayozalisha motives za utajiri au umasikini.
Mshahara upo kukidhi mahitaji ya muhimu ya mfanyakazi na siyo kumtajirisha au kumridhisha kwa kila hali na kila kitu.
 
Pole sana mkuu. Ila nakumbuka enzi za utawala wa jk waziri hawa ghasia aliwahi kutamka kwamba walimu hawawezi kulipwa mishahara mizuri kwa kuwa ni wengi...kwamba kwa sababu ya wingi wao, walilipwa vzr watamakiza fedha za serikali. Hakuishia hapo, ila aliwashauri walimu wasomee fani nyingine zinazolipa mishahara minene. Aidha aljsisitiza kuwa anaueona mshahara wake haumtoshi aache kazi. Hao ndio CCM katika ubora wao.
ukwel mtupu
 
Hii kada ya Ualimu siwezi kuihurumia kabisa.... Hawana umoja, hawana msimamo. So haya yote ni ugonjwa wankijitakia... I stand to be corrected!
Ni mwalimu aliyekuwezesha kuwa na ufahamu wa kuandika herufi hizi ulizo comment hapa hivyo hata kama hawana umoja lakini wahurumie wanapotendewa ndivyo sivyo
 
walimu wenyewe hawajitambui....hawawezi kugoma...
 
Serikali ni we we pia,sijui umesahau unataka Serikali ije ikusaidie kufikiri?tunapenda kulalamika sana lakini lawama huwa haisaidii na haijawahi kumsaidia MTU
Mbona hatutaki kujilaumu wenyewe kwanza?.
Mimi pia ni Mwalimu.
 
Pole sana mkuu. Ila nakumbuka enzi za utawala wa jk waziri hawa ghasia aliwahi kutamka kwamba walimu hawawezi kulipwa mishahara mizuri kwa kuwa ni wengi...kwamba kwa sababu ya wingi wao, walilipwa vzr watamakiza fedha za serikali. Hakuishia hapo, ila aliwashauri walimu wasomee fani nyingine zinazolipa mishahara minene. Aidha aljsisitiza kuwa anaueona mshahara wake haumtoshi aache kazi. Hao ndio CCM katika ubora wao.
Inachukiza sana hii,kwa staili hii watanzania tusitegemee elimu bora nchini
 
Tatizo ni namna tunavyofikiri na sivyo hali ilivyo kuna waalimu Nina ushahidi wana utajiri wa kutosha huwezi amini wana kila aina ya hali ya kuitwa wakwasi ila wapo waalimu choka mbaya kiasi cha kuidhalilisha hata taaluma yao tujiulize ni mini kinasababisha hali zao ziwe tofauti tena utakuta wengine wameanza kazi pamoja shule moja muundo mmoja na mshahara unaofanana."
The biggest problem is in the mind of the people and not what we see"
Hakuna mshahara Mkubwa wala Mdogo suala la msingi ni aina ya akili inayopokea huo mshahara inawaza nini?Hata kama Serikali ikipandisha kima cha chini cha mshahara kwa waalimu kuwa Milioni tank kama ikiwezekana bila Waalimu wenyewe kubadilika na kubadili namna wanavyofikiri bado mshahara huo hautotosha.
Ieleweke kinachomfanya Mtu aridhike ni mawazo yake na siyo kitu anachopata,mshahara haukuandaliwa kumtajirisha Mtu ila mawazo ya Mtu na maamuzi sahihi juu ya matumizi ya kila fedha inayopita mkononi mwake bila kujali ni nyingi au ni kidogo ndiyo yanayozalisha motives za utajiri au umasikini.
Mshahara upo kukidhi mahitaji ya muhimu ya mfanyakazi na siyo kumtajirisha au kumridhisha kwa kila hali na kila kitu.
Sikuungi mkono hoja yako,ukimuona Mwalimu ni tajiri na bado yuko kazini yawezekana familia yake ni tajiri kama ni Mwalimu wa kike wengi huwa na magari Lakini magari hayo hununuliwa na wanaume wao ambao hufanya kazi tofauti na za elimu.
Ukisema walimu wengi hawana ela kwasababu hawafikiri vizuri sio kweli.
Walimu wanapata low wages,what they get they consume all no surplus for tomorrow. Kiasi kwamba hawawezi kuweka akiba ya kesho au kutunza pesa na kupata mtaji labda waanzie biashara au mradi mwingine wowote.
Pia kumbuka kaz ya ualimu ni kazi ya watoto wa wakulima na watu wengine toka hadhi ya chini hawa wote kimbilio la ni kusomea ualimu maana ajira zake sio za kutoa rushwa au hazina kushikana mikono.
Sasa kutokana na walimu wengi wanatoka tabaka la chini hivyo wanakuwa na wategemezi wengi sana( extended family),kila kimshahara kidogo anachopata kinategemea na watu wengi hivyo hawez hata kutunza pesa ili apate mtaji afanyie ujasiliamali wowote.
Sio kweli kuwa walimu wengi hawafikiri vizuri ndiomaana wanakuwa choka mbaya.
 
walimu wenyewe hawajitambui....hawawezi kugoma...
Tatizo serkali imeweka vibaraka kwenye chama cha walimu (cwt),Hata kama walimu wapo tayari kufanya active resistance wanakosa nguvu toka juu,kuna fitina zinapenyezwa kuharibu huo umoja
 
Serikali ni we we pia,sijui umesahau unataka Serikali ije ikusaidie kufikiri?tunapenda kulalamika sana lakini lawama huwa haisaidii na haijawahi kumsaidia MTU
Mbona hatutaki kujilaumu wenyewe kwanza?.
Mimi pia ni Mwalimu.
Nani kakwambia serkali ni Mimi au wewe?
Acha kuleta Maneno ya kijiweni hapa.Serkali inajumuisha rais,makamu wa rais,waziri mkuu,mawaziri,manaibu mawaziri, wakurugenzi,na makatibu wakuu.Sasa wewe unawezaje kusema Mimi au wewe ni serkali?
Acha hizo wewe!
 
Kwani hao wote wanawawakilisha akina nani?ndiyo tulivyo hatutaki kuoneshwa kuwa Sisi ni sehemu ya sababu ya hali zetu.
Komaza akili yako
 
Back
Top Bottom