Serikali yatangaza alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Serikali imetangaza rasmi alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika kwenye Ofisi zote za Serikali na katika shughuli zote rasmi za kiserikali.

Aidha Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mindi Kasiga amezitaja alama hizo kuwa ni bendera ya Taifa, bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wimbo wa Taifa.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaratibu upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasisi, wizara au Ofisi husika.

Pia mkuu huyo wa kitengo cha mawasiliano ndugu Kasiga amesema kuanzia sasa bendera ya Jumuiya hiyo itapepea sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi zote za Serikali huku wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ukiimbwa sambamba na wimbo wa Taifa katika shughuli rasmi za serikali kuanzia ngazi za Halmashauri hadi Taifa, hii ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya hiyo kifungu cha 7(a).

EAC.jpg


Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa wizara ya mambo ya nje amenukuliwa akisema “Mkataba huu unasisitiza jumuiya hii kuwa jumuiya ya watu, hivyo watanzania watahusishwa katika hatua zote za mtangamano huo, pamoja na kushirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za jumuiya ili kujua madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zitakazaopatikana ndani ya Jumuiya hiyo”, Mwisho wa kunukuu.

Matumizi ya alama hizi ni njia mojawapo ya kujenga uzalendo na kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya ushirikiano huu.

Vilevile, taasisi binafsi zinaweza kutumia alama hizi, huku shule na vyuo vikisisitizwa kutumia alama hizi kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
 
Serikali imetangaza rasmi alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika kwenye Ofisi za Serikali na katika shughuli zote rasmi za kiserikali.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mindi Kasiga amezitaja alama hizo kuwa ni bendera ya Taifa, bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wimbo wa Taifa.

Kasiga amesema kuanzia sasa bendera ya Jumuiya hiyo itapepea sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi zote za Serikali huku wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ukiimbwa sambamba na wimbo wa Taifa katika shughuli rasmi za serikali kuanzia ngazi za Halmashauri hadi Taifa, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya hiyo kifungu cha 7(a).

“Mkataba huu unasisitiza jumuiya hii kuwa jumuiya ya watu, hivyo watanzania watahusishwa katika hatua zote za mtangamano huo, pamoja na kushirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za jumuiya ili kujua madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zitakazaopatikana ndani ya Jumuiya hiyo”,

Aidha, Kasiga ameongeza kuwa matumizi ya alama hizi ni njia mojawapop ya kujenga uzalendo na kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya ushirikiano huu.

Vilevile, taasisi binafsi zinaweza kutumia alama hizi, huku shule na vyuo vikisisitizwa kutumia alama hzi kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaratibu upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasisi, wizara au Ofisi husika.

AFRIKA MASHARIKI HOYEEE, mnaoamini katika utengano mtaisoma namba, hapa ni umoja tu.
 
Serikali imetangaza rasmi alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika kwenye Ofisi za Serikali na katika shughuli zote rasmi za kiserikali.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mindi Kasiga amezitaja alama hizo kuwa ni bendera ya Taifa, bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wimbo wa Taifa.

Kasiga amesema kuanzia sasa bendera ya Jumuiya hiyo itapepea sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi zote za Serikali huku wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ukiimbwa sambamba na wimbo wa Taifa katika shughuli rasmi za serikali kuanzia ngazi za Halmashauri hadi Taifa, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya hiyo kifungu cha 7(a).

“Mkataba huu unasisitiza jumuiya hii kuwa jumuiya ya watu, hivyo watanzania watahusishwa katika hatua zote za mtangamano huo, pamoja na kushirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za jumuiya ili kujua madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zitakazaopatikana ndani ya Jumuiya hiyo”,

Aidha, Kasiga ameongeza kuwa matumizi ya alama hizi ni njia mojawapop ya kujenga uzalendo na kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya ushirikiano huu.

Vilevile, taasisi binafsi zinaweza kutumia alama hizi, huku shule na vyuo vikisisitizwa kutumia alama hzi kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaratibu upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasisi, wizara au Ofisi husika.

AFRIKA MASHARIKI HOYEEE, mnaoamini katika utengano mtaisoma namba, hapa ni umoja tu.

Umoja upi huo ndani ya hiyo inayoitwa East Africa Community?, ndani ya hiyo EAC baada ya kuchukizwa na siasa za Kikwete, Rwanda, Uganda na Kenya wakatengeneza CoW ambapo humo Tanzania ilitengwa kwenye miradi na program zote kubwa za kimaendeleo, alivyoingia Magufuli kukafumuka triangle nyingine Tanzania, Rwanda na Uganda, Naona Kenya kawa sided out, ile Miradi mikubwa ambayo Kenya alijua ataipata yote imeamia Tanzania, unafikiri Kenya ana moyo tena wa EAC?,
sijui itakuwaje Raila akiingia Madarakani

East Africa bado sana,
 
Umoja upi huo ndani ya hiyo inayoitwa East Africa Community?, ndani ya hiyo EAC baada ya kuchukizwa na siasa za Kikwete, Rwanda, Uganda na Kenya wakatengeneza CoW ambapo humo Tanzania ilitengwa kwenye miradi na program zote kubwa za kimaendeleo, alivyoingia Magufuli kukafumuka triangle nyingine Tanzania, Rwanda na Uganda, Naona Kenya kawa sided out, ile Miradi mikubwa ambayo Kenya alijua ataipata yote imeamia Tanzania, unafikiri Kenya ana moyo tena wa EAC?,
sijui itakuwaje Raila akiingia Madarakani

East Africa bado sana,

mimi, hayati ghadafi, hayati jk nyerere, hayati nkruma, nk hamuwezi kutuelewa kabisa. hizo zingine ni changamoto tu, zaidi tunataka united states of africa
 
mimi, hayati ghadafi, hayati jk nyerere, hayati nkruma, nk hamuwezi kutuelewa kabisa. hizo zingine ni changamoto tu, zaidi tunataka united states of africa
Hiyo kitu hakuna na haitakuwepo, hivi unajua Nyerere na Nkuruma walishindwa wapi?
Nyerere alikuwa anataka umoja uanzie kwenye blocks kama hizi za East Africa, West Africa (Ecowas) kisha zije kuungana
Kwame alikuwa anataka umija wa Africa hata kwa vita, kama kuna nchi inakataa inavamiwa kijeshi na inaingizwa kinguvu kama walivyofanya USA,
Idea zote mbili zilifail na hazitakuja kutokea, hiyo ya East Africa ni Jumuiya ya kumegeana chuki kati ya nchi na nchi, nchi tatu zinaamua kuinyanyapaa nchi moja na baada ya muda wanaamia kwenye nchi nyingine,
 
hivi kwa mfano nchi za SADC zikianzisha shirikisho Tz tutakuwa kwenye mashirikisho mawili?
 
umoja huu bado una matatitizo lukuki,Tanzania inakataza wataalamu wake kwenda kujiendeleza kitaaluma kwenye nchi za jumuiya ya afrika, kisingizio eti kubana matumizi,mbona wakenya,wanyarwanda wamejaa kwenye vyuo vya bongo,,huu ushirikiano una unafiki mkubwa sana.
 
Dah! Hivi Magufuli yupo serious kuhusu hili la muungano, ni hatua nzuri na tutampa ushirikiano kama hatakua kiongozi wa kusuasua ovyo.
Japo siwaelewi Watanzania, maana mpo SADC na EAC, sasa vipi na SADC wakianzisha wimbo wao na bendera yao, itabidi muongeze kwenye nyimbo zenu. Sasa mtakua mnaimba nyimbo tatu kabla ya kila kikao cha kitaifa. Hehehe!! Yote poa kwa sababu hamjambo kwenye nyimbo, haswa Bongo flavor.... natania tu, msikurupuke.
 
Serikali imetangaza rasmi alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika kwenye Ofisi za Serikali na katika shughuli zote rasmi za kiserikali.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mindi Kasiga amezitaja alama hizo kuwa ni bendera ya Taifa, bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wimbo wa Taifa.

Kasiga amesema kuanzia sasa bendera ya Jumuiya hiyo itapepea sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi zote za Serikali huku wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ukiimbwa sambamba na wimbo wa Taifa katika shughuli rasmi za serikali kuanzia ngazi za Halmashauri hadi Taifa, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya hiyo kifungu cha 7(a).

“Mkataba huu unasisitiza jumuiya hii kuwa jumuiya ya watu, hivyo watanzania watahusishwa katika hatua zote za mtangamano huo, pamoja na kushirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za jumuiya ili kujua madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zitakazaopatikana ndani ya Jumuiya hiyo”,

Aidha, Kasiga ameongeza kuwa matumizi ya alama hizi ni njia mojawapop ya kujenga uzalendo na kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya ushirikiano huu.

Vilevile, taasisi binafsi zinaweza kutumia alama hizi, huku shule na vyuo vikisisitizwa kutumia alama hzi kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaratibu upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasisi, wizara au Ofisi husika.

AFRIKA MASHARIKI HOYEEE, mnaoamini katika utengano mtaisoma namba, hapa ni umoja tu.

Ushirikiano wa kiuchumi YES lakini muungano wa kisiasa NO. Tunahitaji jumuiya ya kiuchumi kama ile ya Ulaya (EEC). Kisiasa hatutaelewana na tutasababisha vurugu kwani sisi waafrika tuna ubinafsi na uroho wa madaraka.
 
Back
Top Bottom