mumagoma
Senior Member
- Jan 15, 2014
- 186
- 95
Kwa taarifa nilizopata toka vyanzo vya ndani hazina ni kwamba mpaka sasa asilimia kubwa kama si wote wanaolipwa kutokea hazina hawajalipwa mishahara yao. Na hii inatokana na serikali kutokuwa na hela mpaka Jana za kutosha kulipa mishahara.
Fedha ambazo zilitengwa kwa ajili ya kulipa mishahara zimelipwa kwa wanafunzi kama bumu yao ili wasikose kura za wanachuo maana mgomo wao ulishaanza kusambaa nchi nzima na hyo ingeathiri uchaguzi wa Oktoba kwa CCM.
Pia inasemekana naibu Waziri wa Fedha anataka kupiga kupata hela ya kampeni.
Kuna tetesi ati kuwa mshahara umetoka, jamani nithibitishieni nipo kijijini kwenda mpaka mjini nauli 30000/= kwenda tu bado kulala geust na nauli ya kurudia.
Mshahara wangu ni laki nne kasoro mimi mwalimu shule ya msingi!