Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,282
Serikali imewasilisha nia ya kukata rufaa Mahakama Kuu, kupinga hukumu na adhabu iliyotolewa na Mahakama ya Kisutu, dhidi ya aliyekuwa rais wa zamani wa TFF, Jamal Malinzi na katibu wake, Celestine Mwesigwa
====
UPANDE wa Mashtaka umewasilisha nia ya kukata rufaa Mahakama Kuu, kupinga hukumu na adhabu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi na Katibu wake, Celestine Mwesigwa.
Katika hukumu hiyo, iliyotolewa Desemba 11, 2019, Malinzi alitakiwa kulipa faini ya Sh 500,000 au kwenda jela mwaka mmoja, huku Mwesigwa, akitakiwa kulipa faini ya Sh 1milioni au kwenda jela miaka miwili baada ya Mahakama ya Kisutu kumtia hatiani katika mashtaka mawili, kati ya 20 yaliyokuwa yanamkabili.
Vigogo hao wa TFF walihukumiwa kifungo hicho baada ya kutiwa hatiani kwa mashtaka ya kughushi muhtasari wa kikao cha Kamati Utendaji ya Shirikisho hilo.
Uamuzi wa kukata rufaa umetolewa leo Jumatatu na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wankyo Simon, ambapo alisema upande wa mashtaka umewasilisha nia hiyo ya kukata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Simon alisema maombi hayo ya rufaa yaliwasilishwa Mahakama Kuu, Desemba 13, 2019.
Alidai kuwa wamewasilisha nia hiyo baada ya kutoridhishwa na adhabu ya hukumu hiyo iliyotolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Maira Kasonde, aliyekuwa akisikiliza shauri hilo katika makosa waliyotiwa hatiani washtakiwa hao.
====
UPANDE wa Mashtaka umewasilisha nia ya kukata rufaa Mahakama Kuu, kupinga hukumu na adhabu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi na Katibu wake, Celestine Mwesigwa.
Katika hukumu hiyo, iliyotolewa Desemba 11, 2019, Malinzi alitakiwa kulipa faini ya Sh 500,000 au kwenda jela mwaka mmoja, huku Mwesigwa, akitakiwa kulipa faini ya Sh 1milioni au kwenda jela miaka miwili baada ya Mahakama ya Kisutu kumtia hatiani katika mashtaka mawili, kati ya 20 yaliyokuwa yanamkabili.
Vigogo hao wa TFF walihukumiwa kifungo hicho baada ya kutiwa hatiani kwa mashtaka ya kughushi muhtasari wa kikao cha Kamati Utendaji ya Shirikisho hilo.
Uamuzi wa kukata rufaa umetolewa leo Jumatatu na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wankyo Simon, ambapo alisema upande wa mashtaka umewasilisha nia hiyo ya kukata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Simon alisema maombi hayo ya rufaa yaliwasilishwa Mahakama Kuu, Desemba 13, 2019.
Alidai kuwa wamewasilisha nia hiyo baada ya kutoridhishwa na adhabu ya hukumu hiyo iliyotolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Maira Kasonde, aliyekuwa akisikiliza shauri hilo katika makosa waliyotiwa hatiani washtakiwa hao.