Serikali yaanza kuhujumu Mameya Dar es Salaam

Serikali yaanza kuhujumu Mameya Dar es Salaam

Nilitarajia hujuma za kuwakwamisha UKAWA ziwepo. Sishangai kwa hayo yaliyotokea. Japo nimechukizwa na hujuma hizo.
Hata ukawa Wanafanya jitihada za Kumkwamisha magufuli na serikali yake. sisi tunawaangalia nani atashinda
Nilitarajia hujuma za kuwakwamisha UKAWA ziwepo. Sishangai kwa hayo yaliyotokea. Japo nimechukizwa na hujuma hizo.
Hata ukawa Wanafanya jitihada za Kumkwamisha magufuli na serikali yake. sisi tunawaangalia nani atashinda
 
Unaposema HAPA KAZI TU hatufikirii tena kuwe na mizengwe ya Kijinga kama hii....hizi ni siasa za kipumbavu kabisa! Kazi tu mana yake siasa kama hizi zinazoondoa maendeleo hazina nafasi....
 
meya ni speaker wa baraza la madiwani tu. tatizo wanaingilia kazi za utendaji kama huyo wa kinondoni utadhani ndio mkurugenzi wa wilaya. mameya wa ukawa hawaelewi kazi yao wanadhani wao ndio serikali kwenye maeneo yao kumbe serikali ya magufuli ya ccm ndio inaongoza nchi.
Nadhani wewe ndio hujui majukumu ya meya. ...nenda kasome upya majukumu ya meya na utekelezaji wake. ....au angalia organogram ya manispaa then utajua meya ni nani. ...
 
Wana Wimbo Wao Wenyewe, CCM Ni Ile Ile..!
Sijui Kama Watanganyika Wengi Waliuelewa Vema Wimbo Ule!
 
Siasa za ccm za kishamba san.Sasa kwa taarifa yao na uchaguzi ujao tutawachagua tena kwa wingi Zaidi..kama ilivyokuwa mbeya na arusha
 
Huyo meya hajaeleza muda alioomba kibali kabla ya tarehe ya safari. Pengine kwa sababu maombi ni mengi ingebidi aombe kama mwezi au zaidi kabla ya safari ili kama hakupewa kibali basi ana nguvu na hoja ya kusema.Pili yake kwani alizuiwa kufuatilia na kujua kibali chake kimeishia wapi kama meya? Si angeenda mwenyewe katika ofisi husika maana isijekuwa ilikuwa ni uzembe tu wa ofisa kutoa barua sehemu na kupeleka sehemu nyingine.
 
Umeshashirikisha ubongo?

Naona unachohitaji ni ku-win an argument!! A classical Mdanganyika....hampendi kufikiria kwa kina pale kunapokuwa na hoja mbadala or possibly learn from other neutral minds. Shida ya watu aina yako wanafikiri wako sahihi kila wakati na wanadhani kwamba Mtanzania yeyote ni either CCM or UKAWA. Na kwa mbaali pia mnafikiri kuwa kama mtu hatakuwa katika moja ya hizo blocks 2 basi labda atakuwa ACT. Very unfortunate. Pole mkuu.

Nevertheless, I made my point very clear hapo juu kutokana na uzoefu wangu wa kiungozi nje na ndani ya Tanzania. Wanaohusika wana hiari ya kuyazingatia mawazo yangu au kuyapuuzia. But time is the best judge. Mbinu zilizofanikiwa jana usifikiri zitafanikiwa kesho pia. Kumbuka kuwa hata mbinu za adui yeyote yule makini huwa zina-evolve !!!
 
serikali ifike pahali iweke siasa kando tushughulike na maendeleo . maendeleo hayana chama...

Mkuu umenene vizuri. Ila liko tatizo moja kila siku vyama vya Upinzani Na mashabiki wanamtukana JPM,Wanaihujumu serikali yake Na Ufuska mwengi tu.Chakushangaza mameya Na ma diwani wako chini ya chama tawala .Kama upinzani ungeongoza nchi wangekubali haya?Wapinzani walimzoea Mzee wa Msoga.JPM ndio komesha
Hakuna Tundu,Mdee wala Yule mdada wa UK(UKerewe).WaTanzania tutanyooka tu maana hamna namna.
 
Hii ni aibu hasa kwa Simbachawene ambaye kesha onyesha dhahiri chuki zake kwa viongozi hao.
Lakini wanachoshindwa kujua ni kuwa ukimchukia Meya wa Dar umewachukia wananchi wa Dar. Waangalie Kule Arusha, walionyesha chuki ya wazi kabisa kwa Lema kilichofuata ni hata ule uhai mdogo wa ccm uliokuwepo wakaumalizia kabisa.
Hizi ni siasa za kishamba kabisa na kama bwana mkubwa anajua na kunyamaza ajue anajimaliza. Akikosa support ndani ya mji mkuu ndio kunalizika kwake, hao wakina Simbachawene na Makonda watanponza, hiyo Dar asijekuta anazomewa ikawa taabu bure!

Jifarijini tu.Kila siku nyie upinzani Ni matusi ,kejeli Na uhujumu wa Serikali ya JPM
Hivi ushirikiano gani mtapata.DAR haiwezi kuwa Kama Arusha kamwe.
 
12919772_837466583066878_5369977595504066415_n-jpg.357871
I really do
 
Sasa huyu Meya hatokani na chama cha kijani, halafu matumizi ya safari yake hayakuwa yana lipwa na serikali. Kwani alitakiwa kuomba ruhusa Ikulu au alitakiwa kuomba ruhusa Chadema?
Mimi naona kama alijichanganya maana yy japo yuko kiutendaji serikalini bali ki utawala hatawaliwi na serikali ya Ccm.

Mmmmmmmmmm someni katiba jamani.
 
Chadema kimekua chama cha watu wa kulia lia tu
Meya mzima analilia safari hana tofauti na msigwa alielilia kwenda Libya
Meya anajaribu kuhadaa umma eti kukosa kwake kwenda kwenye kongamano kakosa msaada wa kutengeneza mto mlalakuwa
Ili upate msaada unaandika andiko la mradi,wafadhili wanaweza kutuma mtu kukagua,halafu wanajadi ukipitishwa unajulishwa,unatoa namba za akaunti wanaingiza fedha,hakuna mambo ya kongamano.
Mstahiki meya ana uchungu tu wa kukosa safari ya kuosha macho kwa mandela
 
Usimbane sana na wewe ungezama kidogo. Serikali imenizuia, Ilipaswa nicommunicate hizi changes kwa mfadhili mapema na kumpa hii option ya teleconference kama inawezekana maana kama mtu ameamua kukusaidia na ukamueleza uhalisia na ikibidi ukampa contact za uhakika kujilidhisha, Nio hiyohiyo ya kutaka niudhulie anaweza kuihamishia kwenye kuongeza option ya Teleconference. Ndio maana jamaa anataka kujua huyu meya alistruggle vipi kutafuta alternative au alikata tamaa na kusubili kutoa tamko. Lazima atueleze na initiative zake alizofanya na ikibidi ushahidi wa maandishi/emails/barua
A great thinker. Siku hizi ukialikwa mkutanoni.. Kama ratiba yako hairuhusu, una-apologize na kisha kuwapa option ya kuchangia kwa video conference. watakupa ratiba, presentation yako utaifanya kwa video conference na utapata comments hapohapo. Usipotoa hiyo option wanakuona mburula pia. Hii inakubalika kwa mikutano karibu yote ya kimataifa.
 
KWANZA TAARIFA YAKO IMENIUMIZA SANA MOYO WANGU KWANI INATUHUSU SISI WANANCHI.Mhe. kwa hili hebu tupate uthibitisho kwa kutafuta appoint wewe pamoja na Viongozi wenzako kufika Ikilu na kumueleza Rais hujuma hii na majibu yake ndiyo yatawapa mwanga kuwa ni wale wale au ni hujuma za vingozi wa ngazi za chini japo kuwa tamko la kuzuia safari za nje yeye Rais ndiye aliye litoa kuwa ni lazima patolewe kibali au ruhusa na sii kuwazuia kwenda nje ya nchi hasa tena kwa manufa ya Taifa.

Na hakika hao wanao fanya hizi hujuma Mungu kawalaani kwa kuwanyima maarifa kwani hawawakomoi ninyi viongozi bali wanatukomoa sisi wananchi kwa kukosa huduma za msingi kwa kusaidiwa na Wahisani ambapo nchi yetu ulishindwa kuwekewa misingi ya kujitegemea pamoja na kuwa na Rasimali zote na kubarikiwa na Mungu kuwa na asali na maziwa lakini viongozi walishindwa na wanashindwa kuzitumia badala yake ni siasa za kipuuzi tu kuziendeleza.

Hakika endapo Viongozi wetu hawato badilika kuna uwezekano mkubwa kwenda kulitumbukiza Taifa ktk Majanga makubwa sana na wao pia hawatokuwa salama na familia zao...na hata kwa Mungu pia hawatojificha au kutumia vyeo vyao na Pesa zao kujinusuru.Taifa hili ni letu sote na si la watu flani hasa wenye upeo mdogo wa kufikiri tu, au chama flani NEVER...Na kama ni kweli Mungu azidi kuwalaani na kuzidi kuwanyima akili na maarifa na awape adhabu stahiki kwa kutunyima na kuwashindwa kutupatia huduma za msingi na maendeleo hadi leo hii...MUNGU AWAPE ADHABU YAKE SAWASAWA NA MATENDO YAO.

Dua la kuku.
Kama Ni kweli mbona hakuwaaita waandishi wa habari.Mara ngapi kawaita kwamba MAKONDA anamuingilia kazi zake Na hawahiitaji Pesa za serikali kujiendesha kodi za Wananchi zinatosha.Huwezi kuwa mbabe Kwa mwenye nyumba kama umekodi chumba.
 
Back
Top Bottom