Serikali yaanza kuhujumu Mameya Dar es Salaam

Serikali yaanza kuhujumu Mameya Dar es Salaam

Meya alitakiwa aambatane na baadhi ya waajiriwa pale Manispaa.. Hao sasa ndo wasingeweza kwenda bila ya kibali toka Ikulu.. Angeenda mwenyewe Meya sidhani kama ingeleta picha nzuri huko kwa wafadhili na kusababisha kuonekana longolongo..

Meya yuko sawa kuwahabarisha wananchi maana vita wanayopigwa ni kubwa sana.. Kuhamisha makusanyo ya kodi ya majengo toka kwa manispaa, ni moja ya hujuma ambayo viongozi wa upinzani kwenye manispaa wamefanyiwa..
Mkulu alimwambia Paulo nmekupa jiji waoneshe kua unaweza (kuwakomoa/fitna) ndo mana utamwona kla siku yeye tu kwene media
Tz kujikwamua kiuchumi itachukua mda sana
 
Inatia uchungu sana yan watu tunaish kama wakimbizi kwenye nnchi yetu wenyewe
 
Nimesoma kwa makini lakini sijaona substance ya kutosha ku-justify malalamiko ya Meya wetu.

Hoja alizozitaja zote ni hoja nyepesi kabisa. Vikwazo hivyo vinahitaji mtu aliyekomaa kiuongozi tu ili ku-nevigate so easily. Dizaini kama watu washaanza kutafuta huruma kwa wananchi.

Swali langu kwa Meya wangu ni kwamba ina maana alitarajia ushirikiano "mkubwa" na unaostahili kutoka CCM na serikali yake?? Ina maana UKAWA walitarajia mteremko kwenye utendaji wao???? Kwanini Mameya wetu wa Dar hawajifunzi kutoka kwa Mameya wengine wenye uzoefu kutoka kwenye maeneo ambayo upinzani una uzoefu wa Umeya kwa muda mrefu kidogo hapa nchini Tanzania au hata kutoka nchi nyingine???

Wale wenzangu wanaoangalia kila jambo linaloletwa na chama chao kwa jicho la aina moja tu inabidi watuvumilie sisi wengine. Huwa sivutiwi kiutendaji hata chembe na mtu ambaye akikutana na changamoto zozote zile kwenye utendaji wake wa kila siku yeye anachofanya badala ya kuendelea kupambana kwa kuleta actionable and sustainable solutions, yeye analalamika na ku-transfer lawama za kushindwa kwake kwa watu wengine. Hii ni sifa ya watu weak na wanaofanikiwa kisanii sanii tu.

Wale waliokaribu na hawa viongozi wetu wa upinzani wawaambie ukweli. Lazima wabadilike. Strategy ya kulalamika inaweza isisaidie kila wakati. They ought to show strong leadership traits and practices to outshine the ruling wing (CCM). Wakiwa bold and strategic enough, CCM hawatakuwa na ujanja but to automatically give way. No shortcuts in my view....hii ya kulialia tena kwa hoja dhaifu ni strategy mfu kwa dunia ya sasa.
 
umeniangusha sana meya unasubiri kibali cha nini,kwea pipa ataisoma namba ukirudi hawezi kukuvua umeya yeye hajakuteua ahaha huyu jamaa veepee
 
wewe ukisubili ruhusa itakula kwako,kama pesa yote ya safali watatoa wao siku nyingine,we nenda tu maana hawato kuvua umeya
Kwani Meya ni mtumishi wa serikali mpaka aombe kibali cha kusafiri? Pili kusafiri kwa kuomba kibali kulikuja kwa ajili ya kubana matumizi ya fedha za serikali, sasa inakuwaje mtu anagharimiwa kila kitu na mwenyeji wake kisha aombe kibali?
 
Nilifikiri awamu ya tano haitaendekeza siasa uchwara, Rais wetu alisema atakuwa raisi wa watu na vyama vyote. Kwa hiyo inawezekana hajui kinachoendelea huku chini. Katika mambo yanayoweza kuturudisha nyuma kiuchumi mojawapo ni kuendekeza siasa uchwara.. Tujaribu kuangalia Zanzibar na siasa zao.. Hapa kazi tu, maana yake hatuna longo longo za siasa...so sad
Hapana
 
Nilifikiri awamu ya tano haitaendekeza siasa uchwara, Rais wetu alisema atakuwa raisi wa watu na vyama vyote. Kwa hiyo inawezekana hajui kinachoendelea huku chini. Katika mambo yanayoweza kuturudisha nyuma kiuchumi mojawapo ni kuendekeza siasa uchwara.. Tujaribu kuangalia Zanzibar na siasa zao.. Hapa kazi tu, maana yake hatuna longo longo za siasa...so sad
yeye ndo anatoa kibali
 
inasikitisha sana kuwa siasa za kivyama zinaingizwa kuzuia maendeleo na uchapaji kazi !! na haswa ikiwa haya yanafanywa na viongozi wa juu serikalini. Uchaguzi umeishapita na badala ya ushirikiano inakuwa ni kukomoana na kuwekeana vikwazo.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI YAANZA KUHUJUMU MAMEYA DSM

Habari za mchana ndugu waandishi wa habari na wananchi wote ndani ya Manispaa ya Kinondoni, awali ya yote nimshukuru mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia pumzi na uhai mpaka leo hii, alikadhalika niwe miongoni mwa wengi tunaowatakia heri ndugu zetu Waislamu, katika mwezi huu Mtukufu wa tiba, mwenyezi Mungu awajalie heri na kuzisikia funga ziwe zenye Baraka kwao na jamii kwa ujumla.

Baada ya kutoa utangulizi huo, ndugu zangu waandishi wa habari na wananchi wa Kinondoni, sio kawaida yangu kuongea habari zinazohusu Serikali Kuu, kwa kuwa ninaamini kuwa Maendeleo ya Wananchi wa Mkoa huu wa Dar es salaam na Wilaya ya Kinondoni, hayawezi kuletwa kwa ubinafsi wa viongozi, bali ushirikiano mwema ya sisi tuliopewa dhamana ya kuziongoza Halmashauri kutoka vyama vinavyounda UKAWA, na CCM wanaounda Serikali Kuu. Jambo hili hufanya tuwe kimya na wavumilivu mara nyingi sana, ingawa bado kuna mahusiano ya kutia shaka kila kukicha.

Ila leo ndugu zetu waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla, tumeamua kuandika na kufikisha ujumbe huu kwenu, ili mjue yalipofikia kama viongozi na Serikali Kuu na mabaya yanayoendelea na ya kusikitisha sana.

Na kusema huku, tutafanya viongozi wakuu wa nchi kama walikuwa hawajui wajue au walitoa baraka hizi, basi sawa watusikie masikitiko yetu haya, kwa kuwa tulikuwa na imani nao sana na bado tutaendelea kuwa na imani nao kama Serikali juu ya kutatua changamoto na matatizo ya Wananchi.

Hali ya kimahusiano kati ya Mameya wanaotokana na UKAWA na Serikali Kuu si mazuri hata kidogo, viongozi tumeamua tuhabarishe umma wa Watanzania kuwa kuna hujuma za waziwazi zinazofanywa na wenzetu juu ya shughuli za Mameya wa Kinondoni, Ilala na Jiji la Dar es salaam.

Si mara ya kwanza hii kwa sisi Mameya kuhisi kuhujumiwa na baadhi ya viongozi serikalini ambao kimsingi, sisi tuliamini uchaguzi umeshapita na kwamba kila mmoja wetu atampa mwenzake heshima inayostahili juu ya ajenda za Maendeleo, ndiyo maana kama nilivyo sema hapo awali, tumekuwa kimya juu ya vikwazo vidogo vidogo ambavyo tulihisi ni hujuma lakini tukaamua kuwa kimya na wavumilivu lakini tunatambua kuwa ipo mikakati ovu mingi dhidi yetu, ya kutukwamisha tusifanikiwe kuleta Maendeleo ndani ya Mkoa wetu na Wilaya zetu, hata tulipo amua kuvumilia uchokozi wa wawaziwazi wa kejeli za kutishia kunyang'anya Mameya magari na vinginevyo, kutoka kwa mtu tunaye muheshimu kama Waziri wa TAMISEMI ofisi ya Rais, akidai wakurugenzi watupore magari tena mbele ya vyombo vya habari.

Ila sasa hujuma zimefika mahali pabaya kiasi kwamba kutukwamisha kupata misaada ya Maendeleo kutoka kwa nchi rafiki na Halmashauri zilizopo Dar es salaam.

Binafsi Manispaa ya Kinondoni nilishawahi kunyimwa ruhusa nisisafiri kwenda nchini Afrika ya Kusini nilipokuwa nimealikwa na wahisani waliotaka kunifadhili kutengeneza mto Mlalakuwa, uliokuwa utengenezwe kingo zake kuanzia Goba,Makongo juu mpaka Kata ya Kawe kuelekea baharini, wafadhili hao ni ICLEI-local government sustainability, mradi ambao ulikuwa unafanyika nchi nyingi za Afrika.

Mbali nakuwa wafadhili walikubali kulipia usafiri,malazi na gharama zote za kongamano lililokuwa lifanyike huko Afrika Kusini, nchi zote zilifika katika kongamano la CIP AIRR, lakini uwakilishi wetu ulikosekana kwa kisingizio cha ruhusa kutopatikana, madhara yake Manispaa ya Kinondoni ikaondolewa kwenye programu ya kufadhiliwa huku nchi kama Ghana,Kenya,Zambia na nyinginezo zikifadhiliwa. Baada ya mkutano kuisha nchini Afrika Kusini, Katibu Mkuu kiongozi akaniandikia kibali cha kusafiri, baada ya kongamano kuisha na kukosa kiasi cha tshs Bilioni 1.3.

Pamoja na hayo, Ubalozi wa Uturuki ulikuwa umedhamini safari ya Mameya kwenda Uturuki kukutana na wadau na wafadhili wa miradi mbalimbali ikiwemo ikiwemo Chuo Cha Ufundi ndani ya Manispaa ya Kinondoni, Ubalozi huo ulikuwa umeshatoa kibali cha kusafiri (Visa) lakini Serikali imevunja Safari hiyo.

Kwa kufanya hivi Serikali imezikosesha Manispaa zetu fursa za Maendeleo ikiwemo Chuo hicho cha Ufundi.

IMETOLEWA NA MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI:

BONIFACE JACOB.
IJUMAA 17/06/2016
Hii issue mbona Simple Tu, Omba Appointment ya kuonana na Mh. Raisi pale magogoni kisha mweleze hizi shida ulizozipata, kuweka post ndeeefu humu haitaweza kutatua hili tatizo bali itaonekana kuwa shida hii mnataka kuitumia kama mtaji wa kisiasa. Come on Tufanyeni kazi sasa.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI YAANZA KUHUJUMU MAMEYA DSM

Habari za mchana ndugu waandishi wa habari na wananchi wote ndani ya Manispaa ya Kinondoni, awali ya yote nimshukuru mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia pumzi na uhai mpaka leo hii, alikadhalika niwe miongoni mwa wengi tunaowatakia heri ndugu zetu Waislamu, katika mwezi huu Mtukufu wa tiba, mwenyezi Mungu awajalie heri na kuzisikia funga ziwe zenye Baraka kwao na jamii kwa ujumla.

Baada ya kutoa utangulizi huo, ndugu zangu waandishi wa habari na wananchi wa Kinondoni, sio kawaida yangu kuongea habari zinazohusu Serikali Kuu, kwa kuwa ninaamini kuwa Maendeleo ya Wananchi wa Mkoa huu wa Dar es salaam na Wilaya ya Kinondoni, hayawezi kuletwa kwa ubinafsi wa viongozi, bali ushirikiano mwema ya sisi tuliopewa dhamana ya kuziongoza Halmashauri kutoka vyama vinavyounda UKAWA, na CCM wanaounda Serikali Kuu. Jambo hili hufanya tuwe kimya na wavumilivu mara nyingi sana, ingawa bado kuna mahusiano ya kutia shaka kila kukicha.

Ila leo ndugu zetu waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla, tumeamua kuandika na kufikisha ujumbe huu kwenu, ili mjue yalipofikia kama viongozi na Serikali Kuu na mabaya yanayoendelea na ya kusikitisha sana.

Na kusema huku, tutafanya viongozi wakuu wa nchi kama walikuwa hawajui wajue au walitoa baraka hizi, basi sawa watusikie masikitiko yetu haya, kwa kuwa tulikuwa na imani nao sana na bado tutaendelea kuwa na imani nao kama Serikali juu ya kutatua changamoto na matatizo ya Wananchi.

Hali ya kimahusiano kati ya Mameya wanaotokana na UKAWA na Serikali Kuu si mazuri hata kidogo, viongozi tumeamua tuhabarishe umma wa Watanzania kuwa kuna hujuma za waziwazi zinazofanywa na wenzetu juu ya shughuli za Mameya wa Kinondoni, Ilala na Jiji la Dar es salaam.

Si mara ya kwanza hii kwa sisi Mameya kuhisi kuhujumiwa na baadhi ya viongozi serikalini ambao kimsingi, sisi tuliamini uchaguzi umeshapita na kwamba kila mmoja wetu atampa mwenzake heshima inayostahili juu ya ajenda za Maendeleo, ndiyo maana kama nilivyo sema hapo awali, tumekuwa kimya juu ya vikwazo vidogo vidogo ambavyo tulihisi ni hujuma lakini tukaamua kuwa kimya na wavumilivu lakini tunatambua kuwa ipo mikakati ovu mingi dhidi yetu, ya kutukwamisha tusifanikiwe kuleta Maendeleo ndani ya Mkoa wetu na Wilaya zetu, hata tulipo amua kuvumilia uchokozi wa wawaziwazi wa kejeli za kutishia kunyang'anya Mameya magari na vinginevyo, kutoka kwa mtu tunaye muheshimu kama Waziri wa TAMISEMI ofisi ya Rais, akidai wakurugenzi watupore magari tena mbele ya vyombo vya habari.

Ila sasa hujuma zimefika mahali pabaya kiasi kwamba kutukwamisha kupata misaada ya Maendeleo kutoka kwa nchi rafiki na Halmashauri zilizopo Dar es salaam.

Binafsi Manispaa ya Kinondoni nilishawahi kunyimwa ruhusa nisisafiri kwenda nchini Afrika ya Kusini nilipokuwa nimealikwa na wahisani waliotaka kunifadhili kutengeneza mto Mlalakuwa, uliokuwa utengenezwe kingo zake kuanzia Goba,Makongo juu mpaka Kata ya Kawe kuelekea baharini, wafadhili hao ni ICLEI-local government sustainability, mradi ambao ulikuwa unafanyika nchi nyingi za Afrika.

Mbali nakuwa wafadhili walikubali kulipia usafiri,malazi na gharama zote za kongamano lililokuwa lifanyike huko Afrika Kusini, nchi zote zilifika katika kongamano la CIP AIRR, lakini uwakilishi wetu ulikosekana kwa kisingizio cha ruhusa kutopatikana, madhara yake Manispaa ya Kinondoni ikaondolewa kwenye programu ya kufadhiliwa huku nchi kama Ghana,Kenya,Zambia na nyinginezo zikifadhiliwa. Baada ya mkutano kuisha nchini Afrika Kusini, Katibu Mkuu kiongozi akaniandikia kibali cha kusafiri, baada ya kongamano kuisha na kukosa kiasi cha tshs Bilioni 1.3.

Pamoja na hayo, Ubalozi wa Uturuki ulikuwa umedhamini safari ya Mameya kwenda Uturuki kukutana na wadau na wafadhili wa miradi mbalimbali ikiwemo ikiwemo Chuo Cha Ufundi ndani ya Manispaa ya Kinondoni, Ubalozi huo ulikuwa umeshatoa kibali cha kusafiri (Visa) lakini Serikali imevunja Safari hiyo.

Kwa kufanya hivi Serikali imezikosesha Manispaa zetu fursa za Maendeleo ikiwemo Chuo hicho cha Ufundi.

IMETOLEWA NA MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI:

BONIFACE JACOB.
IJUMAA 17/06/2016
inasikitisha sana lakini meya sio muajiriwa .nakushauri nenda kwa nguvu ukikosa nauli pita mtaani tutakuchangia.nahisi tunaongozwa na wafu,siasa ya kiafrika ni chafu na hatutakaa tuendele hata kwa machozi,
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI YAANZA KUHUJUMU MAMEYA DSM

Habari za mchana huu ndugu waandishi wa habari na wananchi wote ndani ya Manispaa ya Kinondoni, awali ya yote nimshukuru mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia pumzi na uhai mpaka leo hii, alikadhalika niwe miongoni mwa wengi tunaowatakia heri ndugu zetu Waislamu, katika mwezi huu Mtukufu wa tiba, mwenyezi Mungu awajalie heri na kuzisikia funga ziwe zenye Baraka kwao na jamii kwa ujumla.

Baada ya kutoa utangulizi huo, ndugu zangu waandishi wa habari na wananchi wa Kinondoni, sio kawaida yangu kuongea habari zinazohusu Serikali Kuu, kwa kuwa ninaamini kuwa Maendeleo ya Wananchi wa Mkoa huu wa Dar es salaam na Wilaya ya Kinondoni, hayawezi kuletwa kwa ubinafsi wa viongozi, bali ushirikiano mwema ya sisi tuliopewa dhamana ya kuziongoza Halmashauri kutoka vyama vinavyounda UKAWA, na CCM wanaounda Serikali Kuu. Jambo hili hufanya tuwe kimya na wavumilivu mara nyingi sana, ingawa bado kuna mahusiano ya kutia shaka kila kukicha.

Ila leo ndugu zetu waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla, tumeamua kuandika na kufikisha ujumbe huu kwenu, ili mjue yalipofikia kama viongozi na Serikali Kuu na mabaya yanayoendelea na ya kusikitisha sana.

Na kusema huku, tutafanya viongozi wakuu wa nchi kama walikuwa hawajui wajue au walitoa baraka hizi, basi sawa watusikie masikitiko yetu haya, kwa kuwa tulikuwa na imani nao sana na bado tutaendelea kuwa na imani nao kama Serikali juu ya kutatua changamoto na matatizo ya Wananchi.

Hali ya kimahusiano kati ya Mameya wanaotokana na UKAWA na Serikali Kuu si mazuri hata kidogo, viongozi tumeamua tuhabarishe umma wa Watanzania kuwa kuna hujuma za waziwazi zinazofanywa na wenzetu juu ya shughuli za Mameya wa Kinondoni, Ilala na Jiji la Dar es salaam.

Si mara ya kwanza hii kwa sisi Mameya kuhisi kuhujumiwa na baadhi ya viongozi serikalini ambao kimsingi, sisi tuliamini uchaguzi umeshapita na kwamba kila mmoja wetu atampa mwenzake heshima inayostahili juu ya ajenda za Maendeleo, ndiyo maana kama nilivyo sema hapo awali, tumekuwa kimya juu ya vikwazo vidogo vidogo ambavyo tulihisi ni hujuma lakini tukaamua kuwa kimya na wavumilivu lakini tunatambua kuwa ipo mikakati ovu mingi dhidi yetu, ya kutukwamisha tusifanikiwe kuleta Maendeleo ndani ya Mkoa wetu na Wilaya zetu, hata tulipo amua kuvumilia uchokozi wa wawaziwazi wa kejeli za kutishia kunyang'anya Mameya magari na vinginevyo, kutoka kwa mtu tunaye muheshimu kama Waziri wa TAMISEMI ofisi ya Rais, akidai wakurugenzi watupore magari tena mbele ya vyombo vya habari.

Ila sasa hujuma zimefika mahali pabaya kiasi kwamba kutukwamisha kupata misaada ya Maendeleo kutoka kwa nchi rafiki na Halmashauri zilizopo Dar es salaam.

Binafsi Manispaa ya Kinondoni nilishawahi kunyimwa ruhusa nisisafiri kwenda nchini Afrika ya Kusini nilipokuwa nimealikwa na wahisani waliotaka kunifadhili kutengeneza mto Mlalakuwa, uliokuwa utengenezwe kingo zake kuanzia Goba,Makongo juu mpaka Kata ya Kawe kuelekea baharini, wafadhili hao ni ICLEI-local government sustainability, mradi ambao ulikuwa unafanyika nchi nyingi za Afrika.

Mbali nakuwa wafadhili walikubali kulipia usafiri,malazi na gharama zote za kongamano lililokuwa lifanyike huko Afrika Kusini, nchi zote zilifika katika kongamano la CIP AIRR, lakini uwakilishi wetu ulikosekana kwa kisingizio cha ruhusa kutopatikana, madhara yake Manispaa ya Kinondoni ikaondolewa kwenye programu ya kufadhiliwa huku nchi kama Ghana,Kenya,Zambia na nyinginezo zikifadhiliwa. Baada ya mkutano kuisha nchini Afrika Kusini, Katibu Mkuu kiongozi akaniandikia kibali cha kusafiri, baada ya kongamano kuisha na kukosa kiasi cha tshs Bilioni 1.3.

Kubwa lilofanya kuwatarifu nyinyi na umma juu ya hujuma hizi ni kitendo cha juzi alfajiri. Tukiwa tayari uwanja wa ndege kuanza safari ya mualiko wa kwenda nchini uturuki, ulio andaliwa na kufadhiliwa na ubalozi wa uturuki nchini Tanzania kwa ajili ya kukamilisha maongezi yaliyokwisha anza hapa Dar es salaam juu ya kusaidia kutatua chngamoto za ajira za vijana kwa miradi endelevu; ikiwemo mpango wa ujenzi wa chuo cha ufundi stadi kwa udhamini wa ubalozi wa uturuki,kupitia wafadhili wake.

Ubalozi wa Uturuki ulikuwa umedhamini safari ya Mameya kwenda Uturuki kukutana na wadau na wafadhili wa miradi mbalimbali ikiwemo ikiwemo Chuo Cha Ufundi ndani ya Manispaa ya Kinondoni, Ubalozi huo ulikuwa umeshatoa kibali cha kusafiri (Visa) na kugharamia fedha za usafiri, malazi, chakula na gharama zingine zote, ambapo matayarisho tu yali gharimu kiasi cha dola za kimarekani 42,000/=,sawa na shillingi millioni 88,kwa mameya wote wanne na mtendaji mmoja mmoja kutoka kila Halmashauri.

Safari pamoja na mkutano vilitakiwa kuanza tarehe 16 june mpaka 19 june 2016,huku wafadhili na wadau wetu wa maendeleo wakiandaa mialiko na wawekezaji na wafadhili kutoka sehemu mbali mbali za uturuki,kuja makao makuu ya nvhi hiyo,jiji la instanbul ulitarajiwa lakini Serikali imevunja Safari hiyo.

Kwa kufanya hivi Serikali imezikosesha Manispaa zetu fursa za Maendeleo ikiwemo Chuo hicho cha ufundi.

*Msimamo* wetu kwenye hili suala ni kutaka kujua:

• Je huo ndio msimamo rasmi wa viongozi wote wa serikali,?

• Tungependa kusikia Tamko kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kama maagizo haya ya kubana fedha na matumizi ya serikali yanahusianaje na safari za kufadhiliwa na nchi wahisani?

• Je hakuna namna ya kushirikiana na nchi rafiki kutupatia miradi ya Maendeleo?

Mwisho nimalizie kwa kusema sisi bado tuna imani ya kwamba hujuma hizi Mheshimiwa Rais hazifahamu ila isipokuwa baadhi ya viongozi wa serkali wanajaribu kuweka tafsiri tofauti ya sera ya kuzuia matumizi mabaya ya fedha kwenye safari za nje ya nchi.

Pamoja na kutumia vibaya agizo la Mheshimiwa Rais kuruhusu vibali vya viongozi katika mamlaka mbalimbali za serikali, Sisi tuna amini kuwa agizo la kuomba kibali maalumu ikulu halituhusu sisi (kama viongozi tusio watendaji), wala kutumia bajeti za serikali au halmashauri zetu kwenda kuonana na wadau wamaendeleo.

IMETOLEWA NA MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI.

BONIFACE JACOB.
IJUMAA 17/06/2016
 
Hizo wanaleta wenyewe ila hazifuatwi, wanajipendekeza wenyewe kuahidi. Hata za jamaa wangezileta nadhani kusingekuwa na tatizo.

Lakini mkuu shida ninayo ona hapa ni kuleta kibali late ilhali tarehe ya kusafiri imeandikwa kwenye form husika. Ni afadhali wangekataa kabisa kuliko uhuni waliomfanyia Meya
Ccm hawajiamini na wanachofanya
 
Nimesoma kwa makini lakini sijaona substance ya kutosha ku-justify malalamiko ya Meya wetu.

Hoja alizozitaja zote ni hoja nyepesi kabisa. Vikwazo hivyo vinahitaji mtu aliyekomaa kiuongozi tu ili ku-nevigate so easily. Dizaini kama watu washaanza kutafuta huruma kwa wananchi.

Swali langu kwa Meya wangu ni kwamba ina maana alitarajia ushirikiano "mkubwa" na unaostahili kutoka CCM na serikali yake?? Ina maana UKAWA walitarajia mteremko kwenye utendaji wao???? Kwanini Mameya wetu wa Dar hawajifunzi kutoka kwa Mameya wengine wenye uzoefu kutoka kwenye maeneo ambayo upinzani una uzoefu wa Umeya kwa muda mrefu kidogo hapa nchini Tanzania au hata kutoka nchi nyingine???

Wale wenzangu wanaoangalia kila jambo linaloletwa na chama chao kwa jicho la aina moja tu inabidi watuvumilie sisi wengine. Huwa sivutiwi kiutendaji hata chembe na mtu ambaye akikutana na changamoto zozote zile kwenye utendaji wake wa kila siku yeye anachofanya badala ya kuendelea kupambana kwa kuleta actionable and sustainable solutions, yeye analalamika na ku-transfer lawama za kushindwa kwake kwa watu wengine. Hii ni sifa ya watu weak na wanaofanikiwa kisanii sanii tu.

Wale waliokaribu na hawa viongozi wetu wa upinzani wawaambie ukweli. Lazima wabadilike. Strategy ya kulalamika inaweza isisaidie kila wakati. They ought to show strong leadership traits and practices to outshine the ruling wing (CCM). Wakiwa bold and strategic enough, CCM hawatakuwa na ujanja but to automatically give way. No shortcuts in my view....hii ya kulialia tena kwa hoja dhaifu ni strategy mfu kwa dunia ya sasa.
Misaada kwa wananchi ni hoja nyepesi? Shirikisha ubongo
 
Hii issue mbona Simple Tu, Omba Appointment ya kuonana na Mh. Raisi pale magogoni kisha mweleze hizi shida ulizozipata, kuweka post ndeeefu humu haitaweza kutatua hili tatizo bali itaonekana kuwa shida hii mnataka kuitumia kama mtaji wa kisiasa. Come on Tufanyeni kazi sasa.
Je unahuwakika huko kote Meya ajapita
 
Mapoooovu yooote kumbe ni kutaka kibali cha kusafiri nje ya Nje ukale bata! Akili ndogo haiiishi kulalamika aysee
 
Nina imani Mh. Rais hana taarifa hiyo, watendaji wengi ni wapuuzi badala ya kuangalia maslahi ya umma wao wanaleta siasa kwenye maisha ya wananchi, hayo ni majipu na nina uhakika Mh. Rais apatapo taarifa hizi atayatumbua haraka iwezekanavyo. Endelea kuwatumikia wananchi kaka usikate tamaa.
 
Kila mwananchi mwenye akili na anayejitambua alikwishaona hii serikali ya awamu hii imejaa maruweruwe. Wananchi washaanza kuichukia kama ikiendeleza upuuzi wa namna hii.
Kitu cha msingi na cha muhimu ni viongozi wa ukawa kwenda moja kwa moja ikulu kumuuliza mwenyewe mkulu kama ametoa baraka kwa upuuzi huo tunaofanyiwa wakazi.wa Dar tulioamua kutumia demokrasia yetu kuwachagua ukawa.
Aluta contínua!
 
Back
Top Bottom