Serikali tatu, CCM hoi mpaka UN

Serikali tatu, CCM hoi mpaka UN

upo sahihi mkuu.

Karume alikubali muungano kwa kuwa lilikuwa sharti la Nyerere ili apewe nchi ya Zanzibar kwani mganda ndo alieongoza mapinduzi wakati Karume alikuwa anakula urojo mchambawima

Duh! Kuuumbee!! Asante kwa taarifa kiongozi .
 
Tanzania Daima gazeti la Chadema,habari za kilaghai laghai,kutoka chama cha Kilaghai
 
hahaha Mtani umetudhihaki hapa...ila haina tabu...wa bara wengi huku kwetu sasa wamekua wateja wazuri wa Ulojo...tena wanakua wakali wasipoukuta...chezea znz weyeen!
 
Siitaji kuamini mnacho sema maana maisha kabla ya muungano sijui yalikuwaje kwa kutumia ufahamu wangu vijana wa kileo tumekuwa si wachujaji mambo hebu fikiria kama nyinyi wazazi wetu mnasema j.k nyerere aliiharibu nchi kwa vitu kamahivi c kweli kwani maisha ya kipindi kile ni tofauti sana na ya leo watu walikuwa hawana elimu ya kutosha mfano hai kipindi cha uongozi wa Abdu jumbe angeluwa si kiongozi makini sifahamu tungekuwa wapi pia kama sisi vijana wa leo ambao tunajulikana kama taifa la leo na si la kesho tungejivunia kitu gani tulicho kishikilia kwa miaka hamsini na kitu kwa upendo na ukarimu tusiwe wepesi wa kulaumu ila tunapaswa kujiuliza wapi penye ufa na tunapaziba au tujenge upya na tambua mawazo yako ila ukumbuke hao watanzani wa visiwani wakumbuke bila muungano wetu leo hii wasingekuwa walipo kwa usalama kwani asili ya visiwa hivyo ni mapinduzi je waliopindua hiyo inchi wote waliridhika na ugawji wa madaraka alioufanya mzee karume.kumbuka mapungufu yaliopo kwenye muungani ni mambo yanaowezekana kupatiwa ufumbuzi ila nimichezo michafu ya siasa za watu wachache wenye uloho wa madaraka na si masilahi ya Tanzania wala suala la katiba mpya jifunze kupitia manufaa tulionayo vijana leo tunapata fursa za kufanya biashara na kupata elimu ya vitendo kwa kwenda kujifunza zanzibar bila masharti.ahsanteni ni mimi kijana wenu joseph


umeaandika mengi na kuchanganyachanganya.

1. unaweza kutuambia kero za muungano tangu kuanza kwake zinapunguwa au zinaongezeka? kwanini..

2. Umeongelea uroho wa madaraka, tujadili hili kwa mifano halisi hapa chini

a) baada ya uhuru tulikuwa na mikowa mingapi na hivi sasa tunamikowa mingapi? kwanini

b) baada ya uhuru tulikuwa na wilaya ngapi nasasa tunawilaya ngapi? kwanini

tuanze nahayo kisha tutaendelea na mengine.
 
Tanzania Daima gazeti la Chadema,habari za kilaghai laghai,kutoka chama cha Kilaghai
Wewe pinga hoja usihangaike na karatasi, UN wamesema wao hawana kumbukumbu yeyote ya hati ya muungano wewe unamawazo gani UN waongo au?
 
Sasa hapa NJIA KUU sijui ni ipi na MCHEPUKO nao ni upi! Kwani mbona referundum huwa inatoa majibu yaliyo straight? Ya nn kupigizana kelele na kutafuta manyaraka ambayo hayakuwahi kutokea au kuandikwa.... Wafu hawahukumiwi...njia kuu itajulikana..
 
This is chasing shadows, blame game and never take responsibilities sickness..., kama aliyeharibu nchi ameshafariki, Je sasa nchi ni nzuri kuliko alivyokuwepo ? au nchi ilikuwa nzuri kabla hajaingia madarakani ? au kwanini isiwe nzuri sasa ameshaondoka ?

If you blame others for your failures, don't forget to credit them with your success

Utafananisha uzuri wa nchi ulivyo sasa hivi na wakati wa Nyerere?

I am so sure you were not there, otherwise usingebwabwaja hovyo humu.
 
halafu huwa najisikia vibaya wassira linavyoongelea muundo wa muungano.
unaweza kufikiri nae alichangia mawazo wakati wa kudisign muungano, kumbe ni limelishwa tu maneno kama roboti.
kama mpo wenye uelewa na matoleo ya binadam mnisaidie,
je huyu ndugu wassira ni binadam version gan?
 
Msigida

kuphenja ntoni weev??

kama wewe nimnyataru feki usiwahalibie wanyaturu wengine wenye ufaham kwa kuunga mkono upuuzi.

kipi alichokiandika Foxy cha maana kionekane cha maana zaidi ya mtazamo wake wa jicho la udin dhidi ya Mwal J K Nyerere?

Je nawewe upo kupinga legitimacy na weledi wa Nyerere kwa mtazamo huohuo?

Ndio maana CCm wanajisfia ngome yao ni Singida kwa matazamo kama wako,Kichwa kimejaa mahangahanga wewe,huo nao muungano wa serikali mbili!Yooo.wenyewe hawatutaki tunajipendekeza nini?Kwa kigezo cha usalama,tumepakana na nchi ngapi hadi Zenj iwe threat?Wana uchumi gani ambao tunalazimika jikomba kwao?
Funguka myampaa wan`g
 
halafu huwa najisikia vibaya wassira linavyoongelea muundo wa muungano.
unaweza kufikiri nae alichangia mawazo wakati wa kudisign muungano, kumbe ni limelishwa tu maneno kama roboti.
kama mpo wenye uelewa na matoleo ya binadam mnisaidie,
je huyu ndugu wassira ni binadam version gan?

Nafikiri ni Homoandriod kama sio Homowindow
 
Utafananisha uzuri wa nchi ulivyo sasa hivi na wakati wa Nyerere?

I am so sure you were not there, otherwise usingebwabwaja hovyo humu.
Faiza tunaomba msimamo wako kuhusu muungano. Mbili au tatu au usiwepo kabisa?
 
Utafananisha uzuri wa nchi ulivyo sasa hivi na wakati wa Nyerere?

I am so sure you were not there, otherwise usingebwabwaja hovyo humu.

uzuri wa nchi kwako ni nini ? magari, majengo au nini ? Alafu lazima ufanye correlation kati ya wakati muda na mapato, ndio useme walichokifanya walioleta uhuru kama ni kuharibu au kutengeneza kulinganisha kilichofanyika baada ya wenyewe kuondoka, na rasilimali zilizotumika na kupotea (madini, viwanda n.k.)

Its true Rome was not built in a day..., lakini it did not take a lifetime wala sio kupiga reverse..., swali sio kujiuliza tuna nini sasa tangia tupate uhuru bali ni je tulichonacho kinatosha na kama hakitoshi je sababu ni Marehemu aliyeshaondoka na kuwaachia wengine waendelee ? Sio kwamba kila alichofanya lazima mkifanye na kama mnakifanya na mnaona hakifai makosa sio yake bali ni yenu na blind faith...
 
Utafananisha uzuri wa nchi ulivyo sasa hivi na wakati wa Nyerere?

I am so sure you were not there, otherwise usingebwabwaja hovyo humu.
Fix
Usiwe kigeugeu.Tunajua ww ni muumini wa CCM na mpiga debe wa Sirikali 2!Mbona wapingana na chama chako?
Tunaposema Serikali 3 ndio mwafaka lazima mkubali kuwa Muungano tulionao wa 2 ni kiini macho tu!
 
Fix
Usiwe kigeugeu.Tunajua ww ni muumini wa CCM
Kwenye Mambo ya Muungano hakuna CCM wanaotaka Serikali 3?
Wazanzibar wote wa CCM wamekuambia wanataka serikali mbili?
Mjumbe alazimishwa kupiga kura ya wazi - Mzalendo.net
1493-254x134.jpg

Al- Shymaa Kweigyir Amwaga machozi baada ya kuzomewa, kuitwa msaliti
FaizaFoxy msimuhukumu wapo wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka CCM ambaye ni kati ya akina Lembeli Filikunjombe, Lugola na wengineo alionesha ujasiri wa kugomea Serikali 2
kwani hata maalim Sharif kasema km CCM hataki mbili basi wao hizo zote hawazitaki ila wanataka Muungano wa Katiba tu.
Na mm namuunga mkono Wazanzibar wapeni Kisiwa chao acheni LONGOLONGO ya Serikali 1 au 2 au 3
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom