Serikali pigeni marufuku pombe nchini

Serikali pigeni marufuku pombe nchini

Waulize Qatar Airways walipotaka kupiga pombe marufuku ktk ndege zao walikutana na nini? Maendeleo Nchi hii hayaji kwaajili ya ccm sio pombe. Ni nchi gani duniani ilipiga pombe marufuku kwa muda na ikapata maendeleo?
 
Na hao wanaofanya kaz kutokana na pombe umewahesabu?

Wauza bar, wauza maduka,
Wazalishaji n.k

Au hizo siyo kazi?
 
Kwakuwa nchi yetu bado changa kiuchumi ni bora Serikali ingepiga marufuku uuzwaji wa pombe nchini ili watu wafanye kazi. Watu wengi wanashindwa kumudu majukumu mbalimbali kutokana na unywaji wa pombe, hivyo hupelekea kutokufika malengo yaliyokusudiwa.

Hivyo ushauri wangu kwa Serikali ipige marufuku unywaji wa pombe kwa raia wake na ipige marufuku uuzwaji pia utengenezaji wa pombe hapa nchini. Ipige marufuku hata kwa muda wa miaka 10 - 15 hivi

Nawasilisha.
Kwakupitia bandiko lako hili inaonesha ni kiasi gani u mbumbumbu kuhusiana na maswala ya uchumi.
Unajua serikali inakusanya kiasi gani cha mapato toka kwenye kampuni za vinywaji especially pombe hapa nchini? Kwakukufumbua macho tu kidogo: kuna bidhaa mahitaji yake yapo kwasababu ya mazoea (demand by habit) Yaani demand yake inapanda kadri unavyoitumia hiyo bidhaa na ukishaizoea hata bei yake iongezeke kiasi gani we utainunua tu. Sasa serikali inapandisha kodi ya hizo bidhaa na makampuni ili yaweze kupata faida nayo yanapandisha bei nawe mtumiaji utanunua tu. Serikali inakusanya mapato mengi kutoka kwenye kampuni zinazozalisha aina hizo za bidhaa na pombe ikiwa moja wapo.
So ili serikali iweze kujiendesha na kukuhudumia wewe na mimi na Jamii kwa ujumla kwa kutupatia huduma muhimu kama miundombinu, elimu bora, huduma bora za kiafya n.k ni lazima ipate mapato yakutosha na chanzo kimoja cha mapato ni kama hapo juu nilivyoelekeza.
Natumai umeelewa sasa
 
Najua....Ila madhara yake ni makubwa kuliko faida
Kwetu mahari ni pombe, ndoa lazima pombe iwepo, mtoto akizaliwa anapewa kakonyagi ili kutuliza tumbo, misiba yote bila pombe ni kwisheni. Shughuli zote bila pombe ni bure heri msipike chakula. Watu wanatoka nyumbani wameshiba ili wajipatie raha zao. Ngoma na pombe ndo raha ya kwetu.

Wewe na ukoo wako kaa mbali na pombe ila usiwaeleze watu wengine sababu hata harusi ya Kanaan Yesu alitengeneza mvinyo hivyo hata tunakommunica mvinyo. Ukae na lako moyoni na ukoo wako basi.
 
Back
Top Bottom