BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Date::12/10/2008
Huduma za ndege ATCL zasitishwa ndani, nje ya nchi
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL), ambalo limekuwa na matatizo makubwa tangu ndoa yake ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) ivunjike, limenyanganywa cheti cha kuruka angani na Mamlaka ya Anga (TCAA) baada ya kukosa viwango vya ubora kuruka angani.
Taarifa kutoka ndani ya ya ATCL zimeeleza kuwa shirika hilo limenyanganywa cheti hicho tangu Desemba 8 mwaka huu na hivyo litashindwa kusafirisha abiria hadi hapo litakapokidhi masharti ya usalama wa anga na kurejeshewa cheti hicho.
Miongoni mwa viwango hivyo vya usalama ni ukaguzi wa mara kwa mara wa ndege zake, kuwa na wataalamu wa kutosha kama marubani na wahandisi, vitu ambavyo vimeonekana kukosekana kwenye shirika hilo la serikali.
Kufungiwa huko kumekuja huku kukiwa na uwezekano wa shirika hilo kufungiwa na Chama cha Kimataifa cha Usafiri wa Anga (IATA) kufanya safari zake baada ya kubaini zaidi ya makosa 500.
Mwishoni mwa wiki iliripotiwa kuwa ATCL ilikaguliwa mwezi Oktoba na kubainika na makosa hayo ya usafiri wa anga, lakini ikashindwa kuyarekebisha na ndipo IATA ilipoanza mchakato wa kutaka kuizuia kufanya safari.
Ni kweli ATCL imenyanganywa cheti cha viwango kwa kukosa ubora wa kuruka angani hivyo haitafanya safari za nje wala ndani ya nchi, alisema mmoja wa watu wa ndani TCAA alipohojiwa na Mwananchi.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, ndege za ATCL zilizokuwa zikifanya safari zake ndani na nje ya nchi haitaweza kufanya tena safari hizo na vigogo wa ATCL jana walikuwa na vikao na TCAA kuzungumzia suala hilo.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo katibu mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo alisema hana taarifa kuhusu kunyanganywa cheti kwa ATCL na kudai kuwa mkurugenzi wa shirika hilo, David Mataka ndiye anayeweza kueleza suala hilo.
Sina taarifa kuhusu suala hilo... hayo ni mambo ya ATCL na anayeweza kukueleza ni Mataka, hivyo wasiliana naye... haiwezekani toka tarehe nane hadi leo mimi sijui, alisema Chambo.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mataka alisema taarifa hizo si za kweli na kwamba wako kwenye kikao na watu wengine na si TCAA kama habari zilivyoeleza awali.
Mataka alisema taarifa hizo ni za uzushi na zinatokana na habari zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuhusu matatizo ya shirika hilo ambalo hivi karibuni lilishindwa kusafirisha abiria wake kwenda Afrika Kusini.
Taarifa hizo ni za uzushi, na hivi sasa niko kwenye kikao na watu wengine na si TCAA, alisema Mataka.
Mwananchi ilipojaribu kuwasiliana na TCAA, ilithibitishiwa habari hizo kuwa ATCL imezuiwa kufanya safari zake za ndani na nje.
ATCL imekuwa ikitegemewa sana kwa safari za mikoa ya kusini, kaskazini, Kanda ya Ziwa, Zanzibar na safari za Afrika Kusini, ambako katika siku za karibuni safari za kusini mwa Afrika zimekuwa na matatizo makubwa kiasi cha wasafiri kukwama kwa siku kadhaa jijini Dar es salaam.
Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi uliopita, ATCL ilikuwa na ndege mbili tu zilizokuwa zikifanya kazi, kati ya ndege zake tano na udhaifu huo ulilifanya shirika hilo lipoteze wateja wake wengi wa safari za Mwanza-Dar es salaam na Dar es salaam-Johannesburg.
Serikali imekiri kuwepo na tatizo kubwa la kuliendesha shirika hilo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwaambia wahariri wa vyombo vya habari katika mkutano wake wa Novemba 24 kuwa serikali itafanyia kazi matatizo hayo.
Alisema kuwa suala hilo amekaa nalo na atashughulikia na ili shirika hilo liweze kusimama na kujiendesha.
Huduma za ndege ATCL zasitishwa ndani, nje ya nchi
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL), ambalo limekuwa na matatizo makubwa tangu ndoa yake ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) ivunjike, limenyanganywa cheti cha kuruka angani na Mamlaka ya Anga (TCAA) baada ya kukosa viwango vya ubora kuruka angani.
Taarifa kutoka ndani ya ya ATCL zimeeleza kuwa shirika hilo limenyanganywa cheti hicho tangu Desemba 8 mwaka huu na hivyo litashindwa kusafirisha abiria hadi hapo litakapokidhi masharti ya usalama wa anga na kurejeshewa cheti hicho.
Miongoni mwa viwango hivyo vya usalama ni ukaguzi wa mara kwa mara wa ndege zake, kuwa na wataalamu wa kutosha kama marubani na wahandisi, vitu ambavyo vimeonekana kukosekana kwenye shirika hilo la serikali.
Kufungiwa huko kumekuja huku kukiwa na uwezekano wa shirika hilo kufungiwa na Chama cha Kimataifa cha Usafiri wa Anga (IATA) kufanya safari zake baada ya kubaini zaidi ya makosa 500.
Mwishoni mwa wiki iliripotiwa kuwa ATCL ilikaguliwa mwezi Oktoba na kubainika na makosa hayo ya usafiri wa anga, lakini ikashindwa kuyarekebisha na ndipo IATA ilipoanza mchakato wa kutaka kuizuia kufanya safari.
Ni kweli ATCL imenyanganywa cheti cha viwango kwa kukosa ubora wa kuruka angani hivyo haitafanya safari za nje wala ndani ya nchi, alisema mmoja wa watu wa ndani TCAA alipohojiwa na Mwananchi.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, ndege za ATCL zilizokuwa zikifanya safari zake ndani na nje ya nchi haitaweza kufanya tena safari hizo na vigogo wa ATCL jana walikuwa na vikao na TCAA kuzungumzia suala hilo.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo katibu mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo alisema hana taarifa kuhusu kunyanganywa cheti kwa ATCL na kudai kuwa mkurugenzi wa shirika hilo, David Mataka ndiye anayeweza kueleza suala hilo.
Sina taarifa kuhusu suala hilo... hayo ni mambo ya ATCL na anayeweza kukueleza ni Mataka, hivyo wasiliana naye... haiwezekani toka tarehe nane hadi leo mimi sijui, alisema Chambo.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mataka alisema taarifa hizo si za kweli na kwamba wako kwenye kikao na watu wengine na si TCAA kama habari zilivyoeleza awali.
Mataka alisema taarifa hizo ni za uzushi na zinatokana na habari zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuhusu matatizo ya shirika hilo ambalo hivi karibuni lilishindwa kusafirisha abiria wake kwenda Afrika Kusini.
Taarifa hizo ni za uzushi, na hivi sasa niko kwenye kikao na watu wengine na si TCAA, alisema Mataka.
Mwananchi ilipojaribu kuwasiliana na TCAA, ilithibitishiwa habari hizo kuwa ATCL imezuiwa kufanya safari zake za ndani na nje.
ATCL imekuwa ikitegemewa sana kwa safari za mikoa ya kusini, kaskazini, Kanda ya Ziwa, Zanzibar na safari za Afrika Kusini, ambako katika siku za karibuni safari za kusini mwa Afrika zimekuwa na matatizo makubwa kiasi cha wasafiri kukwama kwa siku kadhaa jijini Dar es salaam.
Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi uliopita, ATCL ilikuwa na ndege mbili tu zilizokuwa zikifanya kazi, kati ya ndege zake tano na udhaifu huo ulilifanya shirika hilo lipoteze wateja wake wengi wa safari za Mwanza-Dar es salaam na Dar es salaam-Johannesburg.
Serikali imekiri kuwepo na tatizo kubwa la kuliendesha shirika hilo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwaambia wahariri wa vyombo vya habari katika mkutano wake wa Novemba 24 kuwa serikali itafanyia kazi matatizo hayo.
Alisema kuwa suala hilo amekaa nalo na atashughulikia na ili shirika hilo liweze kusimama na kujiendesha.