Serikali msiwakomoe wanunuzi wa korosho

Serikali msiwakomoe wanunuzi wa korosho

Namichiga

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2017
Posts
356
Reaction score
554
Katika vyombo vingi vya habari limetawala sakata la ukaguzi wa maduka ya kubadili fedha za kigeni,sakata ambalo limeleta taharuki kwa kuwa limehusisha jeshi la ulinzi (JW). Nyuma ya pazia kuna fununu!
Makampuni mengi yaliyojisajili kwa manunuzi ya korosho hapa Tanzania, mfano Afrisian, Export ,Olam, Alpha, Alpha Choice, Alpha Crust,Viikat,Alpha na Mata, Mkemi Agrix,Maviga na mengineyo mengi ni madalali (agents).Makampuni haya huingia makubaliano ya kuyanunulia korosho makampuni kutoka India, Vietnam ,Singapore na kwengineko duniani.

Hivyo basi bodi ya korosho Tanzania (CBT) inapotangaza ratiba ya manunuzi ya korosho kwenye minada,makampuni haya huanza kuingiziwa fedha na makampuni hayo ya nje kwa ajili ya manunuzi.

Hivyo basi kwa mwaka huu mpaka wakati serikali inatangaza kufuta leseni za ununuzi wa korosho,makampuni mengi tayari yalishakua na pesa za watu. Na kwakua biashara hakuna basi inawapasa kurudisha.
Lakini kilicho cha ajabu,hakuna zoezi gumu kwa sasa kama kutuma pesa za kigeni nje ya nchi. Lengo likiwa ni kuyakomoa makampuni yote yaliyotaka kununua korosho,kwani pesa zinahitajika zikafanye manunuzi ya korosho kwenye nchi nyingine lakini hazitoki.

Rai yangu kwa serikali kama raia mwema, figisu hizi zikizidi tutafukuza wawekezaji. Makampuni haya japo tumeshindwa kupata muafaka wa manunuzi ya korosho lakini bado tunawategemea kwenye manunuzi ya Ufuta, Dengu,Girigiriani,Choroko na mazao mengine.
 
ni kama sijakuelewa ugumu wa kutuma fedha uko vipi wakati taratibu ziko wazi kabisa tena kwa maandishi
Masharti yamekua magumu mno kwenye mabenki,hivyo wanasaka na kwengineko!. Na ili kutisha basi mpaka jeshi linatumika!
 
Mimi sio mwanasiasa ni mdau wa sekta ya mazao tu,wakinijibu kisiasa wanakosea.Uchumi unaanguka huu!!
Ndiyo hivyo tena !! Tusubiri kama utapewa majibu ya ki taalamu [emoji23][emoji1787][emoji850][emoji40]
 
Hizo zinazoanza na Alpha zote ni kampuni ,dhumuni la kuweka masharti magumu ni kuwakomoa kwanini walikataa kununua korosho kwa bei aliyosema mzee!
Kama hizo hela ziliingia kwenye masandarusi sawa.
Lakini kama ni through bank haina tabu zinarudi tu
Halafu mbona Alpha nyingi walikosa majina au
 
Siku zote uzalendo si kukaa kimya tu,hata kusema pale mtu anapotuumiza ni uzalendo pia.We waache washangilie lakini tunaumia sote.
uzalendo wa kusemasema sasa unaweza hata kukufanya uthibitishwe kuwa adui no.4 wa taifa
 
uzalendo wa kusemasema sasa unaweza hata kukufanya uthibitishwe kuwa adui no.4 wa taifa
Basi ngoja tukae kimya lakini korosho haijawahi kumuacha mtu salama,wangemuuliza JK ilimfanya nini mpaka akaikimbia.Hao tunaowaletea ubabe ndio wenye sauti kwenye makampuni mengi ya nje,twendeni Guine Bissau tukaulize kilichowakuta!
 
Weka masharti yaliyoongezwa yanayofanya utumaji wa pesa nje ya nchi kuwa mgumu kama hauna hizi ni ngonjera za wamama wa TAMWA huna jipya.
Halafu unabidi ujue hii ni operation ya tatu je zile mbili za mwanzo zilimlenga nani?
Kama mtu ameingiza hela yake kihalali nani wa kumsumbua anapotaka kuituma nje ya nchi?
Wapiga dili awamu hii mtapiga kelele za kila rangi but in vain.
 
Weka masharti yaliyoongezwa yanayofanya utumaji wa pesa nje ya nchi kuwa mgumu kama hauna hizi ni ngonjera za wamama wa TAMWA huna jipya.
Halafu unabidi ujue hii ni operation ya tatu je zile mbili za mwanzo zilimlenga nani?
Kama mtu ameingiza hela yake kihalali nani wa kumsumbua anapotaka kuituma nje ya nchi?
Wapiga dili awamu hii mtapiga kelele za kila rangi but in vain.
Na mimi nashangaa
Yaani kelele tutazisikia sana na kila jiwe likitupwa lazima limpate mtu hahaha
 
[emoji41][emoji41][emoji41]
tapatalk_jpeg_1542131910472.jpeg
 
Back
Top Bottom